Traffic / fire: Sticker za fire za station wagon kuuzwa 20,000, na saloon 5,000 why?

Elly-The Tishbite

New Member
Oct 29, 2012
3
0
Hivi karibuni baada ya kupata usumbufu wa traffic polisi kudai sticker za fire pamoja na kuonyesha mtungi wa fire extinguisher niliamua kwenda kupeleka mtungi ule kukaguliwa ili nipate sticker. Afisa mkaguzi akaniambia nitoe 20,000 nikakumbuka mara ya mwisho nilikata kwa 5000. Nilipouliza kulikonimajibu ni kuwa magari ya station wagon ndio 20000 na saloon 5,000. Ukichunguza unakuta mitungi inayotumika ni size moja, uzito wa injini ni cc sawa, idadi ya passangers ni moja. Hoja hapa ni mamlaka ipi imepanga bei hizo za stika? na jukumu la serikali ni kufanya biashara au kutoa huduma? kuna act yoyote iliyoipa idhini Idara ya Zimamoto kufanya biashara hivyo? Mbona ukaguzi wa traffic polisi unaotoa sticker za Road Worthness ni tsh 3000/ ambazo kimsingi ni kama gharama za printing? Naomba ushauri kwa sababu nataka kuipeleka mbele zaidi-bungeni au mahakamani
 
Hivi karibuni baada ya kupata usumbufu wa traffic polisi kudai sticker za fire pamoja na kuonyesha mtungi wa fire extinguisher niliamua kwenda kupeleka mtungi ule kukaguliwa ili nipate sticker. Afisa mkaguzi akaniambia nitoe 20,000 nikakumbuka mara ya mwisho nilikata kwa 5000. Nilipouliza kulikonimajibu ni kuwa magari ya station wagon ndio 20000 na saloon 5,000. Ukichunguza unakuta mitungi inayotumika ni size moja, uzito wa injini ni cc sawa, idadi ya passangers ni moja. Hoja hapa ni mamlaka ipi imepanga bei hizo za stika? na jukumu la serikali ni kufanya biashara au kutoa huduma? kuna act yoyote iliyoipa idhini Idara ya Zimamoto kufanya biashara hivyo? Mbona ukaguzi wa traffic polisi unaotoa sticker za Road Worthness ni tsh 3000/ ambazo kimsingi ni kama gharama za printing? Naomba ushauri kwa sababu nataka kuipeleka mbele zaidi-bungeni au mahakamani


Ninavyojua kwa sasa ukienda kurenew road licence unalipia na stika za fire. Kwa magari yasiyozidi CC 2000 unalipa 30,000/= na unapewa risiti na TRA. Ukitoka na risiti yako TRA unaenda nayo fire ukiwa na mtungi wa wako wa gas wanaukagua na kama wakiuona u mzima wanakupa stika bila malipo. Kama una matatizo wanautengeneza ila sijajua ni kwa gharama za nani.

Sina uhakika kama huu utaratibu umebadilika tena ila najua umeanza kutumika toka julai mwaka huu.
 
  • Thanks
Reactions: Paw
Sticker haiuzwi ukienda lipa road license unalipia na mambo ya fire wenyewe watakagua extinguisher yako na watakupa sticker angalia usitapeliwe ndugu yangu .........................!:bowl::nimekataa
 
Serikali ya CCM inatumia mbinu nyingi kuwakamua wananchi. Na hii ndiyo sababu umasikini hautaisha. Kodi hii ya mitungi na hata motor vehicle licence ni kero na ni namana nyingine serikali hii dhalimu inavyowakomoa raia wake maskini.
 
Sticker haiuzwi ukienda lipa road license unalipia na mambo ya fire wenyewe watakagua extinguisher yako na watakupa sticker angalia usitapeliwe ndugu yangu .........................!:bowl::nimekataa
Ndo sera ilivyo kwasasa lakini mkuu nikwambie kuwa hili halitekelezwi kwa mujibu wa utaratibu, nilikwenda kukata Road Licence, na baada ya hapo nikapeleka mtungi na hao jamaa wa TRA walinambia "kwasasa hatuna sticker njoo baadaye. Nimekwenda baadaye hola, nimekaa mwezi mzima na niliporudi hakuna. Juzi nimempeleka ndugu yangu naye akakate road licence na nkaulizia sticker za fire HOLA. Tangu 28 June 2012 hadi leo sijapata kabisa hiyo sticker. Mbaya zaidi polisi katika wilaya moja hapa nchini walikuwa wanakagua vyombo vya usafiri katika wiki ya nenda kwa usalama lakini hawakuwa na zile stickers za nenda kwa usalama. wizi mtupu na hii ninaisema kutokana na uzoefu wangu mimi mwenyewe!!!!
 
Back
Top Bottom