Elly-The Tishbite
New Member
- Oct 29, 2012
- 3
- 0
Hivi karibuni baada ya kupata usumbufu wa traffic polisi kudai sticker za fire pamoja na kuonyesha mtungi wa fire extinguisher niliamua kwenda kupeleka mtungi ule kukaguliwa ili nipate sticker. Afisa mkaguzi akaniambia nitoe 20,000 nikakumbuka mara ya mwisho nilikata kwa 5000. Nilipouliza kulikonimajibu ni kuwa magari ya station wagon ndio 20000 na saloon 5,000. Ukichunguza unakuta mitungi inayotumika ni size moja, uzito wa injini ni cc sawa, idadi ya passangers ni moja. Hoja hapa ni mamlaka ipi imepanga bei hizo za stika? na jukumu la serikali ni kufanya biashara au kutoa huduma? kuna act yoyote iliyoipa idhini Idara ya Zimamoto kufanya biashara hivyo? Mbona ukaguzi wa traffic polisi unaotoa sticker za Road Worthness ni tsh 3000/ ambazo kimsingi ni kama gharama za printing? Naomba ushauri kwa sababu nataka kuipeleka mbele zaidi-bungeni au mahakamani