TRAFFIC ENGINEERING: Ni vigezo gani huzingatiwa katika kufanya maamuzi ya kufunga "traffic lights" au kuweka "roundabout" kwenye makutano ya barabara?

Infantry Soldier

JF-Expert Member
Feb 18, 2012
15,893
16,317
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wote wa hapa jamiiforums.

Ndugu zangu watanzania (Traffic Engineers) eti;

Ni vigezo gani vya kitaalam huzingatiwa na engineers katika kufanya maamuzi ya kufunga "traffic lights" au kuweka "roundabout" kwenye makutano ya barabara za mijini?

images (8).jpg


(1) Kama kigezo ni upatikanaji wa umeme, mbona Dar umeme upo karibia sehemu nzima ya jiji na bado kuna round abouts?

(2) Kama issue ni wingi wa magari, mbona maeneo ya city center kama vile mtaa wa Samora, Sanamu ya askari kuna gari nyingi na bado hakuna traffic lights?

NINAOMBA KUELIMISHWA: Ni vigezo gani huzingatiwa katika kufanya maamuzi haya?

NB: Kwanini "traffic lights" zisiwe na remote controllers ili kuipunguzia kazi mikono ya askari? Wataam wa ICT hapo DIT kwani hili haliwezekani?

3-dar-traffic.jpg


USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
 
Na kwa maswali hayo hayo, ni vigezo gani huzingatiwa kuwekwa Kwa "flyovers/interchanges"
 
Chato kuna trafic light na foleni hakuna so sometimes ni mapambo tu kunogesha mandhari
 
Mkuu, itapendeza zaidi kama vichwa vya mabandiko yako uwe unavifanya vifupi.
Jamiiforums ina members zaidi ya 500,000 hivyo siwezi kumfurshisha kila mtu humu. Ninaomba uniwie radhi sana kama jibu langu litakuwa limekukwaza.
 
Kuna mambo kadhaa ya kuzingatia katika selection ya machaguzi hayo mawili, Traffic Lights Vs Roundabouts;

1. Swala la capacity ya magari lazima lizingatiwe katika kuangalia whether kufanya traffic lights installation au kuweka roundabout. Mfano kama magari ni mengi mno, like zaidi 2500vph(vehicles per hour) katika eneo husika, na ni more than single/double lane huwezi kuweka roundabout coz drivers' behaviours zitasababisha jam tu lazima.

2. Safety ya waendesha magari, waendesha pikipiki, waenda kwa miguu pia muhimu izingatiwe, kuna sehemu ukiweka roundabouts utaumiza sana wavuka barabara kwa miguu coz hakuna kusubiriana, speed limits zaweza kuwa kubwa hivyo ni hatari kwa wanaovuka barabara.

3. Muda wa kusubiri(delay time), intensity ya magari yanayopita, muda yanayotakiwa kusubiri ili taa ziruhusu pia ni kigezo cha kuzingatia. Ndio maana sehemu nyingi zenye traffic lights usiku zinaruhusu magari yapite kwa "uangalifu" bila kuzingatia taa coz kwa mahesabu yaliyofanywa waliona intensity ya magari usiku ni ndogo.

4. Lane moja au mbili ni bora zaidi kuwa na roundabout kuliko lanes nyingi. Lanes nyingi utalazimika kuweka circle kubwa ili kufanya magari yanayozunguka yawe mengi which in the end inaweza leta msongamano.

Chukulia mfano wa makutano ya Sam Nujoma na Bagamoyo road, ukiweka roundabout pale ni majanga, unless iwe circle kubwa sana ili iwe na uwezo wa ku accommodate magari mengi, lakini in the end lazima kutakuwa na msongamano, maeneo kama askari monument it's a matter of choice.

...my two cents though sio engineer
 
Kuna mambo kadhaa ya kuzingatia katika selection ya machaguzi hayo mawili, Traffic Lights Vs Roundabouts;

1. Swala la capacity ya magari lazima lizingatiwe katika kuangalia whether kufanya traffic lights installation au kuweka roundabout. Mfano kama magari ni mengi mno, like zaidi 2500vph(vehicles per hour) katika eneo husika, na ni more than single/double lane huwezi kuweka roundabout coz drivers' behaviours zitasababisha jam tu lazima.

2. Safety ya waendesha magari, waendesha pikipiki, waenda kwa miguu pia muhimu izingatiwe, kuna sehemu ukiweka roundabouts utaumiza sana wavuka barabara kwa miguu coz hakuna kusubiriana, speed limits zaweza kuwa kubwa hivyo ni hatari kwa wanaovuka barabara.

3. Muda wa kusubiri(delay time), intensity ya magari yanayopita, muda yanayotakiwa kusubiri ili taa ziruhusu pia ni kigezo cha kuzingatia. Ndio maana sehemu nyingi zenye traffic lights usiku zinaruhusu magari yapite kwa "uangalifu" bila kuzingatia taa coz kwa mahesabu yaliyofanywa waliona intensity ya magari usiku ni ndogo.

4. Lane moja au mbili ni bora zaidi kuwa na roundabout kuliko lanes nyingi. Lanes nyingi utalazimika kuweka circle kubwa ili kufanya magari yanayozunguka yawe mengi which in the end inaweza leta msongamano.

Chukulia mfano wa makutano ya Sam Nujoma na Bagamoyo road, ukiweka roundabout pale ni majanga, unless iwe circle kubwa sana ili iwe na uwezo wa ku accommodate magari mengi, lakini in the end lazima kutakuwa na msongamano, maeneo kama askari monument it's a matter of choice.

...my two cents though sio engineer
Umejitahidi kwa mbaaaaaali kijana wangu
 
Kwa nini umeweka picha za daslam peke yake ?
Hata sisi huku mikoani tunakaa kusubiri kama zitakuja lakini haziji sijui sisiem mnamatatizo gani yaani.
 
Sijawahi kuona Tanzania taa kwenye mzunguko, ila niliona Nairobi mimi mwenyewe nilishangaa, ...
 
Inategemea nani yuko madarakani, waziri wa fedha nani na waziri wa ujenzi nani. Hivi kwa akili yako ya std 1 unaweza kufanya maamuzi ya kujenga uwanja wa kimataifa chato badala ya kupanua wa mwanza na kuweka taa ule wa Mbeya ambao ndege hazitui usiku kwa kukosa taa?. Utaalamu ni ulaya sio afrika.
 
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wote wa hapa jamiiforums.

Ndugu zangu watanzania (Traffic Engineers) eti;

Ni vigezo gani vya kitaalam huzingatiwa na engineers katika kufanya maamuzi ya kufunga "traffic lights" au kuweka "roundabout" kwenye makutano ya barabara za mijini?

View attachment 1659332

(1) Kama kigezo ni upatikanaji wa umeme, mbona Dar umeme upo karibia sehemu nzima ya jiji na bado kuna round abouts?

(2) Kama issue ni wingi wa magari, mbona maeneo ya city center kama vile mtaa wa Samora, Sanamu ya askari kuna gari nyingi na bado hakuna traffic lights?

NINAOMBA KUELIMISHWA: Ni vigezo gani huzingatiwa katika kufanya maamuzi haya?

NB: Kwanini "traffic lights" zisiwe na remote controllers ili kuipunguzia kazi mikono ya askari? Wataam wa ICT hapo DIT kwani hili haliwezekani?

View attachment 1659334

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Iko hivi, traffic control kwenye intersections ina stages, inategemea na idadi ya magari yanayopita,
1. ile ambayo haina control yoyote, au tuiite gombania goli, hii hua sehemu zenye volume ndogo
2. ikizidiwa ya kwnza inayofata ni round about,
3 ikizidiwa ndo tunaweka traffic lights
4 .stage ya mwisho baada ya hizo zote ni grade separation, kwa maana ya underpass au overpass.
Though some stages might be skipped kutokana na mahitaji ya eneo husika.
 
Iko hivi, traffic control kwenye intersections ina stages, inategemea na idadi ya magari yanayopita,
1. ile ambayo haina control yoyote, au tuiite gombania goli, hii hua sehemu zenye volume ndogo
2. ikizidiwa ya kwnza inayofata ni round about,
3 ikizidiwa ndo tunaweka traffic lights
4 .stage ya mwisho baada ya hizo zote ni grade separation, kwa maana ya underpass au overpass.
Though some stages might be skipped kutokana na mahitaji ya eneo husika.
Umejitahidi sana mkuu
 
Back
Top Bottom