TRA yagawa mashine za EFD kwa makatibu wa Wizara

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,395
Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) imegawa Mashine za kukusanyia mapato za Kieletroniki za EFD zipatazo tano kwa kila katibu Mkuu wa Wizara kwa ajili ya kuzitumia kukusanya maduhuli ya serikali.

Hatua hiyo imetokana na agizo la Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ya kutaka Wizara zinazotoa huduma ziwe na mashine za EFD ili kuweza kujiletea maendeleo na kukuza uchumi wa taifa. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Kamishna Mkuu wa TRA, Alphayo Kidata amesema kuwa ugawaji wa mashine hizo kwa taasisi za serikali zitasaidia kutunza kumbukumbu katika kupanga maduhuli.

Aidha amesema mashine hizo ni mashine za kwanza katika mashine zote kutokana na kuwa za kisasa katika kutunza kumbukumbu za huduma ambazo wanazitoa. Kamishna wa Mapato ya Ndani wa TRA, Ellijah Mwandumbya amesema kuwa watawafundisha wakuu wa idara hizo jinsi ya kuzitumia.
 
Kwa Magufuli kila goti litapigwa.

Pia hamna jiwe litakalobaki bila kugeuzwa
 
  • Thanks
Reactions: MTK
Sasa ninavyojua EFD ni kwa ajili ya kukusanyia kodi i.e. ni kwa walipa kodi wenye TIN number na waliojisajili na VAT.
Swali langu hapa ni je, hizi taasisi zimejisajili na VAT na zina TIN number!?
Je, hizi taasisi nazo ni 'walipa kodi'?
Hapa ndio nashangaa hata traffic kutengeneza namba za Tigo/M-Pesa nk kwa ajili ya kukusanyia penalty za barabarani!
 
Sasa ninavyojua EFD ni kwa ajili ya kukusanyia kodi i.e. ni kwa walipa kodi wenye TIN number na waliojisajili na VAT.
Swali langu hapa ni je, hizi taasisi zimejisajili na VAT na zina TIN number!?
Je, hizi taasisi nazo ni 'walipa kodi'?
Hapa ndio nashangaa hata traffic kutengeneza namba za Tigo/M-Pesa nk kwa ajili ya kukusanyia penalty za barabarani!

Mkuu unajua maana ya maduhuli?
 
hapana sijui na ndio maana comment yangu iko kwenye maswali, hebu nipe mwanga katika hilo.
Nimemjibu mdau hapo juu kuwa maduhuli ni revenue, na pesa yote inayokusanywa na serikali kutoka kwenye taasisi na idara zake ni revenue.
 
Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) imegawa Mashine za kukusanyia mapato za Kieletroniki za EFD zipatazo tano kwa kila katibu Mkuu wa Wizara kwa ajili ya kuzitumia kukusanya maduhuli ya serikali.

Hatua hiyo imetokana na agizo la Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ya kutaka Wizara zinazotoa huduma ziwe na mashine za EFD ili kuweza kujiletea maendeleo na kukuza uchumi wa taifa. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Kamishna Mkuu wa TRA, Alphayo Kidata amesema kuwa ugawaji wa mashine hizo kwa taasisi za serikali zitasaidia kutunza kumbukumbu katika kupanga maduhuli.

Aidha amesema mashine hizo ni mashine za kwanza katika mashine zote kutokana na kuwa za kisasa katika kutunza kumbukumbu za huduma ambazo wanazitoa. Kamishna wa Mapato ya Ndani wa TRA, Ellijah Mwandumbya amesema kuwa watawafundisha wakuu wa idara hizo jinsi ya kuzitumia.
i
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom