TUNTEMEKE
JF-Expert Member
- Jun 15, 2009
- 4,587
- 579
Katika hali ambayo sikuweza kuiamini, ni pale nilipoikuta treni iliyokua ikitokea mpanda kuelekea Tabora ikiwa imezima katikati ya Station ya Urambo Na na Station ya Ussoke (Maeneo ya Checkline alimaarufu kama ckeleni) Siku ya Jmosi mida ya saa kumi jioni. Baada ya kutafuta chanzo cha tatizo la gari moshi hiyo, niliamabiwa kua mafuta yameisha na yameagiziwa toka Urambo, sikuweza kuamini niliyo yasikia kuwa kumbe Shilika hili kwa sasa wananunua mafuta ya mitaani kwa kutumia kidumu. Nilikaa kwa takribani dakika 13 katika eneo hilo, ndipo nilipo ona gari la moja la serikali likileta mafuta kwenye madumu. Ndugu zangu wana wa TZ sasa hali inatisha ndani ya TRA. Serikali inatupeleka wapi. Kwani TRA huwa ina visima vyake vya mafuta.
Mhemiwa Nundu Tueleze, najua thread hii utaiona.
Mhemiwa Nundu Tueleze, najua thread hii utaiona.