TRA sasa hii ni too much, ni ukiukwaji wa kanuni za kodi

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,128
18,733
Tanzania bwana, hasa katika hii awamu ya uongozi, tutasikia kila namna ya mambo ya ajabu.

Hili la hivi karibuni la TRA kuwaambia timu ya Yanga na timu nyingine kwamba pale watakapoamua kuwaingiza mashabiki wao bure kuangalia mechi za mpira, bado watakatwa kodi. Sasa unajiuliza, ikiwa kodi inatakiwa kukatwa kutokana na mapato, msingi wa kuwakata kodi timu y mpira wakiamua kuingiza mashabiki bure ili wapate nguvu ya kushangiliwa unakuwa nini hasa? Je hii si itakuwa kwamba timu hizo zinakatwa kodi toka mapato ya awali yaliyotozwa kodi tayari? Kuingiza watazamaji bure maana yake timu inajiingiza hasara, sasa utakataje kodi sehemu yenye "negative" revenue, hasara? TRA wamefikia mahali ambapo "charity act" inatakiwa kukatwa kodi?

Tunaelekea kuambiwa kwamba ukitoa msaada wa aina fulani lazima ukatwe kodi, ambapo ni kinyume na kanuni za kodi.

Labda hii mbiu ya Raisi Magufuli ya kusema shule itakuwa bure inabidi iachwe sasa, maana toka itangazwe tumeona ni jinsi gani hii elimu sio bure kwa kweli - ni kama TRA sasa wameshikwa na munkari wa kukamua kodi kwa kila namna, hata zile ambazo hazikubaliki katika misingi ya kodi. Tumesikia kodi za kodi za taasisi za dini, malipo ya kiinua mgongo, miamala ya benki, utalii, na sasa charity acts - hivi hizi mbio za kodi za kulazimsha zitaishia wapi? Kama suala ni kupata fedha za elimu ya bure basi afadhali turudi kule kule kwa jana ili tusitwikwe mizigo ya kodi ambazo hazieleweki sasa! It is too much!
 
Huwezi ukakosesha serikali mapato kwa sababu zisizo na msingi kama hizi. Kwani nani alisema wasipowalipia watazamaji hawataingia? Kama viongozi waliamua kuwalipia washabiki wao basi gharama za ziada ni kodi ya serikali ambayo ilitakiwa ilipwe.

Ni sawa sawa, na concept ya transfer pricing, yaani kuuziana vitu kwa bei ya chini kati ya kampuni moja na nyingine kwa kuwa zina uhusiano haimaanishi ndio kukosekana kwa mapato ya serikali. Kwa kuliangalia hili ndio kukaanzishwa transfer pricing regulations ili kuikazia the Income Tax Act, 2004. Kwa hili nadhani TRA walikuwa sahihi.

Moja ya tatizo linaloikabili nchi yetu kwa sasa ni kwamba 'hisia' zinatumika sana kwenye maamuzi kuliko 'mantiki'. Mtoa mada, kihisia up sahihi bali kimantiki hapana. Yanga walijitengenezea hasara wenyewe kwa kuwalipia washabiki, kodi lazima ilipwe.

NB: Sina ubia na TRA wala hii serikali wala CCM, ni mtanzania mlipa kodi na mpenda michezo
 
Tanzania bwana, hasa katika hii awamu ya uongozi, tutasikia kila namna ya mambo ya ajabu.

Hili la hivi karibuni la TRA kuwaambia timu ya Yanga na timu nyingine kwamba pale watakapoamua kuwaingiza mashabiki wao bure kuangalia mechi za mpira, bado watakatwa kodi. Sasa unajiuliza, ikiwa kodi inatakiwa kukatwa kutokana na mapato, msingi wa kuwakata kodi timu y mpira wakiamua kuingiza mashabiki bure ili wapate nguvu ya kushangiliwa unakuwa nini hasa? Je hii si itakuwa kwamba timu hizo zinakatwa kodi toka mapato ya awali yaliyotozwa kodi tayari? Kuingiza watazamaji bure maana yake timu inajiingiza hasara, sasa utakataje kodi sehemu yenye "negative" revenue, hasara? TRA wamefikia mahali ambapo "charity act" inatakiwa kukatwa kodi?

Tunaelekea kuambiwa kwamba ukitoa msaada wa aina fulani lazima ukatwe kodi, ambapo ni kinyume na kanuni za kodi.

Labda hii mbiu ya Raisi Magufuli ya kusema shule itakuwa bure inabidi iachwe sasa, maana toka itangazwe tumeona ni jinsi gani hii elimu sio bure kwa kweli - ni kama TRA sasa wameshikwa na munkari wa kukamua kodi kwa kila namna, hata zile ambazo hazikubaliki katika misingi ya kodi. Tumesikia kodi za kodi za taasisi za dini, malipo ya kiinua mgongo, miamala ya benki, utalii, na sasa charity acts - hivi hizi mbio za kodi za kulazimsha zitaishia wapi? Kama suala ni kupata fedha za elimu ya bure basi afadhali turudi kule kule kwa jana ili tusitwikwe mizigo ya kodi ambazo hazieleweki sasa! It is too much!

Maswala ya kodi Elimu kabisa inayosomewa Chuo Kikuu,
na TRA wana hao Wataalamu, kama hao Yanga wako watakuwa wameonewa kuna mahali pa kwenda!
 
Huwezi ukakosesha serikali mapato kwa sababu zisizo na msingi kama hizi. Kwani nani alisema wasipowalipia watazamaji hawataingia? Kama viongozi waliamua kuwalipia washabiki wao basi gharama za ziada ni kodi ya serikali ambayo ilitakiwa ilipwe. Ni sawa sawa, na concept ya transfer pricing, yaani kuuziana vitu kwa bei ya chini kati ya kampuni moja na nyingine kwa kuwa zina uhusiano haimaanishi ndio kukosekana kwa mapato ya serikali. Kwa kuliangalia hili ndio kukaanzishwa transfer pricing regulations ili kuikazia the Income Tax Act, 2004. Kwa hili nadhani TRA walikuwa sahihi. Moja ya tatizo linaloikabili nchi yetu kwa sasa ni kwamba 'hisia' zinatumika sana kwenye maamuzi kuliko 'mantiki'. Mtoa mada, kihisia up sahihi bali kimantiki hapana. Yanga walijitengenezea hasara wenyewe kwa kuwalipia washabiki, kodi lazima ilipwe.
NB: Sina ubia na TRA wala hii serikali wala CCM, ni mtanzania mlipa kodi na mpenda michezo

Mkuu, ningekubaliana na wewe ikiwa Yanga walifanya hivyo ili kujinufaisha (financial gan). Huwezi kulinganisha kuingiza watazamaji bure na kampuni mbili kuuziana kitu kwa bei ya chini isiyo halisi katika suala la transfer pricing. Kwa kuuziana kitu kwa bei ya chini lengo inakuwa ni kuongeza faida na kukwepa kodi - financial gain objectives. Sasa kuingiza mashabiki bure, kuna financial gain objectives gani kwa timu kiasi kwamba wawe penalized? Huwezi kusema lazima kuwe na penalty ya kuikosesha serikali mapato - kwa sabau ukisema hivyo, basi mie ile fedha yangu nyingi niliyoiweka benki kwenye current account ambayo haina interest, badala ya ku-invest, ninatakiwa niwe penalized kwa kuikosesha nchi mapato.

Yes, nchi yetu inapitia kipindi cha uongozi wa "kihisia", na hili litatia ndani maamuzi mengine ya TRA.
 
Maswala ya kodi Elimu kabisa inayosomewa Chuo Kikuu, na TRA wana hao Wataalamu, kama hao yanga wako watakuwa wameonewa kunamahali pa kwenda!

Ninavyokumbuka, huwezi kushitaki serikali kwa kukuonea kwenye kodi, hata kama leo ikitangazwa leo utakatwa kodi ya 70% ya mhahara wako. Unachotakiwa kufanya ni kubadili uongozi. Ndio maana wana siasa wanalitumia suala la kodi kwenye kampeni.
 
Ninavyokumbuka, huwezi kushitaki serikali kwa kukuonea kwenye kodi, hata kama leo ikitangazwa leo utakatwa kodi ya 70% ya mhahara wako. Unachotakiwa kufanya ni kubadili uongozi. Ndio maana wana siasa wanalitumia suala la kodi kwenye kampeni.


Sidhani kama hilo ni la kweli, kama ukikatwa kodi ambayo haukustahili kukatwa kisheria unaweza kuidai lkn sina uhakika kama nilivyosema mambo ya kodi ni fani inayojitegemea na ina mambo mengi sana hivyo kuanza kuhukumu hapa kwenye mambo tusioyafahamu siyo sawa!
 
Mkuu, ningekubaliana na wewe ikiwa Yanga walifanya hivyo ili kujinufaisha (financial gan). Huwezi kulinganisha kuingiza watazamaji bure na kampuni mbili kuuziana kitu kwa bei ya chini isiyo halisi katika suala la transfer pricing. Kwa kuuziana kitu kwa bei ya chini lengo inakuwa ni kuongeza faida na kukwepa kodi - financial gain objectives. Sasa kuingiza mashabiki bure, kuna financial gain objectives gani kwa timu kiasi kwamba wawe penalized? Huwezi kusema lazima kuwe na penalty ya kuikosesha serikali mapato - kwa sabau ukisema hivyo, basi mie ile fedha yangu nyingi niliyoiweka benki kwenye current account ambayo haina interest, badala ya ku-invest, ninatakiwa niwe penalized kwa kuikosesha nchi mapato.

Yes, nchi yetu inapitia kipindi cha uongozi wa "kihisia", na hili litatia ndani maamuzi mengine ya TRA.
Hapo kulinganisha na transfer pricing mkuu sio mfano wa moja kwa moja. Point yangu ni kwamba ni mfano wa measures zinazoweza kutumika na serikali kuhakikisha kwamba mapato yanakusanywa hata kama mhamala husika unaonekana hauna faida ya moja kwa moja. Specifically kwa suala la yanga ni kwamba hakukuwa na ulazima wa kulipia viiingilio. Hiyo ni hasara waliyojitakia wenyewe. Zipo kodi zinazotozwa kwenye faida (profit) na zipo zinazotozwa kwenye mapato (revenue). Na ndio maana kama kampuni ikiendelea kupata hasara kwa Zaidi ya miaka mitatu mfululizo inaanza kutozwa kodi kwenye mapato badala ya faida.
 
Sidhani kama hilo ni la kweli, kama ukikatwa kodi ambayo haukustahili kukatwa kisheria unaweza kuidai lkn sina uhakika kama nilivyosema mambo ya kodi ni fani inayojitegemea na ina mambo mengi sana hivyo kuanza kuhukumu hapa kwenye mambo tusioyafahamu siyo sawa!

Wewe hufahamu lakini wengi wanaochangia hapa wanafahamu wanachokiongea
 
Mkuu mwenyew nilishtuka sana nilipoona Jamal Malinzi kwenye press conference yake akiitaka Yanga walipe kodi, nishangazwa na kauli yake, ina maana hajui kodi inatozwa Vp,? unatozaje kodi kitu ambacho hakipo, wakasome sheria za kodi vizuri, huwez kulipa kodi kama ukipata hasara na Yanga wapo sawa kabisa Sababu hapakua na mapato kwenye ule mchezo, sasa hiyo kodi wataikata kwenye kitu gani? Ifike mahali tuache siasa kwenye mambo yanayoongozwa kwa kanuni
 
Huwezi ukakosesha serikali mapato kwa sababu zisizo na msingi kama hizi. Kwani nani alisema wasipowalipia watazamaji hawataingia? Kama viongozi waliamua kuwalipia washabiki wao basi gharama za ziada ni kodi ya serikali ambayo ilitakiwa ilipwe. Ni sawa sawa, na concept ya transfer pricing, yaani kuuziana vitu kwa bei ya chini kati ya kampuni moja na nyingine kwa kuwa zina uhusiano haimaanishi ndio kukosekana kwa mapato ya serikali. Kwa kuliangalia hili ndio kukaanzishwa transfer pricing regulations ili kuikazia the Income Tax Act, 2004. Kwa hili nadhani TRA walikuwa sahihi. Moja ya tatizo linaloikabili nchi yetu kwa sasa ni kwamba 'hisia' zinatumika sana kwenye maamuzi kuliko 'mantiki'. Mtoa mada, kihisia up sahihi bali kimantiki hapana. Yanga walijitengenezea hasara wenyewe kwa kuwalipia washabiki, kodi lazima ilipwe.
NB: Sina ubia na TRA wala hii serikali wala CCM, ni mtanzania mlipa kodi na mpenda michezo

Well said!
 
Mkuu mwenyew nilishtuka sana nilipoona Jamal Malinzi kwenye press conference yake akiitaka Yanga walipe kodi, nishangazwa na kauli yake, ina maana hajui kodi inatozwa Vp,? unatozaje kodi kitu ambacho hakipo, wakasome sheria za kodi vizuri, huwez kulipa kodi kama ukipata hasara na Yanga wapo sawa kabisa Sababu hapakua na mapato kwenye ule mchezo, sasa hiyo kodi wataikata kwenye kitu gani? Ifike mahali tuache siasa kwenye mambo yanayoongozwa kwa kanuni

Tuwe makini. Sheria ya kodi inabidi isomwe vizuri si kwa juu juu. Tusipokuwa makini tuta tengenezewa hasara ambazo zitatumika kukwepa kodi. Mambo haya yameishatokea kwa wenzetu nchi za nje na wamejifunza kuyathibiti. Kwa mfano uingereza, zawadi au urithi zina sheria zake za kodi. Kwani waligundua kuwa mapato yalikuwa yanatolewa kama zawadi kwa watu wenye uhusiano na kisha aliyetoa zawadi akiendelea kutumia zawadi hizo kama pesa yake na hivyo kukwepa kodi.
 
Back
Top Bottom