TRA sasa hii ni too much, ni ukiukwaji wa kanuni za kodi

Mkuu, ningekubaliana na wewe ikiwa Yanga walifanya hivyo ili kujinufaisha (financial gan). Huwezi kulinganisha kuingiza watazamaji bure na kampuni mbili kuuziana kitu kwa bei ya chini isiyo halisi katika suala la transfer pricing. Kwa kuuziana kitu kwa bei ya chini lengo inakuwa ni kuongeza faida na kukwepa kodi - financial gain objectives. Sasa kuingiza mashabiki bure, kuna financial gain objectives gani kwa timu kiasi kwamba wawe penalized? Huwezi kusema lazima kuwe na penalty ya kuikosesha serikali mapato - kwa sabau ukisema hivyo, basi mie ile fedha yangu nyingi niliyoiweka benki kwenye current account ambayo haina interest, badala ya ku-invest, ninatakiwa niwe penalized kwa kuikosesha nchi mapato.

Yes, nchi yetu inapitia kipindi cha uongozi wa "kihisia", na hili litatia ndani maamuzi mengine ya TRA.
hivi tunaposikia watazamaji wameingia bure huwa tunaelewaje?..

Je Yanga wana rasilimali uwanja wao ambao wana nguvu ya kufanya hivyo au wanaulupia uwanja mwingine kwa idadi ya ujazo wa uwanja?

Na kama wanalipia watazamaji..hapo tayari kuna biashara imefanyika na kodi lazima ilipwe
 
Tuwe makini. Sheria ya kodi inabidi isomwe vizuri si kwa juu juu. Tusipokuwa makini tuta tengenezewa hasara ambazo zitatumika kukwepa kodi. Mambo haya yameishatokea kwa wenzetu nchi za nje na wamejifunza kuyathibiti. Kwa mfano uingereza, zawadi au urithi zina sheria zake za kodi. Kwani waligundua kuwa mapato yalikuwa yanatolewa kama zawadi kwa watu wenye uhusiano na kisha aliyetoa zawadi akiendelea kutumia zawadi hizo kama pesa yake na hivyo kukwepa kodi.
Mkuu sheria zetu za kodi ni kama tumecopy Uingereza na India, mambo mengi sana yanaendana, hata hiyo unayozungumzia ya kutoa mapato kama zawadi, ama mahari kwenye sheria zetu ipo, na kama hivyo vitu vikiingizwa kama expenses ilikua kupunguza kodi hua zinajumlishwa, maana yake vnakatwa kodi, kwahiyo sio kwamba hivyo vitu havipo, ni kwa kuwa labda tu hujawahi kutana na hicho kitu, Ila suala la kutolipa kodi kama ukipata hasara ni jambo la kawaida sana Ila kama utapata hasara kwa miaka kadhaa TRA wanaruhusiwa kufungia kampuni yako
 
Hapo kulinganisha na transfer pricing mkuu sio mfano wa moja kwa moja. Point yangu ni kwamba ni mfano wa measures zinazoweza kutumika na serikali kuhakikisha kwamba mapato yanakusanywa hata kama mhamala husika unaonekana hauna faida ya moja kwa moja. Specifically kwa suala la yanga ni kwamba hakukuwa na ulazima wa kulipia viiingilio. Hiyo ni hasara waliyojitakia wenyewe. Zipo kodi zinazotozwa kwenye faida (profit) na zipo zinazotozwa kwenye mapato (revenue). Na ndio maana kama kampuni ikiendelea kupata hasara kwa Zaidi ya miaka mitatu mfululizo inaanza kutozwa kodi kwenye mapato badala ya faida.
Unatumia vigezo gani kupima ulazima wa Yanga kuwalipia viingilio mashabiki wake?

Kodi inakatwa kwenye mapato, kama hakuna mapato hakuna kodi. Hizi zingine unazoambatanisha hapa ni ngonjera tu. Kuna wawekezaji wangapi wamehodhi mashamba hawayalimi? TRA wameshaenda kukata kodi ya mazao ambayo yangelimwa? Tupunguze mihemko na kutaka kujifanya wawajibikaji, tuendako tutatoza kodi sadaka
 
hivi tunaposikia watazamaji wameingia bure huwa tunaelewaje?..

Je Yanga wana rasilimali uwanja wao ambao wana nguvu ya kufanya hivyo au wanaulupia uwanja mwingine kwa idadi ya ujazo wa uwanja?

Na kama wanalipia watazamaji..hapo tayari kuna biashara imefanyika na kodi lazima ilipwe
Unajua viingilio vya mechi huwa anachukua nani? Maana namna yako ya kuitafsiri Yanga kulipa viingilio inaonesha unadhani labda Yanga wamepeleka hela sehemu ili hao mashabiki waruhusiwe kuingia.

Yanga ndio wanufaika wa viingilio kama vingelipwa, walichofanya ni kuamua kutokulipwa. Sasa unatoza kodi kwa pato lipi ambalo kapata nani?
 
Unatumia vigezo gani kupima ulazima wa Yanga kuwalipia viingilio mashabiki wake?

Kodi inakatwa kwenye mapato, kama hakuna mapato hakuna kodi. Hizi zingine unazoambatanisha hapa ni ngonjera tu. Kuna wawekezaji wangapi wamehodhi mashamba hawayalimi? TRA wameshaenda kukata kodi ya mazao ambayo yangelimwa? Tupunguze mihemko na kutaka kujifanya wawajibikaji, tuendako tutatoza kodi sadaka
Itakuaje kila timu ikiwa inafanya hivyo? Ninachosisitiza hapa ni kwamba kama maamuzi yale yangeifanya serikali kukosa kodi basi kodi hiyo ilipaswa ilipwe na wahusika na walitakiwa kuiweka kwenye gharama zao za kuwalipia washabiki. Mhemko ni pale unapoweka hisia kwamba kodi haikutozwa kihalali kwa sababu za kuwalipia washabiki viingilio. Hata hao waliotozwa kodi wana njia mbalimbali za kupingana na kodi hizo kisheria, kuna baraza/bodi ya usuluhishi wa kodi na pia kuna mahakama, n.k. Kama wanahisi wameonewa wakatumie vifungu vya sharia kupinga mambo hayo. Mihemko ni kutoangalia sheria za kodi husika zinasemaje kabla ya kulalamika. Ungeweka vifungu vya sheria vilivyokiukwa na TRA katika ukusanyaji huo.
 
Tanzania bwana, hasa katika hii awamu ya uongozi, tutasikia kila namna ya mambo ya ajabu.

Hili la hivi karibuni la TRA kuwaambia timu ya Yanga na timu nyingine kwamba pale watakapoamua kuwaingiza mashabiki wao bure kuangalia mechi za mpira, bado watakatwa kodi. Sasa unajiuliza, ikiwa kodi inatakiwa kukatwa kutokana na mapato, msingi wa kuwakata kodi timu y mpira wakiamua kuingiza mashabiki bure ili wapate nguvu ya kushangiliwa unakuwa nini hasa? Je hii si itakuwa kwamba timu hizo zinakatwa kodi toka mapato ya awali yaliyotozwa kodi tayari? Kuingiza watazamaji bure maana yake timu inajiingiza hasara, sasa utakataje kodi sehemu yenye "negative" revenue, hasara? TRA wamefikia mahali ambapo "charity act" inatakiwa kukatwa kodi?

Tunaelekea kuambiwa kwamba ukitoa msaada wa aina fulani lazima ukatwe kodi, ambapo ni kinyume na kanuni za kodi.

Labda hii mbiu ya Raisi Magufuli ya kusema shule itakuwa bure inabidi iachwe sasa, maana toka itangazwe tumeona ni jinsi gani hii elimu sio bure kwa kweli - ni kama TRA sasa wameshikwa na munkari wa kukamua kodi kwa kila namna, hata zile ambazo hazikubaliki katika misingi ya kodi. Tumesikia kodi za kodi za taasisi za dini, malipo ya kiinua mgongo, miamala ya benki, utalii, na sasa charity acts - hivi hizi mbio za kodi za kulazimsha zitaishia wapi? Kama suala ni kupata fedha za elimu ya bure basi afadhali turudi kule kule kwa jana ili tusitwikwe mizigo ya kodi ambazo hazieleweki sasa! It is too much!

Ni ukweli ulio wazi kabisa, haiwezekani kukawa na watu kuingia bure bila gharama yoyote kuwepo. Ikumbukwe kwamba Yanga huo sio uwanja wao hivyo ni lazima walipie gharama kwa mmiliki wa uwanja. Hizo gharama ni kama kununua bidhaa, LAZIMA KODI IKATWE KWA MLAJI yaani YANGA.
 
Mkuu mbona hata mwaka haujafika, hadi miaka mitano ikipita nadhani tutakuwa tumeshashika adabu yetu.
Naisubiria kodi ya matuta yangu ya mchicha na Chinese cabbage .
Amesema Leo muuza mchicha asibuguziwe na tozo zisizo na miguu
 
Tanzania bwana, hasa katika hii awamu ya uongozi, tutasikia kila namna ya mambo ya ajabu.

Hili la hivi karibuni la TRA kuwaambia timu ya Yanga na timu nyingine kwamba pale watakapoamua kuwaingiza mashabiki wao bure kuangalia mechi za mpira, bado watakatwa kodi. Sasa unajiuliza, ikiwa kodi inatakiwa kukatwa kutokana na mapato, msingi wa kuwakata kodi timu y mpira wakiamua kuingiza mashabiki bure ili wapate nguvu ya kushangiliwa unakuwa nini hasa? Je hii si itakuwa kwamba timu hizo zinakatwa kodi toka mapato ya awali yaliyotozwa kodi tayari? Kuingiza watazamaji bure maana yake timu inajiingiza hasara, sasa utakataje kodi sehemu yenye "negative" revenue, hasara? TRA wamefikia mahali ambapo "charity act" inatakiwa kukatwa kodi?

Tunaelekea kuambiwa kwamba ukitoa msaada wa aina fulani lazima ukatwe kodi, ambapo ni kinyume na kanuni za kodi.

Labda hii mbiu ya Raisi Magufuli ya kusema shule itakuwa bure inabidi iachwe sasa, maana toka itangazwe tumeona ni jinsi gani hii elimu sio bure kwa kweli - ni kama TRA sasa wameshikwa na munkari wa kukamua kodi kwa kila namna, hata zile ambazo hazikubaliki katika misingi ya kodi. Tumesikia kodi za kodi za taasisi za dini, malipo ya kiinua mgongo, miamala ya benki, utalii, na sasa charity acts - hivi hizi mbio za kodi za kulazimsha zitaishia wapi? Kama suala ni kupata fedha za elimu ya bure basi afadhali turudi kule kule kwa jana ili tusitwikwe mizigo ya kodi ambazo hazieleweki sasa! It is too much!
Upo vizuri sana mkuu, nami nashangaa hivi ni kigezo gani watatumia kukata kodi kwenye mapato 0,na ijulikane kuwa kama timu imejitolea kuingiza watazamaji bure ni kutafuta uungwaji mkono yaani kushangiliwa na wapenzi ili kupata matokeo mazuri hasa kwenye mashindano ya kimataifa, hili ni kwa manufaa ya taifa,au utawala wetu hauhitaji michango ya michezo?
 
Mkuu mbona hata mwaka haujafika, hadi miaka mitano ikipita nadhani tutakuwa tumeshashika adabu yetu.
Naisubiria kodi ya matuta yangu ya mchicha na Chinese cabbage .
Hiyo haipo mbali utamuona mwenyekiti wa serikali ya mtaa ana kutembelea na efd
 

Maswala ya kodi Elimu kabisa inayosomewa Chuo Kikuu,
na TRA wana hao Wataalamu, kama hao Yanga wako watakuwa wameonewa kuna mahali pa kwenda!
Wewe tangu umetupwa kwenye uteuzi wa juzi naona umeamua kuwa mwanaharakati wakutetea kila udhaifu
 
Sidhani kama hilo ni la kweli, kama ukikatwa kodi ambayo haukustahili kukatwa kisheria unaweza kuidai lkn sina uhakika kama nilivyosema mambo ya kodi ni fani inayojitegemea na ina mambo mengi sana hivyo kuanza kuhukumu hapa kwenye mambo tusioyafahamu siyo sawa!
Sasa kitu hujui alafu unajidai kuchangia?wewe kweli inabidi upate mshauri nasaha
 
Amesema Leo muuza mchicha asibuguziwe na tozo zisizo na miguu
Hawana maana kama mkia wa mbuzi hawa, utasikia "tumegundua anaingiza elfu 50000 kwa siku,anatakiwa alipe kodi ya urea na NPK" ,acha tu maana hakuna namna.
 
Itakuaje kila timu ikiwa inafanya hivyo?
Kwani alikwambia nani kuwa PRIMARY OBJECTIVE YA MPIRA KUCHEZWA NI SERIKALI KUPATA KODI?

Ninachosisitiza hapa ni kwamba kama maamuzi yale yangeifanya serikali kukosa kodi basi kodi hiyo ilipaswa ilipwe na wahusika na walitakiwa kuiweka kwenye gharama zao za kuwalipia washabiki
Yanga haijaingia gharama yeyote kuwalipia mashabiki. Ni sawa na mimi nikukatie muwa shambani kwangu bila kukuuzia, au ndio kwamba sasa sheria zenu mpya ni kwamba haturuhusiwi kukirimiana kitu? Wakati mnaandaa futari kwa halaiki, hamjui kuwa kwa kitendo kile mnaua transactions za manunuzi ya futari somewhere else?

Mhemko ni pale unapoweka hisia kwamba kodi haikutozwa kihalali kwa sababu za kuwalipia washabiki viingilio. Hata hao waliotozwa kodi wana njia mbalimbali za kupingana na kodi hizo kisheria, kuna baraza/bodi ya usuluhishi wa kodi na pia kuna mahakama, n.k. Kama wanahisi wameonewa wakatumie vifungu vya sharia kupinga mambo hayo. Mihemko ni kutoangalia sheria za kodi husika zinasemaje kabla ya kulalamika. Ungeweka vifungu vya sheria vilivyokiukwa na TRA katika ukusanyaji huo.
Punguza jazba, huu mchezo hauhitaji hasira. Hapa si tunaongea kwa hoja, povu la nini...kwani nimekwambia mimi ni wakili wao? Nakupa tu facts. Primary objectives za mpira kuchezwa sio KODI, kodi inachajiwa tu kwenye mapato yatokanayo. Kitu cha lazima ni tozo za uwanja, ambazo zimelipwa...sasa povu la nini?

Ina maana Yanga wakigomea kucheza mechi, TRA wataidai Yanga kodi ambayo ingelipwa kwenye mechi hiyo?
 
Tukirudi kulekule huenda hata madawati yakapatikana bila kuomba kwa wasamalia wema
Tanzania bwana, hasa katika hii awamu ya uongozi, tutasikia kila namna ya mambo ya ajabu.

Hili la hivi karibuni la TRA kuwaambia timu ya Yanga na timu nyingine kwamba pale watakapoamua kuwaingiza mashabiki wao bure kuangalia mechi za mpira, bado watakatwa kodi. Sasa unajiuliza, ikiwa kodi inatakiwa kukatwa kutokana na mapato, msingi wa kuwakata kodi timu y mpira wakiamua kuingiza mashabiki bure ili wapate nguvu ya kushangiliwa unakuwa nini hasa? Je hii si itakuwa kwamba timu hizo zinakatwa kodi toka mapato ya awali yaliyotozwa kodi tayari? Kuingiza watazamaji bure maana yake timu inajiingiza hasara, sasa utakataje kodi sehemu yenye "negative" revenue, hasara? TRA wamefikia mahali ambapo "charity act" inatakiwa kukatwa kodi?

Tunaelekea kuambiwa kwamba ukitoa msaada wa aina fulani lazima ukatwe kodi, ambapo ni kinyume na kanuni za kodi.

Labda hii mbiu ya Raisi Magufuli ya kusema shule itakuwa bure inabidi iachwe sasa, maana toka itangazwe tumeona ni jinsi gani hii elimu sio bure kwa kweli - ni kama TRA sasa wameshikwa na munkari wa kukamua kodi kwa kila namna, hata zile ambazo hazikubaliki katika misingi ya kodi. Tumesikia kodi za kodi za taasisi za dini, malipo ya kiinua mgongo, miamala ya benki, utalii, na sasa charity acts - hivi hizi mbio za kodi za kulazimsha zitaishia wapi? Kama suala ni kupata fedha za elimu ya bure basi afadhali turudi kule kule kwa jana ili tusitwikwe mizigo ya kodi ambazo hazieleweki sasa! It is too much!
 
Mkuu, ningekubaliana na wewe ikiwa Yanga walifanya hivyo ili kujinufaisha (financial gan). Huwezi kulinganisha kuingiza watazamaji bure na kampuni mbili kuuziana kitu kwa bei ya chini isiyo halisi katika suala la transfer pricing. Kwa kuuziana kitu kwa bei ya chini lengo inakuwa ni kuongeza faida na kukwepa kodi - financial gain objectives. Sasa kuingiza mashabiki bure, kuna financial gain objectives gani kwa timu kiasi kwamba wawe penalized? Huwezi kusema lazima kuwe na penalty ya kuikosesha serikali mapato - kwa sabau ukisema hivyo, basi mie ile fedha yangu nyingi niliyoiweka benki kwenye current account ambayo haina interest, badala ya ku-invest, ninatakiwa niwe penalized kwa kuikosesha nchi mapato.

Yes, nchi yetu inapitia kipindi cha uongozi wa "kihisia", na hili litatia ndani maamuzi mengine ya TRA.
Sasa wao waliowaingiza watu bure wameikosesha serikali kwakukaba nafasi za watu ambao wangezilipa, acheni kulalamika lalamika
 
Mkuu, ningekubaliana na wewe ikiwa Yanga walifanya hivyo ili kujinufaisha (financial gan). Huwezi kulinganisha kuingiza watazamaji bure na kampuni mbili kuuziana kitu kwa bei ya chini isiyo halisi katika suala la transfer pricing. Kwa kuuziana kitu kwa bei ya chini lengo inakuwa ni kuongeza faida na kukwepa kodi - financial gain objectives. Sasa kuingiza mashabiki bure, kuna financial gain objectives gani kwa timu kiasi kwamba wawe penalized? Huwezi kusema lazima kuwe na penalty ya kuikosesha serikali mapato - kwa sabau ukisema hivyo, basi mie ile fedha yangu nyingi niliyoiweka benki kwenye current account ambayo haina interest, badala ya ku-invest, ninatakiwa niwe penalized kwa kuikosesha nchi mapato.

Yes, nchi yetu inapitia kipindi cha uongozi wa "kihisia", na hili litatia ndani maamuzi mengine ya TRA.
Kwahiyo kama wewe(Mashabiki for this matter) hawakujinufaisha ndio waitie hasara serikali kurekebisha miundo mbinu waliyoiharibu?
 
Hapo kulinganisha na transfer pricing mkuu sio mfano wa moja kwa moja. Point yangu ni kwamba ni mfano wa measures zinazoweza kutumika na serikali kuhakikisha kwamba mapato yanakusanywa hata kama mhamala husika unaonekana hauna faida ya moja kwa moja. Specifically kwa suala la yanga ni kwamba hakukuwa na ulazima wa kulipia viiingilio. Hiyo ni hasara waliyojitakia wenyewe. Zipo kodi zinazotozwa kwenye faida (profit) na zipo zinazotozwa kwenye mapato (revenue). Na ndio maana kama kampuni ikiendelea kupata hasara kwa Zaidi ya miaka mitatu mfululizo inaanza kutozwa kodi kwenye mapato badala ya faida.
Kama Yanga wataamua kujitoa katika mashindano pia watatozwa kodi?
 
Back
Top Bottom