TRA kwanini mnawanyanyasa wafanyabiashara kiasi hicho?

TRA wakiwasimbua sana wafanyabiashara jaribuni ku "organize" mgomo nchi nzima, fungeni maduka na biashara kwa siku kadhaa serikali itatia akili tu, duniani mabadiliko na hali bora haviombwi bali vinadaiwa na kuchukuliwa, ni muda wa kudai hari bora kwa wafanya biashara.
 
Ndugu yangu kuwa na roho ya nyama,hawa walipa kodi kidogo waliopo nchini wanahitaji utu,ni binaadamu ndugu yangu?lazima pawepo na urafiki kati ya mlipa kodi,na mtoza kodi,lkn usisahau mm nawazungumzia wafanyabiashara wa ngazi ya chini wenye maduka mtaani ndio wanakutana na hizo faini ndugu yangu
I'm sorry.
 
Tanzania ni Nchi ngumu kufanya biashara kwa Nchi za kusini maana wana usumbufu sana...Nchi zote ukilipa kodi basi ni kuuza tuu Bongo kodi watu wanalipa tena unaona sijui majembe wanafata risiti Mara police huo ni umasikini wa akili sana...fanyeni kama Zambia au SA kuhakikisha mizigo inayoingia yote ilipiwe kodi tena ya kawaida sio kandaminizi kama hizo kodi ya 40ft contena la suit ni 70milioni hapo mnata watu wakwepe kodi tuu utadhani tumerogwa nguvu nyingi akili kidogo..
 
Kaka upo sahihi sana tunafanya biashara kwa hofu utafikil tunauza ngoz za watu!!!
 
@lendile unamaanisha nini ukisema faini ya 3? Kwa kosa gani?
Hata kama una mashine ya efd,imeharibika na taarifa umetoa kwa maandishi tra ukikutwa hutumii mashine ya efd unapigwa faini milion 3 taka usitake,wanatumia kauli ya hapa kazi tu
 
Halafu eti kwemye mikutano huko tunasikia sikia kwamba wanaambiwa eti huu ndo muda muafaka mzuri wa wafanyabiashara na wanapendwa ETI
 
Leo wakiongozana na viongozi wa kisiasa hapa Iringa wamevamia duka la mfanyabiashara mmoja wakiwa na askari kadhaa wenye bunduki. Sasa unajiuliza haya mabunduki ni ya nini kwenye kukusanya kodi?
Ili wapandishwe VYEO ..wewe hujui staili ya kupandishwa cheo
 
Kwanini katika kupiga faini wasiwe wanaangaki na mtaji wa mtu?
 
TRA irudishe mfumo wa sales tax kwa kila mfanyabiashara apangiwe kwa mwezi atoa kiasi gani kama kodi ya mauzo.
EFDA Machine ni usumbufu na imeongeza masuala rushwa kwa watumishi wa TRA Kodi za Ndani
Fanya hesabu kama kila mfanyabiashara mdogo atatoa sh 20000 kwa mwezi kama kodi ya mauzo Fixed serikali itapata shilingi ngapi
Serikali ipange maduka kwa madaraja iwepo Class A Class B Class C Class D na hizo kodi za sales tax zitolewee kufuatana na mtaji/aina ya biashara na iwepo kitengo cha Investigation kuchunguza ulipaji wa kodi unakuwa sahihi. Hapo bado serikali itawekea kiwango cha kutoza gari za biashara pia kila mwezi.
EFDA Machine ni hasara kwa serikali na wafanyabiashara.
Mashine zenyewe mbovumbovu sana yaani ni usumbufu tu.
 
Leo wakiongozana na viongozi wa kisiasa hapa Iringa wamevamia duka la mfanyabiashara mmoja wakiwa na askari kadhaa wenye bunduki. Sasa unajiuliza haya mabunduki ni ya nini kwenye kukusanya kodi?
Kiongozi gani huyo wa kisiasa anaeenda kukusanya kodi?/tueleze uzuri...mtaje
 
Tatizo jamaa anafikiri wafanyabiashara wote wanatokea kaskazini kileee alikonyimqa kura.
 
Back
Top Bottom