BRAVO 2 ZERO
JF-Expert Member
- Jul 16, 2013
- 1,175
- 1,189
Mbona wanaokamatwa na madawa ya kulevya airpot ndege walizopanda hasizishikiliwi...Unatakiwa wewe unaebeba mzigo ujiridhishe kwamba mzigo umelipiwa kodi zote stahiki.
Kubeba mzigo ambao hauna risiti zote na wewe unakua umekubali hatari ama risk inayotokana na kuubeba huo mzigo.
Ni sawa useme ubebe mtu na bangi ama cocaine halafu ukamatwe useme wakuachie gari yako waende na mwenye mzigo. Pale wote nyie ni wauza madawa ya kulevya. Maana yake unakua umesaidia mtu kutenda kosa, aiding and abetting.
Ili kuepuka kosa la aiding and abetting, hakikisha mzigo unaouchukua uko clear, sio magendo ama madawa ya kulevya maana TRA wakikukamata wanasema unasafirisha magendo ama mzigo usiolipiwa kodi inakua wewe huna cha kujitetea.
Hili liko wazi mkuu sio lazima usome PGO.