Chukwu emeka
JF-Expert Member
- Jan 12, 2018
- 23,410
- 36,559
Habari wanaJF,
Niende moja kwa moja kwenye hoja yangu, kumekuwa na usumbufu mkubwa wanaoupata madereva wa magari madogo katika eneo la Kariakoo, wanapokodiwa na Wafanyabiashara wanaonunua mizigo, pindi mzigo unapokamatwa kwa madai mbalimbali ikiwemo kukosa risiti inayojitosheleza,maofisa hao wa TRA wanalishikilia na gari iliyokamatwa na mzigo katika eneo lao bila kujali kuwa lile gari limekodiwa tu na halina tatizo.
Kuna baadhi ya magari yanakaa pale zaidi ya mwezi mzima huku wakiwa na majibu yasiyo na staa kwa watu wanaoenda kudai magari yao ili kuendelea na biashara.Madereva wanaonja joto la jiwe pale kwa majibu ya kejeli wakati wao (madereva) magari yao hayana tatizo lolote.
Dereva anakua hana kosa kwani yeye amepaki kwenye kituo chake cha kazi yeye hausiki na ukusanyaji wa mizigo .
Cha ajabu TRA wanakamata gari pamoja na mzigo na mara nyingi mwenye mzigo anakuwepo kwenye gari. Mzigo unapofikishwa TRA kwa madai kuwa risiti hazijitoshelezi maafisa wanagoma kuliruhusu gari licha ya kuwa mwenye mzigo wapo naye.
Japokuwa mzigo unakuwa si wa wizi na mmiliki wa mzigo yupo,bado imekuwa kero kubwa hata kwa wamiliki wakifuatilia magari yao wanapata majibu amabayo hayaridhishi wakati shida siyo gari ni mzigo ulio ndani na gari limekodiwa tu.
Madereva wanashindwa kupata hesabu za maboss wao na wenye magari wanapata hasara isiyo na sababu.
Waziri na wahusika ingilieni kati hili suala, magari yamejazana pale ofisini kwao wakati hayana hatia yoyote na mwenye mzigo anakuwepo.
Hii ni kero kubwa sana watumishi TRA Kariakoo wamulikwe inawezekana ni namna ya kutengeneza mazingira ya rushwa.
Mdogo wangu Mwigulu Nchemba tupia jicho kwa vijana wako
Niende moja kwa moja kwenye hoja yangu, kumekuwa na usumbufu mkubwa wanaoupata madereva wa magari madogo katika eneo la Kariakoo, wanapokodiwa na Wafanyabiashara wanaonunua mizigo, pindi mzigo unapokamatwa kwa madai mbalimbali ikiwemo kukosa risiti inayojitosheleza,maofisa hao wa TRA wanalishikilia na gari iliyokamatwa na mzigo katika eneo lao bila kujali kuwa lile gari limekodiwa tu na halina tatizo.
Kuna baadhi ya magari yanakaa pale zaidi ya mwezi mzima huku wakiwa na majibu yasiyo na staa kwa watu wanaoenda kudai magari yao ili kuendelea na biashara.Madereva wanaonja joto la jiwe pale kwa majibu ya kejeli wakati wao (madereva) magari yao hayana tatizo lolote.
Dereva anakua hana kosa kwani yeye amepaki kwenye kituo chake cha kazi yeye hausiki na ukusanyaji wa mizigo .
Cha ajabu TRA wanakamata gari pamoja na mzigo na mara nyingi mwenye mzigo anakuwepo kwenye gari. Mzigo unapofikishwa TRA kwa madai kuwa risiti hazijitoshelezi maafisa wanagoma kuliruhusu gari licha ya kuwa mwenye mzigo wapo naye.
Japokuwa mzigo unakuwa si wa wizi na mmiliki wa mzigo yupo,bado imekuwa kero kubwa hata kwa wamiliki wakifuatilia magari yao wanapata majibu amabayo hayaridhishi wakati shida siyo gari ni mzigo ulio ndani na gari limekodiwa tu.
Madereva wanashindwa kupata hesabu za maboss wao na wenye magari wanapata hasara isiyo na sababu.
Waziri na wahusika ingilieni kati hili suala, magari yamejazana pale ofisini kwao wakati hayana hatia yoyote na mwenye mzigo anakuwepo.
Hii ni kero kubwa sana watumishi TRA Kariakoo wamulikwe inawezekana ni namna ya kutengeneza mazingira ya rushwa.
Mdogo wangu Mwigulu Nchemba tupia jicho kwa vijana wako