FredKavishe
JF-Expert Member
- Dec 4, 2010
- 1,090
- 318
Kama tunavyojua kodi nchi mwetu inakusanywa na TRA(Tanzania revenue authority) naona kama wamelala kimawazo au wanashindwa ubinifu wa kuongeza mapato yao ya kila siku kila mwezi kulifanya taifa lisiwe tegemezi kwa mataifa ya nje,world bank,IMF na mashirika mengine ya kimataifa.
Tanzania ni nchi yenye watu wanaokadiriwa milioni 50 bado tunasubiri report kamili ya sensa mwaka huu itatupa majibu tupo wangapi lakini cha kusangaza tunakusanya kidogo sana kuliko idadi ya wananchi na mali zetu nchini.
Kodi zetu kwa haraka zinatoka na mishahara ya waajiriwa,viwanda,makampuni,migodi(hapa tunadanganywa sana) na bidhaa kama chakula viwanji vya viminika.
Hivi nataka niwaulize TRA wanajua tanzania tuna watu wangapi wanapangisha nyumba zao na je wanawakata kodi hao watu.tuchukulie mfano ni wangapi wa nyumba osterbay,masaki,mbezi beach,njiro na maeneo mengine ambayo nyumba ni bei ghali.unakuta nyumba masaki ni dola 3000 kwa mwezi mtu anaingia pale analipia kwa mwaka mzima zaidi ya dola 36000 hivi sasa mtu ana nyumba hata 3 ambazo bei zake ni hizo je serikali imechukua kodi asilimia ngapi hapo.
Turudi huku mtaani sasa chumba 50000 unakuta mwenye nyumba ana vyumba hata 8 ina maana kwa mwezi ana 400000 je serikali inapata kodi kweli hapa maana naona nyumba nyingi unamlipa mwenye nyumba yenye anaenda lilipia kodi ya ardhi na nyumba ambayo ni 10000 tu.
Ni wakati sasa tuzijue nyumba zote za biashara serikali ukusanye kodi kwa kutokana na kile mwenye nyumba anachoingiza kwa mwezi na kwa mwaka ni wakati wa TRA kuanza kupita kwenye nyumba za watu na kuzisajili na kutoa vitabu mpangaji yoyote atakayelipa kodi awe anapewa risiti hii itaongeza kujua mwenye nyumba anaingiza kiasi gani.
Sijui kama kuna mfumo wa kuwabana wenye nyumba ambao wanaingiza pesa nyingi sana na hazilipiwi kodi kabisa ni uhakika kabisa hapa serikali inapoteza matapo na kungangania kuwabana wananchi kwenye vyakula na vinywaji.
Kingine kuna wakina mama wana migahawa barabarani sehemu za vitu kwa kuwa wanauza chakula hawakwati kodi jiulize kuna vijana wana vibanda vya chipsi kwa siku wanaingiza faida ya 20000-50000 je serikali inapataje kodi zao.
Ni wakati wa TRA kuandaa mfumo kwa wafanya biashara wote wenye vibanda barabarani kukatia TIN no na kufungiliwa account kwenye mabenk yaweke huduma nafuu ili hizi pesa zinazoenda kuwekwa nyumbani ziwekwe kwenye mabenk.
Mimi nadhani kama hawa kina mama,vijana wote watakatia TIN no hata TRA wakipata 2000 kwa mwezi kwa biashara na hizi hela wanazokusanywa wakaelezwa umuhimu wake wawe wanaziwekwa benk nchi yetu itapiga hatua kubwa sana tuseme mimi kijana nauza chips ninapata faida ya 30000 kwa siku labda kwa wiki naenda kuhifadhi bank 100000 kwa mwezi nina laki 4.sijaimalisha maisha yangu kuliko kukaa na ile hela nyumbani tu.
Hii itasaidia vipi hawa kina mama na vijana
1.Hela zinakua safe
2.Unaweza chukua mkopo upanue biashara yako
3.Ukipatwa na shida ni rahisi kuzichukua hela kuliko kukaa nazo unaweza kuwa na matumizi ya ajabu.
Shime kwa TRA kufanyia tafiti hizi nyumba za wapangaji,biashara ndogo ndogo na kukusanya mapato.
Tanzania bora italetwa pale tutakapolipa kodi
Fred kavishe
Tanzania ni nchi yenye watu wanaokadiriwa milioni 50 bado tunasubiri report kamili ya sensa mwaka huu itatupa majibu tupo wangapi lakini cha kusangaza tunakusanya kidogo sana kuliko idadi ya wananchi na mali zetu nchini.
Kodi zetu kwa haraka zinatoka na mishahara ya waajiriwa,viwanda,makampuni,migodi(hapa tunadanganywa sana) na bidhaa kama chakula viwanji vya viminika.
Hivi nataka niwaulize TRA wanajua tanzania tuna watu wangapi wanapangisha nyumba zao na je wanawakata kodi hao watu.tuchukulie mfano ni wangapi wa nyumba osterbay,masaki,mbezi beach,njiro na maeneo mengine ambayo nyumba ni bei ghali.unakuta nyumba masaki ni dola 3000 kwa mwezi mtu anaingia pale analipia kwa mwaka mzima zaidi ya dola 36000 hivi sasa mtu ana nyumba hata 3 ambazo bei zake ni hizo je serikali imechukua kodi asilimia ngapi hapo.
Turudi huku mtaani sasa chumba 50000 unakuta mwenye nyumba ana vyumba hata 8 ina maana kwa mwezi ana 400000 je serikali inapata kodi kweli hapa maana naona nyumba nyingi unamlipa mwenye nyumba yenye anaenda lilipia kodi ya ardhi na nyumba ambayo ni 10000 tu.
Ni wakati sasa tuzijue nyumba zote za biashara serikali ukusanye kodi kwa kutokana na kile mwenye nyumba anachoingiza kwa mwezi na kwa mwaka ni wakati wa TRA kuanza kupita kwenye nyumba za watu na kuzisajili na kutoa vitabu mpangaji yoyote atakayelipa kodi awe anapewa risiti hii itaongeza kujua mwenye nyumba anaingiza kiasi gani.
Sijui kama kuna mfumo wa kuwabana wenye nyumba ambao wanaingiza pesa nyingi sana na hazilipiwi kodi kabisa ni uhakika kabisa hapa serikali inapoteza matapo na kungangania kuwabana wananchi kwenye vyakula na vinywaji.
Kingine kuna wakina mama wana migahawa barabarani sehemu za vitu kwa kuwa wanauza chakula hawakwati kodi jiulize kuna vijana wana vibanda vya chipsi kwa siku wanaingiza faida ya 20000-50000 je serikali inapataje kodi zao.
Ni wakati wa TRA kuandaa mfumo kwa wafanya biashara wote wenye vibanda barabarani kukatia TIN no na kufungiliwa account kwenye mabenk yaweke huduma nafuu ili hizi pesa zinazoenda kuwekwa nyumbani ziwekwe kwenye mabenk.
Mimi nadhani kama hawa kina mama,vijana wote watakatia TIN no hata TRA wakipata 2000 kwa mwezi kwa biashara na hizi hela wanazokusanywa wakaelezwa umuhimu wake wawe wanaziwekwa benk nchi yetu itapiga hatua kubwa sana tuseme mimi kijana nauza chips ninapata faida ya 30000 kwa siku labda kwa wiki naenda kuhifadhi bank 100000 kwa mwezi nina laki 4.sijaimalisha maisha yangu kuliko kukaa na ile hela nyumbani tu.
Hii itasaidia vipi hawa kina mama na vijana
1.Hela zinakua safe
2.Unaweza chukua mkopo upanue biashara yako
3.Ukipatwa na shida ni rahisi kuzichukua hela kuliko kukaa nazo unaweza kuwa na matumizi ya ajabu.
Shime kwa TRA kufanyia tafiti hizi nyumba za wapangaji,biashara ndogo ndogo na kukusanya mapato.
Tanzania bora italetwa pale tutakapolipa kodi
Fred kavishe