Kididimo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2016
- 3,791
- 3,360
Ili kusaidia TRA kukusanya mapato na malimbikizo yake kwa wepesi,nashauri hilo lifanyike. Hii itafanya wasiolipa kujitokeza kama wapo. Pia itapunguza malalamiko kwa waliotelekeza magari miaka mingi na kumbe hawayahitaji tena na hawakujua kuna sheria ya kuripoti na kuyafuta. Pia ni rahisi wezi wa magari kugundulika!kwani kwa kufutiwa usajili, magari yaliyofichwa yatapatikana wakati wa kurenew usajili. Naamini kwa utaratibu huu TRA watapata takwimu halisi ya idadi halisi ya magari yaliyopo,na makisio ya mapato kamili.