TRA fuatilieni hii kampuni ya wachina inayoitwa Hiview International Co Ltd, wanakwepa kodi sana

Awakomalie watarajesha tu,tena aambatane na maofisa wa TRA na TAKUKURU atawashika tu
Akikomaa inakula kwake,

Hazijui figisu za mjini uyu.

Akileta ujuaji,
Mzigo unataifishwa afu watu wa tra wanajifanya wamempiga faini feki muuzaji.

Kisha wanamwambia jamaa akungute matako yake haende maana kwa mujibu wa sheria Mali ya magendo hairudishwi kwa mhusika.

Afu baadae,
Jamaa wa maduka wanaenda kuwapoza tra kitu kidogo afu mzigo unawarudia wao wenyewe.

Mjini shule bwashee
 
unashangaa nini mbona hata TRA penyewe ukiingia ofisini unakutana na madalali wanaoweza kukuchezeshea ili kodi ipungue? labda kama ndio umeanza biashara hivi karibuni ndio utashangaa kusikia unaweza kukutana na dalali ndani ya ofisi flani
Atakua mgeni wa biashara uyu
 
Soma maelezo yangu vizuri.hakuna sehemu nimelia bei
Mkuu,
Kubali ukatae wee Ni mgeni kwenye biashara.

Kama na wenzio walokuelekeza ilo chimbo wangekua wanakamatwa na kupigwa izo faini kila siku,
bila shaka na wao wangeshafilisika na kamwe usingelijua pia ilo chimbo.

Wafanyabiashara wa JUMLA always huwa tunalindana.

HAKUNA Mfanyabiashara was JUMLA anaclaim exact efd receipt,

Miundo mbinu iko wazi na inaeleweka mjini kote.

Unakwama wapi mkuu?
 
hajawahi kuwepo kabisa na ukileta mambo ya professionalism kwenye biashara za Tanzania utapotea mapema sana kwenye scene, do what you do to survive, siri ya biashara za bongo unapaswa kumjua mtu anayemjua mtu, information is akey
Mtoa mada aliliparamia chimbo la watu kichwa kichwa.

Hakua na information Sahii ya Nini hatar ya alichokua anakifata.

Wengi Sana tumekumbwa na madhila ya hivi,
Na hatujawai Kuna apa Kuanzisha Uzi.

Na nimfahamishe mtu mtoa mada,
Kitendo alichokifanya kuweka details zake Kwenye Huu Uzi, ili kuwasagia kunguni wenzie.

Lawama zote zitaenda kwa waliokuelekeza pale.

Na always Kwenye biashara ukishajulikana hunaga kifua afu unatabia za snitch snitch,

kinachofata huwa Ni kukufungia tu vioo Kabisa na ikiwezekana kukupoteza Kabisa Kwenye ramani usiwaletee washkaji wengine jau.

Kama Kuna mtu wako wa karibu mnafanya biashara na ameuona huh Uzi wako,
Bila shaka utaona ambavyo mabadiliko jinsi gan hajafurahushwa na hiki ulichokifanya humu.
 
Ndugu,ukisoma maelezo yangu,mimi nimelipia full price nikiwa nahitaji documents zangu zote ili kuepusha usumbufu, kungekua na maelewano mengine wala hata nisingejisumbua kuleta huu uzi humu jf.na mbaya zaidi huyo Sylvester Katambi sijui ndio meneja wao ana mdomo mchafu balaa,hana customer care nzuri, hajataka kunielewesha vizuri yeye kaniachia msala.mpaka nimehisi huenda yeye ndiye amenifanyia huo uhuni.
Muuzaji kakujibu juu juu tu kwa maana anaaasume wee Ni mwenyeji wa hizi biashara na unajua utaratibu husika.

Niliwai mpeleka rafk angu mmoja kampuni flai Kwenye godown Moja kupakia mzigo.

Baada ya kuandika oda,
jamaa mchana kweupe kumbe tayar keshaanda fuso ije ipakie.

Afu asivyo na aibu,
baada ya kulipa akaomba risiti, Akapewa ya maandishi.
Ghafla kaanza kulalamikia eti anataka apewe ya efd.

Mhasibu akaingia ndani na kurudi na kitita Cha pesa zake zote (14.2million) na kumkabidhi na kumwambia "PESA ZAKO HIZI HAPA KANUNUE KWINGINE".

Niko zangu nje naongea na simu,
Jamaa anakuja analalamika eti hawana customer care nzuri wamenirudishia pesa.

Nkarudi ndai kujua tatizo Nini,

Wauzaji wanalalamika nimewaletea mtu wa ovyo afu mshamba Sana.

Ila baadae walimpa TU mzgo kupitia jina langu.
Kwa utaratibu ule ule ulozoeleka kwa wadau.

Kwaiyo watu Aina ya mtoa mada,
Mjini ni wengi
 
A
Mimi ni mjasirilismali,nina duka la matairi ya magari huku Mwanza.

Nilielekezwa kwenye hiyo kampuni tajwa hapo juu kuwa wanauza matairi ya jumla,basi nikafunga safari mpaka dar nikawatafuta mpaka ofisini kwao,ofisi zao ziko mikocheni sehemu inaitwa njia panda ya mawaziri.

Nilivyofika nikaandika order yangu nikalipia wakanipa risiti ya malipo tu,wakaniambia mzigo wangu wataupeleka wenyewe kwa transporter wangu na documents zote watampa transporter,nami sikuona ni tatizo kwani documents zinatakiwa ziambatane na mzigo njiani ili kuepuka usumbufu.

Kweli mzigo walipeleka kwa transporter lakini bila documents zozote, na mbaya zaidi siku hiyo TRA walikuwa na ukaguzi maeneo hayo ya Ilala hivyo mzigo wangu ukakamatwa na TRA, transporter akanijulisha hilo suala,nikawapigia wahusika kwa kutumia hizi number 0713174... na 0763235... ili kujua kulikoni. Hiyo number ya kwanza ni ya mtu niliyeambiwa anaitwa Sylvester Katambi ndiye meneja wa hiyo kampuni,huyo jamaa baada ya kumueleza shida yangu alichonijibu ni kuwa wao mzigo ukishafika kwa transporter hauwahusu tena na ana majibu mabaya sana utadhani sio Mtanzania. Sasa TRA wamenipiga fine ya 1.5m kwa makosa yaliyosababishwa na hao wapuuzi.

Nimejaribu kufanya uchunguzi kwa baadhi ya jamaa zangu Kariakoo kuhusiana na hii kampuni,wengi wanasema hawa jamaa ndiyo michezo yao hiyo,hawatoi risiti kwa wateja na mzigo ukikamatwa wao hawakusaidii chochote.

Wito wangu kwa TRA ifuatilieni hii kampuni kwa ukaribu muwachukulie hatua za kinidhamu kwa sababu wanafanya biashara za kihuni.

Nimeambatanisha risiti ya malipo waliyoniandikia ofisini kwao kama ushahidi.

View attachment 2032318
Asante Sana mzalendo wa kweli.Hawa TRA siku hizi wanafanya utani na makusanyo
 
Hii nchi ni tajiri Sana, naangalia michango ya nguli wa biashara wanavyokwepa kulipa Kodi wakishirikiana na TRA, alafu TRA hao hao ofisini wanajilipa mi-allowance ya kufa mtu....dah!

Rais aliomba maelezo ya kwanini polisi wengi wanagombamia wapangwe trafiki, sijuhi kama alijibiwa!
 
Hii nchi ni tajiri Sana, naangalia michango ya nguli wa biashara wanavyokwepa kulipa Kodi wakishirikiana na TRA, alafu TRA hao hao ofisini wanajilipa mi-allowance ya kufa mtu....dah!

Rais aliomba maelezo ya kwanini polisi wengi wanagombamia wapangwe trafiki, sijuhi kama alijibiwa!
Nchi ngumu Sana Hii mkuu, kila mtu anapambania ugali wake
 
Muuzaji kakujibu juu juu tu kwa maana anaaasume wee Ni mwenyeji wa hizi biashara na unajua utaratibu husika.

Niliwai mpeleka rafk angu mmoja kampuni flai Kwenye godown Moja kupakia mzigo.

Baada ya kuandika oda,
jamaa mchana kweupe kumbe tayar keshaanda fuso ije ipakie.

Afu asivyo na aibu,
baada ya kulipa akaomba risiti, Akapewa ya maandishi.
Ghafla kaanza kulalamikia eti anataka apewe ya efd.

Mhasibu akaingia ndani na kurudi na kitita Cha pesa zake zote (14.2million) na kumkabidhi na kumwambia "PESA ZAKO HIZI HAPA KANUNUE KWINGINE".

Niko zangu nje naongea na simu,
Jamaa anakuja analalamika eti hawana customer care nzuri wamenirudishia pesa.

Nkarudi ndai kujua tatizo Nini,

Wauzaji wanalalamika nimewaletea mtu wa ovyo afu mshamba Sana.

Ila baadae walimpa TU mzgo kupitia jina langu.
Kwa utaratibu ule ule ulozoeleka kwa wadau.

Kwaiyo watu Aina ya mtoa mada,
Mjini ni wengi
Ntakutafuta mkuu..nataka kuyajua vyema machimbo ya mjini.
 
pole jombaa.
ila ningekuwa ni mim hela wanatoa mzee tena ya ukweli. unakubalije kupigwa kirahc hivyo aisee! hao hao TRA ndio wakuwakamatisha. mi nakumbuka miaka hyo ninajenga kuna mhind aliniletea za kuleta nikampa General mmoja wa Jwz laki 3 akajifanya mzigo ni wake mi nilitumwa tu. kilichotokea yule mhind hatakaa anisahau aisee.
 
Kwa mfanyabiashara mzoefu.

Maelekezo aliyopewa mtoa mada Ni maelekezo common Sana kwa biashara za jumla kusafirisha mikoani.

Hamna kigeni wala janja janja pale.

Labda atwambie mtoa mada Ndo alikua anaanza biashara sikU iyo.

Hizo ajali Sio yeye TU,
Zimetukuta wengi Sana.

Ila the way unavyohandle ile situation, Ndo the way itaamua hatma yako khs mzgo husika.

Yaani Itoshe kusema TU,
Mtoa mada Ni mshamba,
afu limbukeni,
afu ana kiroho Cha kwanini.
Yaani kile kiroho Cha kimaskini.
Kile kiroho Cha Bora tukose wote.

Mtoa mada Ndo Aina ile ya watu enzi zile primary mmenda kuiba miwa ya babu,
Afu akakamatwa yeye tu Kisha akataja kua nilikua na flani na flani na flani.

Yaani anaona Ni furaha Sana mharibikiwe wote.

UYU JAMAA MIYEYUSHO SANA
Mkuu muwe mnaweka na risiti,sio kila mtu anataka janja janja yenu.
 
Akikomaa inakula kwake,

Hazijui figisu za mjini uyu.

Akileta ujuaji,
Mzigo unataifishwa afu watu wa tra wanajifanya wamempiga faini feki muuzaji.

Kisha wanamwambia jamaa akungute matako yake haende maana kwa mujibu wa sheria Mali ya magendo hairudishwi kwa mhusika.

Afu baadae,
Jamaa wa maduka wanaenda kuwapoza tra kitu kidogo afu mzigo unawarudia wao wenyewe.

Mjini shule bwashee
Duh,changamoto
 
Mkuu muwe mnaweka na risiti,sio kila mtu anataka janja janja yenu.
Wazalendo,
Huwa mnasehemu yenu ya kuchukulia mzigo kwa Bei kubwa afu mnapewa na risiti halali ya efd.

Sisi Wahujumu uchumi huwa tuna sehemu yetu rasmi ya kuchukulia mizigo kwa Bei rahisi zaidi afu kwa makubaliano ya hiari ya bila ya kupewa risiti but at your own risk.

Chaguo Ni lako, usuke au unyoe
 
Nahisi TRA wangekua serious, hata haya matozo ya kijinga yasingekuwepo kwa sasa.
Mama uku kwa wafanyabiashara keshaona maruweruwe tayar
Anacheza TU mziki wanaoutaka wafanyabiashara.

Ndo maana kakomaa na miamala maana uko kila kitu Kiko wazi
 
Ntakutafuta mkuu..nataka kuyajua vyema machimbo ya mjini.
Haina shida mkuu,
Hizi biashara usipozielewa miundo yake huwezi toboa apa mjini.

Utajikuta mshindani wako anauza Bei ya reja reja ndogo kuliko Bei yako wewe uliyonunulia mzigo wa jumla.
Mfano: umenunua CTN kwa 10,000 ili uuze 12,000 rejareja.
Afu Kuna jitu liko opposite na wewe linauza rejareja 8,000, na wale wanaonunuaga mzigo mkubwa linawashushia mpaka elfu 6 kila katoni

Wateja wote wanakuhama unaanza kumsingizia wachawi.

Kumbe machimbo huyajui, umezoea TU kwenda kununua maduka ya wachuuzi yanayoonekana usoni.

Wakati magwiji tunaendaga kupakia moja kwa moja godown au Kwenye makontena ya maboss uko majumbani mwao mizigo isiyokua na risiti, haijalipiwa ushuru wa bandari, Wala haijatozwa gharama za tbs na taka taka nyinginezo.

Tukifika sokoni,
Tunakukimbiza mchaka mchaka unarudi mwenyewe kijijini kwenu kulima mbaazi bila shuruti
 
Back
Top Bottom