TPDC yaingia mkataba na Kampuni ya Uingereza ya Baker Botts kwa ajili ya ushauri wa Kisheria

Zile zama za makampuni ya nje kupiga hela kwa mgongo wa ushauri zimerudi.

TPDC imeingia mkataba ya kampuni ya Uingereza za Baker Botts kwa ajili ya ushauriwa kisheria kwenye mikataba ya gesi.

Hivi Tanzania bado hatuna kampuni zenye uwezo wa kutoa ushauri wa kisheria hadi tutoe Ulaya?


View attachment 2095378


UPDATE: Jan 25, 2022

TPDC yalazimika kutoa ufafanuzi

UFAFANUZI KUHUSU UPATIKANAJI WA MSHAURI ELEKEZI (TRANSACTION ADVISOR) WA SERIKALI KATIKA MRADI WA KUCHAKATA NA KUSINDIKA GESI ASILIA (LIQUEFIED NATURAL GAS [LNG] PROJECT)

25 Januari, 2022

Mnamo tarehe 25 Januari 2022, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) na Kampuni ya Baker Botts (UK) LLP walisaini Mkataba wa Huduma ya Ushauri wa Kitaalam na Kampuni ya Baker Botts (UK) LLP ya Uingereza ili kushirikiana na Serikali katika majadiliano ya kutekeleza Mradi wa LNG.

Mchakato wa kumpata Mshauri Elekezi ulianza tarehe 12 Aprili 2018 ambapo TPDC ilitoa tangazo katika magazeti na tovuti mbalimbali kwa ajili ya kualika kampuni mbalimbali kuonesha nia ya kutekeza jukumu hilo kwa Serikali.

Tangazo hili lilichapishwa katika gazeti la Dailynews la tarehe 12 Aprili 2018 pamoja na kuwekwa katika tovuti za TPDC, UNDP na AfDB. Hadi kufikia tarehe 4 Mei 2018, kampuni 64 ziliwasilisha nia ya kushiriki katika zabuni tajwa.

Tathmini ya maombi yote ilifanyika kwa mujibu wa Sheria ya Manunuzi ya Mwaka ya 2011 ambapo Kampuni 3 kati ya 64 zilifanikiwa kutimiza vigezo vyote vilivyotumika katika tathmini na hivyo kuendelea na hatua zinazofuata ambayo ilihusisha ufunguzi wa mapendekezo ya kifedha (Financial Proposal). Hata hivyo, mchakato wa zabuni ulisimama kutokana na kusimamishwa kwa majadiliano baina ya Serikali na Wawekezaji.

Mwezi Novemba 2021, Serikali na Wawekezaji walikubaliana kuendeleza majadiliano. Hivyo, TPDC ilihuisha mchakato wa kumpata Mshauri Elekezi baada ya kushauriana na taasisi mbalimbali zinazosimamia manunuzi ya umma na mikataba. Mchakato huu ulikamika na kupelekea TPDC na Mzabuni aliyeshinda kusaini Mkataba tarehe 25 Januari, 2022.

Ikumbukwe kuwa Mradi wa LNG, ni mradi mkubwa na wa kwanza kutelekezwa hapa nchini. Mradi huu unahusisha kuvuna gesi asilia kutoka kwenye kina kirefu cha Bahari takribani kilometa tano kutoka usawa wa Bahari na kuisafirisha takribani kilometa 200 mpaka ufukwe wa Bahari ya Hindi katika eneo la Likong’o, Lindi kwa ajili ya kuichakata na kuisindika ili kuisafirisha kwenye masoko ya kimataifa na gesi nyingine kutumika kwa mahitaji ya ndani na ya kikanda. Mradi huu unatarajiwa kuwa na gharama ya takribani Shilingi trilioni sabini (70).

Kutokana na ukubwa na upekee wa Mradi huu, Serikali iliona umuhimu wa kushirikana na Mshauri Elekezi mwenye uzoefu wa utekelezaji wa miradi ya aina hii duniani ili kushauri kuhusu masuala ya kiufundi, kiuchumi, kifedha na kisheria.

Serikali ina lengo la kumtumia Mshauri Elekezi kwa ajili ya kupata ushauri stahiki hususani katika masuala ya teknolojia, kifedha na masoko ya kimataifa ili kuuza gesi iliyogundulika katika misingi ya ushindani na kulinda maslahi ya Taifa.

Kampuni ya Baker Botts (UK) LLP ni moja ya kampuni kubwa Duniani yenye uzoefu wa kimataifa wa kutoa ushauri wa kitaalam kwenye miradi ya aina hii. Kampuni hii itashirikiana na kampuni nyingine za kimataifa zenye ubobezi wa masuala ya teknolojia, kifedha na masoko. Vilevile, Kampuni hiyo itafanya kazi na Kampuni ya Kitanzania ya Apex Attorneys Advocates. Pia Kampuni hiyo itatoa mafunzo maalum kwa watanzania katika mada mbalimbali kuhusu Mradi ili kuwajengea uwezo wakati wa utekelezaji wa Mradi.

Imetolewa na:
Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano SHIRIKA LA MAENDELEO YA PETROLI TANZANIA​


B16D748A-24CC-4A57-8771-37362A375BDE.jpeg
 
Zile zama za makampuni ya nje kupiga hela kwa mgongo wa ushauri zimerudi.

TPDC imeingia mkataba ya kampuni ya Uingereza za Baker Botts kwa ajili ya ushauriwa kisheria kwenye mikataba ya gesi.

Hivi Tanzania bado hatuna kampuni zenye uwezo wa kutoa ushauri wa kisheria hadi tutoe Ulaya?


View attachment 2095378


UPDATE: Jan 25, 2022

TPDC yalazimika kutoa ufafanuzi

UFAFANUZI KUHUSU UPATIKANAJI WA MSHAURI ELEKEZI (TRANSACTION ADVISOR) WA SERIKALI KATIKA MRADI WA KUCHAKATA NA KUSINDIKA GESI ASILIA (LIQUEFIED NATURAL GAS [LNG] PROJECT)

25 Januari, 2022

Mnamo tarehe 25 Januari 2022, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) na Kampuni ya Baker Botts (UK) LLP walisaini Mkataba wa Huduma ya Ushauri wa Kitaalam na Kampuni ya Baker Botts (UK) LLP ya Uingereza ili kushirikiana na Serikali katika majadiliano ya kutekeleza Mradi wa LNG.

Mchakato wa kumpata Mshauri Elekezi ulianza tarehe 12 Aprili 2018 ambapo TPDC ilitoa tangazo katika magazeti na tovuti mbalimbali kwa ajili ya kualika kampuni mbalimbali kuonesha nia ya kutekeza jukumu hilo kwa Serikali.

Tangazo hili lilichapishwa katika gazeti la Dailynews la tarehe 12 Aprili 2018 pamoja na kuwekwa katika tovuti za TPDC, UNDP na AfDB. Hadi kufikia tarehe 4 Mei 2018, kampuni 64 ziliwasilisha nia ya kushiriki katika zabuni tajwa.

Tathmini ya maombi yote ilifanyika kwa mujibu wa Sheria ya Manunuzi ya Mwaka ya 2011 ambapo Kampuni 3 kati ya 64 zilifanikiwa kutimiza vigezo vyote vilivyotumika katika tathmini na hivyo kuendelea na hatua zinazofuata ambayo ilihusisha ufunguzi wa mapendekezo ya kifedha (Financial Proposal). Hata hivyo, mchakato wa zabuni ulisimama kutokana na kusimamishwa kwa majadiliano baina ya Serikali na Wawekezaji.

Mwezi Novemba 2021, Serikali na Wawekezaji walikubaliana kuendeleza majadiliano. Hivyo, TPDC ilihuisha mchakato wa kumpata Mshauri Elekezi baada ya kushauriana na taasisi mbalimbali zinazosimamia manunuzi ya umma na mikataba. Mchakato huu ulikamika na kupelekea TPDC na Mzabuni aliyeshinda kusaini Mkataba tarehe 25 Januari, 2022.

Ikumbukwe kuwa Mradi wa LNG, ni mradi mkubwa na wa kwanza kutelekezwa hapa nchini. Mradi huu unahusisha kuvuna gesi asilia kutoka kwenye kina kirefu cha Bahari takribani kilometa tano kutoka usawa wa Bahari na kuisafirisha takribani kilometa 200 mpaka ufukwe wa Bahari ya Hindi katika eneo la Likong’o, Lindi kwa ajili ya kuichakata na kuisindika ili kuisafirisha kwenye masoko ya kimataifa na gesi nyingine kutumika kwa mahitaji ya ndani na ya kikanda. Mradi huu unatarajiwa kuwa na gharama ya takribani Shilingi trilioni sabini (70).

Kutokana na ukubwa na upekee wa Mradi huu, Serikali iliona umuhimu wa kushirikana na Mshauri Elekezi mwenye uzoefu wa utekelezaji wa miradi ya aina hii duniani ili kushauri kuhusu masuala ya kiufundi, kiuchumi, kifedha na kisheria.

Serikali ina lengo la kumtumia Mshauri Elekezi kwa ajili ya kupata ushauri stahiki hususani katika masuala ya teknolojia, kifedha na masoko ya kimataifa ili kuuza gesi iliyogundulika katika misingi ya ushindani na kulinda maslahi ya Taifa.

Kampuni ya Baker Botts (UK) LLP ni moja ya kampuni kubwa Duniani yenye uzoefu wa kimataifa wa kutoa ushauri wa kitaalam kwenye miradi ya aina hii. Kampuni hii itashirikiana na kampuni nyingine za kimataifa zenye ubobezi wa masuala ya teknolojia, kifedha na masoko. Vilevile, Kampuni hiyo itafanya kazi na Kampuni ya Kitanzania ya Apex Attorneys Advocates. Pia Kampuni hiyo itatoa mafunzo maalum kwa watanzania katika mada mbalimbali kuhusu Mradi ili kuwajengea uwezo wakati wa utekelezaji wa Mradi.

Imetolewa na:
Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano SHIRIKA LA MAENDELEO YA PETROLI TANZANIA​


E523289C-9B73-4893-B62C-326A28B2F9FC.jpeg
 
sasa kwa nini mashuleni tunatumia kiingereza?
Boss hujui kweli hilo? Tumeachiwa nchi na mkoloni na official language Kiingereza na tulilishwa madini Kiingereza ni bora kuliko lugha yetu ya Kiswahili, na utaalam wetu mwingi tumesomea kwao kwa lugha ya kiingereza, na njaa zetu hizi kuanza kuweka kila kitu kiswahili sina uhakika
 
Bado naisubiri kwa hamu sana hiyo Tanzania ya kuongozwa na Makamba🤣, na nitakuwa radhi kwenda kuishi Rwanda ila sio Tanzania ya kuongozwa na Makamba. ......................................................................................................................................................... 2030 Ruagwa ni lazima hao wengine watasindikiza tu.
Historia ya Tz inatuambia kwamba PMs hawawi Marais (except Nyerere). Msuya alijaribu hakuwa, Malecela alijaribu hakuwa, Sumaye alijaribu hakuwa, Salim Ahmed alijaribu hakuwa, Lowassa alijaribu hakuwa, Pinda alijaribu hakuwa, Majaliwa atajaribu na hatokuwa...

Wakati fulani nafikiri ni bora kuwa Waziri wa Mambo ya Nje kuliko kuwa Waziri Mkuu kama unataka kugombea Urais wa JMT.

Kikwete alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje akaja kuwa rais, Big Ben (Mkapa) alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje akaja kuwa rais.
 
Namuona Mataragio akisaini na huyu muingereza, matumaini ni kwamba nia ni njema kwa taifa.

Maana Samia anachukuliwa kama ni kivuli cha JK ambaye haaminiwi na kundi lililomuamini JPM. Ni kazi ya kina January kuonyesha kwamba imani hii potofu juu ya awamu ya sita ni potofu kweli.

Uwe ni uzalendo kwa asilimia mia moja, ingawa uzalendo wa kweli ni siri ya moyo wa mtu, hauwezi kuonwa wala kutazamwa kwa macho ya kibinadamu.
 
Kazi gani anayoifanya ndugu zaidi ya kutumia muda wake kuunyesha umma wa Tanzania that he is there, Kazi ilisha mshinda. Wala sina majungu dhidi yake na nina muheshimu sana kwani yeye ni chaguo na pia nakukumbusha aliye muweka amemuweka kwaajili yetu wanyonge. :D
Wakati fulani public perception inani-drive kutamani kwamba kama hekima ilimuongoza mama kurudisha mtu wa zamani kwenye cabinet aliyekwishashindwa na kuondolewa basi bora angemrudisha Mhe. Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo (MB) kwa sababu ni Tecnocrat and Institutional Memory kwenye wizara hiyo, sekta hiyo, taaluma hiyo kwa viwango vilivyotukuka kitaifa na kimataifa KUMZIDI Makamba.

Naamini Muhongo angesimamia maslahi ya nchi kama alivyofanya kwamba wawekezaji mmoja mmoja wazawa kwenye uchumi wa gesi wata-pool mitaji yao chini ya uangalizi, uwakala na uratibu wa TPDC badala ya mtu binafsi.

Japo leo sijajuwa TPDC inaposukumwa ku-hire consultant wa kigeni kwa gharama kubwa za mabilioni je, gharama hizo zitalipwa toka kwenye hisa za serikali au kwenye hisa za wananchi mmoja mmoja walio-pool rasilimali zao TPDC?

1643289418847.png

Taswira kwa hisani ya google.
 
Historia ya Tz inatuambia kwamba PMs hawawi Marais (except Nyerere). Msuya alijaribu hakuwa, Malecela alijaribu hakuwa, Sumaye alijaribu hakuwa, Salim Ahmed alijaribu hakuwa, Lowassa alijaribu hakuwa, Pinda alijaribu hakuwa, Majaliwa atajaribu na hatokuwa...

Wakati fulani nafikiri ni bora kuwa Waziri wa Mambo ya Nje kuliko kuwa Waziri Mkuu kama unataka kugombea Urais wa JMT.

Kikwete alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje akaja kuwa rais, Big Ben (Mkapa) alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje akaja kuwa rais.
😅
 
Namuona Mataragio akisaini na huyu muingereza, matumaini ni kwamba nia ni njema kwa taifa.

Maana Samia anachukuliwa kama ni kivuli cha JK ambaye haaminiwi na kundi lililomuamini JPM. Ni kazi ya kina January kuonyesha kwamba imani hii potofu juu ya awamu ya sita ni potofu kweli.

Uwe ni uzalendo kwa asilimia mia moja, ingawa uzalendo wa kweli ni siri ya moyo wa mtu, hauwezi kuonwa wala kutazamwa kwa macho ya kibinadamu.
Ni ajabu sana kwamba hata mabeberu wanathamini uzalendo ilhali mafisadi hawana uzalendo katu.

Hii inamfanya beberu aonekane kama malaika na fisadi aonekane kama ibilisi kwa sababu beberu ana wajibu wa kuona himaya ya nchi yake inakuwa endelevu wakati fisadi ana jukumu kubwa la msingi la kuhujumu na kufisha kila kinachotafutwa kwa ajili ya kuendeleza taifa.

Kwa hulka hizi, ni rahisi kwa beberu kupenya tundu la sindano kuliko fisadi. Mabeberu wako kwa mujibu wa mfumo, itikadi na sheria za mataifa yao ambazo hizi zinatambua uwepo wao, lakini mafisadi wanazuka nje ya wigo wa sheria na wala hawana itikadi ya kusimamia.

Kuondoa ubeberu kunahitaji kufanya mabadiliko ya mfumo, itikadi na sheria ila kuondoa ufisadi kunahitaji dhamira ya kizalendo tu maana hauna uhalali wa kuwepo kisheria.

Iko siku Tz itarejea kwenye Azimio la Arusha ikiwa imeishakomba rasilimali ambazo Azimio hilo la Arusha lingetakiwa kuzilinda!
 
Ni ajabu sana kwamba hata mabeberu wanathamini uzalendo ilhali mafisadi hawana uzalendo katu.

Hii inamfanya beberu aonekane kama malaika na fisadi aonekane kama ibilisi kwa sababu beberu ana wajibu wa kuona himaya ya nchi yake inakuwa endelevu wakati fisadi ana jukumu kubwa la msingi la kuhujumu na kufisha kila kinachotafutwa kwa ajili ya kuendeleza taifa.

Kwa hulka hizi, ni rahisi kwa beberu kupenya tundu la sindano kuliko fisadi. Mabeberu wako kwa mujibu wa mfumo, itikadi na sheria za mataifa yao ambazo hizi zinatambua uwepo wao, lakini mafisadi wanazuka nje ya wigo wa sheria na wala hawana itikadi ya kusimamia.

Kuondoa ubeberu kunahitaji kufanya mabadiliko ya mfumo, itikadi na sheria ila kuondoa ufisadi kunahitaji dhamira ya kizalendo tu maana hauna uhalali wa kuwepo kisheria.

Iko siku Tz itarejea kwenye Azimio la Arusha ikiwa imeishakomba rasilimali ambazo Azimio hilo la Arusha lingetakiwa kuzilinda!
Ubeberu ni dhana zilizoko huku afrika. Zipo kichwani zaidi na ni za kihisia kuliko uhalisia. Huyo huyo mzungu anayejenga hospitali huko Muhutwe au munjebwe anaitwa rafiki wa maendeleo lakini akifanya kama mtoto wa Margret Thatcher kutaka kuipindua nchi fulani ya afrika ndio anaitwa beberu.

Ufisadi husababishwa na sababu nyingi kwa wakati mmoja. Tamaa ya mali inayoambatana na mimi peke yangu ndio nipate. Malengo ya kweli ya kutaka kuwa mfanya biashara mkubwa na anayeishi vizuri na familia yake. Dhuluma kwa maana ya neno lenyewe. Zote hizo ni sifa za ufisadi.

Lakini kisichokuwa cha kwako huwa hakiliki hata siku moja. Kama umepangiwa na Mungu upate kitu fulani hata wakiziba kwa namna ipi utapata tu.

Na tatizo la ufisadi unakuwa na mali ambazo kiuhalisia sio haki yako, ni jasho la walipa kodi wenye kuishi wakiwa wananung'unika kila kukicha hivyo kuwa na hizo mali za wizi hata kama ni wa kisomi kwa namna ipi bado ni kama umeshikilia tu kitu kisichokuwa cha kwako.

Baba yangu mzazi aliwahi kuniambia miaka ya nyuma kuwa mali ya wizi (ufisadi) huwa haimfikii mjukuu hata siku moja, huisha kwa aibu inayoyafuata maisha ya mwizi husika. Pia huambatana na maisha ya wasiwasi, simu ikilia mhusika anajua ni jamaa wa TAKUKURU wanampigia mapigo ya moyo yanaanza kwenda kasi, ilimradi hana amani na mali ambayo sio ya kwake.
 
Historia ya Tz inatuambia kwamba PMs hawawi Marais (except Nyerere). Msuya alijaribu hakuwa, Malecela alijaribu hakuwa, Sumaye alijaribu hakuwa, Salim Ahmed alijaribu hakuwa, Lowassa alijaribu hakuwa, Pinda alijaribu hakuwa, Majaliwa atajaribu na hatokuwa...

Wakati fulani nafikiri ni bora kuwa Waziri wa Mambo ya Nje kuliko kuwa Waziri Mkuu kama unataka kugombea Urais wa JMT.

Kikwete alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje akaja kuwa rais, Big Ben (Mkapa) alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje akaja kuwa rais.
Ni rahisi kwa waziri mkuu kuhusishwa na matokeo mabovu ya watendaji wengine kwa maana ya mawaziri wenzake.

Ni cheo ambacho mema yako hayaonekani hata kama ni mengi sana lakini baya moja tu linakuondoa.
 
3099CC47-78B0-4E56-9149-294B61837F93.png

D5D9FC93-AF05-4EFA-82AF-764A53C8057A.png


Huyo ndio main senior partner wa hiyo Law ame specialise kwenye mikataba ya mafuta na Gas.

He has background ya accounts why is that important main aspect ya contract consideration kwenye natural resources ni finances. Sasa ina maana kama nchi hatuna accountants wakujadili hayo mambo.

Hatuna wataalamu wengine wa kujadili vipengele vingine kama vya mazingira in terms of environmental costs and so forth. Hao watu lazima wapo. Wana sheria wana draft tu mkataba in legal terms in the end.

Mambo mengine ni ignorance tu ya viongozi wetu; huko nyuma mbona watu hao hao walikuwa wanajadiliana bila ya consultants.

Matumizi mabaya ya hela za serikali na uwezo wa mdogo wa waziri kwenye sector ndio unapelekea mambo kama haya.
 
Ubeberu ni dhana zilizoko huku afrika. Zipo kichwani zaidi na ni za kihisia kuliko uhalisia. Huyo huyo mzungu anayejenga hospitali huko Muhutwe au munjebwe anaitwa rafiki wa maendeleo lakini akifanya kama mtoto wa Margret Thatcher kutaka kuipindua nchi fulani ya afrika ndio anaitwa beberu.

Ufisadi husababishwa na sababu nyingi kwa wakati mmoja. Tamaa ya mali inayoambatana na mimi peke yangu ndio nipate. Malengo ya kweli ya kutaka kuwa mfanya biashara mkubwa na anayeishi vizuri na familia yake. Dhuluma kwa maana ya neno lenyewe. Zote hizo ni sifa za ufisadi.

Lakini kisichokuwa cha kwako huwa hakiliki hata siku moja. Kama umepangiwa na Mungu upate kitu fulani hata wakiziba kwa namna ipi utapata tu.

Na tatizo la ufisadi unakuwa na mali ambazo kiuhalisia sio haki yako, ni jasho la walipa kodi wenye kuishi wakiwa wananung'unika kila kukicha hivyo kuwa na hizo mali za wizi hata kama ni wa kisomi kwa namna ipi bado ni kama umeshikilia tu kitu kisichokuwa cha kwako.

Baba yangu mzazi aliwahi kuniambia miaka ya nyuma kuwa mali ya wizi (ufisadi) huwa haimfikii mjukuu hata siku moja, huisha kwa aibu inayoyafuata maisha ya mwizi husika. Pia huambatana na maisha ya wasiwasi, simu ikilia mhusika anajua ni jamaa wa TAKUKURU wanampigia mapigo ya moyo yanaanza kwenda kasi, ilimradi hana amani na mali ambayo sio ya kwake.
Kila zama na wahanga wake:-

1. Mwl Nyerere: GAPEX kashfa ya Nyakyoma.

2. Mwinyi: V.G. Chavda na P.G. Chavda $3.5 million za debt conversion program (DCP) 1993 kwa ajili ya mashamba ya katani. Agustino Mrema na wanasiasa wengine walitajwa kunufaika lakini wakafanikiwa kukwepa mkono wa sheria.

Mwinyi: 1995 kashfa ya Mohamed Enterprises ya kusambaza chakula kisichofaa kwa matumizi ya binadamu. Agustino Mrema akaondoka CCM na serikalini.

Mwinyi: 1992 Agustino Mrema alikamata dhahabu ya thamani ya $36,000 JKNIA ikatajwa ni mali ya mkubwa..

3. Big Ben: BoT kwenye bajeti ya 2005/6 ililipa $116 million toka kwenye akaunti ya madeni EPA.

Big Ben: 2001 Idd Simba ajiuzulu kwa kashfa ya sukari. Mporogomyi naye alivuliwa (sikumbuki kwa kashfa ya nini vile sijui minofu ya sangara?)

Big Ben: Ununuzi wa hisa za Kiwira Coal Mine.

Big Ben: Ununuzi wa rada na ndege ya rais, Basil Mramba, Gray Mgonja na Daniel Yona wa mradiakaingia matatani.

4. Kikwete: Waziri wa Ardhi Tibaijuka na AG Frederick Werema wang'olewa kwa kashfa ya Escrow iliyohusu fedha zilizochotwa (Tiba alikuwa mmoja wa wanufaika) ambazo zilihusu wadau wa mradi wa ufuaji umeme IPTL na Tanesco kwa upande wa serikali na fungu kuiendea PAP iliyokuwa mmiliki wa mradi.

5. Magufuli: 2017 Makinikia za thamani ya zaidi ya Tzs.400 tr zamwondoa Sospeter Mwijarubi Muhongo.

2020 $458 ml za drone zamwondoa Kangi Alphaxard Lugola.

NB.
Samia Suluhu naye atakuwa na mbuzi wake wa kafara, hawakosekani na haikwepeki kwenye siasa.
 
Kila zama na wahanga wake:-

1. Mwl Nyerere: GAPEX kashfa ya Nyakyoma.

2. Mwinyi: V.G. Chavda na P.G. Chavda $3.5 million za debt conversion program (DCP) 1993 kwa ajili ya mashamba ya katani. Agustino Mrema na wanasiasa wengine walitajwa kunufaika lakini wakafanikiwa kukwepa mkono wa sheria.

Mwinyi: 1995 kashafa ya Mohamed Enterprises ya kusambaza chakula kisichofaa kwa matumizi ya binadamu. Agustino Mrema akaondoka CCM na serikalini.

Mwinyi: 1992 Agustino Mrema alikamata dhahabu ya thamani ya $36,000.

3. Big Ben: BoT kwenye bajeti ya 2005/6 ililipa $116 million toka kwenye akaunti ya madeni.

Big Ben: 2001 Idd Simba ajiuzulu kwa kashafa ya sukari. Mporogomyi naye alivuliwa (sikumbuki kwa kashfa ya nini vile sijui minofu ya sangara?)

Big Ben: Ununuzi wa hisa za Kiwira Coal Mine.

4. Kikwete: Waziri wa Ardhi Tibaijuka na AG Frederick Werema wang'olewa kwa kashfa ya Escrow iliyohusu fedha zilizochotwa (Tiba alikuwa mmoja wa wanufaika) ambazo zilihusu wadau wa mradi wa ufuaji umeme IPTL na Tanesco kwa upande wa serikali na fungu kuiendea PAP iliyokuwa mmiliki.

5. Magufuli: 2017 Makinikia za thamani ya zaidi ya Tzs.400 tr zamwondoa Sospeter Mwijarubi Muhongo.

2020 $458 ml za drone zamwondoa Kangi Alphaxard Lugola.

NB.
Samia Suluhu naye atakuwa na mbuzi wake wa kafara, hawakosekani na haikwepeki kwenye siasa.
Hatuwezi kuwa sawa, Mtihani ni mmoja wanafundishwa wanafunzi 100. Mmoja anakuwa wa kwanza na mmoja anakuwa wa mwisho.

Ni mapambano mpaka dakika ya mwisho tunapokwenda kaburini.
 
View attachment 2097589
View attachment 2097590

Huyo ndio main senior partner wa hiyo Law ame specialise kwenye mikataba ya mafuta na Gas.

He has background ya accounts why is that important main aspect ya contract consideration kwenye natural resources ni finances. Sasa ina maana kama nchi hatuna accountants wakujadili hayo mambo.

Hatuna wataalamu wengine wa kujadili vipengele vingine kama vya mazingira in terms of environmental costs and so forth. Hao watu lazima wapo. Wana sheria wana draft tu mkataba in legal terms in the end.

Mambo mengine ni ignorance tu ya viongozi wetu; huko nyuma mbona watu hao hao walikuwa wanajadiliana bila ya consultants.

Matumizi mabaya ya hela za serikali na uwezo wa mdogo wa waziri kwenye sector ndio unapelekea mambo kama haya.
Makamba yeye anamini kila kitu kizuri lazim kitoke nje .juzi hapa kawapa wwhindi tenda ya software as humo ndani hatuna hao watu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Makamba yeye anamini kila kitu kizuri lazim kitoke nje .juzi hapa kawapa wwhindi tenda ya software as humo ndani hatuna hao watu

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu, nitajie kampuni yoyote ya kitanzania ambayo ipo juu kwenye masuala ya kutengeneza software solutions na zikakubalika kimataifa.

Kuna masuala mengine sisi kama watanzania hatuyawezi hata kule DTI hakuna kitu.
 
Mkuu, nitajie kampuni yoyote ya kitanzania ambayo ipo juu kwenye masuala ya kutengeneza software solutions na zikakubalika kimataifa.

Kuna masuala mengine sisi kama watanzania hatuyawezi hata kule DTI hakuna kitu.
Watu kama nyie mnafurahisha kweli umeshawahi kuangalia documentary yoyote ya cyber war.

Watu wanatumiana salamu kwa kuingilia infrastructures za nchi, Iran mitambo yao nuclear enrichment ilipoingiliwa walirudisha salamu kwa kuzima traffic lights na kuchezea kidogo New York subway kwa lengo la kuonyesha ata wao wakiamua wanaweza peleka mazara U.S.

U.S wenyewe na wao wakadai wana uwezo huohuo wakiamua kuingilia mifumo yao mpaka ya maji na kupeleka madhara makubwa aijatokea.

Wewe unashangilia system ya TANESCO kutengenezwa na wahindi halafu kusimamiwa in real time India; we might as well tell them where the nation stores its military ammunition’s.

It’s just stupid, ata watu wakishanunua ndege za vita kitu cha kwanza wana configure electronic systems zake, usidhani waarabu wananunua tu ndege US na software za US.

............................

Na ata hiyo tender ya TPDC ilikuwa kwa ajili ya consultants kuja kuwanoa wataalamu kabla ya majadiliano kuanza; waingie wamejipanga. Sio consultant aje au ashiriki kipindi cha majadiliano na kuweka influence zake.
 
Back
Top Bottom