BWANKU M BWANKU

JF-Expert Member
Jan 12, 2019
328
414
Mamlaka ya usimamizi wa bandari Tanzania (TPA) Leo Jumatano Machi 16, 2022 imeingia makubaliano ya kibiashara na kiwanda cha Saruji cha Dangote kilichopo Mkoani Mtwara yenye lengo la kurahisisha usafirishaji wa Saruji kwa kutumia bandari ya Mtwara.

Makubaliano hayo Yanawezesha kampuni ya Dangote kutumia bandari ya Mtwara , Tanga na Dar es salaam na yanatarajiwa kuongeza uzalishaji wa saruji katika kiwanda hicho kutoka tani 15000 za mwanzo mpaka 43000 kwa mwezi .

Akizungumza kwenye Hafla hiyo ya Utiaji Saini Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Brig. Jen. Marco Gaguti amesema hatua hii ni mafanikio ya Serikali ya Rais Samia kuweka mazingira mazuri na wezeshi kwa Wafanyabiashara na Wawekezaji kufanya biashara bila kugudha yoyote huku mazingira yakiwa yameboreshwa sana.

Makubaliano hayo pia yameshuhudiwa na viongozi mbalimbali wa Mkoa akiwemo Mkuu wa mkoa wa Mtwara Mhe. Brig. Jen. Marco Gaguti, Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Dunstan Kyobya na Viongozi wengine mbalimbali.

IMG-20220316-WA0032.jpg


IMG-20220316-WA0031.jpg


IMG-20220316-WA0017.jpg


IMG-20220316-WA0018.jpg


IMG-20220316-WA0023.jpg


IMG-20220316-WA0024.jpg


IMG-20220316-WA0025.jpg


IMG-20220316-WA0028.jpg
 
Bandari ya Mtwara au huo mkataba namna gani unaongeza huo uzarishaji kutoka 15000 to 43000 kwenye hicho kiwanda cha Dangote...? Muandishi hebu tuweke sawa hapo..

Hicho kiwanda, installed capacity ni 6000ton per day, malighafi kwa kiasi kikubwa inapatikana hapo hapo Mtwara, Coal wanapata songea japo kwa sasa wanatumia Gas ambayo iko hapo hapo mtwara....Hebu tuambieni hiyo bandari itaongeza vipi huo uzarishaji?
 
Bandari ya Mtwara au huo mkataba namna gani unaongeza huo uzarishaji kutoka 15000 to 43000 kwenye hicho kiwanda cha Dangote...? Muandishi hebu tuweke sawa hapo..

Hicho kiwanda, installed capacity ni 6000ton per day, malighafi kwa kiasi kikubwa inapatikana hapo hapo Mtwara, Coal wanapata songea japo kwa sasa wanatumia Gas ambayo iko hapo hapo mtwara....Hebu tuambieni hiyo bandari itaongeza vipi huo uzarishaji?
Mkuu, moja kati ya limitation ni warehousing na logistics. Huwezi kuzalisha zaidi ya uwezo wako wa kuhifadhi au kusafirisha. Kuhifadhi kuna gharama sana, na kusafirisha kwa malori nako ni gharama sana. Wakiweza kutumia meli, wataweza kusambaza mzigo haraka, na kuweza kuzalisha zaidi.
 
Mamlaka ya usimamizi wa bandari Tanzania (TPA) Leo Jumatano Machi 16, 2022 imeingia makubaliano ya kibiashara na kiwanda cha Saruji cha Dangote kilichopo Mkoani Mtwara yenye lengo la kurahisisha usafirishaji wa Saruji kwa kutumia bandari ya Mtwara...
It creates trust between the private sector and the public sector which will in turn stimulate the economy positively,,,,,,,

let the private sector be confident, get stronger, invest more, generate more jobs and income to create a favourable tax base for the government machinery and low cost of the final products for the final consumers

Positive move....
 
Back
Top Bottom