Uncle Jei Jei
JF-Expert Member
- Jan 7, 2011
- 1,684
- 2,157
Binafsi nimefanikiwa sana kuzunguka mikoa kadhaa ya nchi kwa kazi maalumu za miradi ya afya. Kwa sehemu kubwa nimejionea namna zahanati zilivyojengwa hadi vijijini kabisa
Tatizo kubwa la nchi hii ni zahanati hizo kukosa wahudumu hasa za vijijini, dawa na vifaa tiba
Zahanati ili ikamilike haitegemei jengo pekee. Zahanati/kituo Cha afya/ hospital ni jumla ya jengo, wahudumu, vifaa tiba na dawa.
Jengo hata likiwa zuri kiasi gani na rangi za kupendeza Kama hakuna wahudumu na dawa ni kazi bure!
Tuboreshe vilivyopo kwanza tuokoe maisha ya wananchi wetu! Hebu angalia yule tabibu wa Korogwe aliyefumua nyuzi jeraha la mgonjwa wake kisa tu ameshindwa kulipa hela ya huduma!
Serikali ingewekeza zaidi kwenye upatikanaji wa dawa na vifaa tiba kirahisi kuliko majengo hata huduma za afya zingekuwa nafuu sana!
Ukija kwenye Shule hali ni hiyo hiyo. Madiwani wamekazana kujenga maboma pasipokuyakamilisha na ukiangalia idadi kubwa ya wanafunzi wanakaa chini kwa kukosa madawati
Shule hazina vyoo bora, hazina ofisi ila zimejaa maboma yasiyokamilika
Madarasa hayakarabatiwi ila wamekazana kujenga maboma
Maabara toka enzi za Lowasa ni maboma kwa sehemu kubwa. Sasa unajiuliza, hizi gharama za maboma zingetumika kuboresha madarasa na kutengeneza madawati si Shule zingependeza na kuvutia wanafunzi kujifunza?
Wanajenga madarasa kwa kisingizio Cha kupunguza msongamano lakini hayakamiliki. Msongamano unabaki pale pale, uchakavu unabaki pale pale na uhaba wa madawati unabaki pale pale kinachoongezeka ni 'unfinished buildings"
Tatizo kubwa la nchi hii ni zahanati hizo kukosa wahudumu hasa za vijijini, dawa na vifaa tiba
Zahanati ili ikamilike haitegemei jengo pekee. Zahanati/kituo Cha afya/ hospital ni jumla ya jengo, wahudumu, vifaa tiba na dawa.
Jengo hata likiwa zuri kiasi gani na rangi za kupendeza Kama hakuna wahudumu na dawa ni kazi bure!
Tuboreshe vilivyopo kwanza tuokoe maisha ya wananchi wetu! Hebu angalia yule tabibu wa Korogwe aliyefumua nyuzi jeraha la mgonjwa wake kisa tu ameshindwa kulipa hela ya huduma!
Serikali ingewekeza zaidi kwenye upatikanaji wa dawa na vifaa tiba kirahisi kuliko majengo hata huduma za afya zingekuwa nafuu sana!
Ukija kwenye Shule hali ni hiyo hiyo. Madiwani wamekazana kujenga maboma pasipokuyakamilisha na ukiangalia idadi kubwa ya wanafunzi wanakaa chini kwa kukosa madawati
Shule hazina vyoo bora, hazina ofisi ila zimejaa maboma yasiyokamilika
Madarasa hayakarabatiwi ila wamekazana kujenga maboma
Maabara toka enzi za Lowasa ni maboma kwa sehemu kubwa. Sasa unajiuliza, hizi gharama za maboma zingetumika kuboresha madarasa na kutengeneza madawati si Shule zingependeza na kuvutia wanafunzi kujifunza?
Wanajenga madarasa kwa kisingizio Cha kupunguza msongamano lakini hayakamiliki. Msongamano unabaki pale pale, uchakavu unabaki pale pale na uhaba wa madawati unabaki pale pale kinachoongezeka ni 'unfinished buildings"