Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,480
- 30,152
Habari za kusikitisha sana ni kuwa zile tozo kubwa Sana za simu zilizopitishwa kwenye bajeti na Bunge letu, zilizotangazwa na waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba, zinaanza kutumika rasmi leo na kuwaumiza sana wananchi wanyonge wa nchi hii
Kwa hakika ni kilio kikubwa kwa mamilioni ya wananchi wanyonge ambao walikuwa wameona makampuni ya simu yamewaletea afueni katika kutumiana miamala ya simu.
Ni jambo linaloshangaza kuona vile wabunge wa CCM waliamua kuipitisha bajeti hiyo ya uonevu mkubwa kwa asilimia 100!
Ndipo hapo Taifa hili linapoona umuhimu wa hali ya juu kuwa na Katiba mpya ya nchi, ambapo wananchi wenyewe ndiyo tutakaokuwa na kauli ya namna ya kuiendesha Nchi hii badala ya mfumo wa sasa ambapo Chama cha Mapinduzi (CCM) ndicho kinachoamini kuwa kina hati miliki ya kutawala nchi hii na kutuona wananchi tuliobakia kukubaliana na maamuzi yanayofanywa na chama hicho cha CCM
Kwa hakika ni kilio kikubwa kwa mamilioni ya wananchi wanyonge ambao walikuwa wameona makampuni ya simu yamewaletea afueni katika kutumiana miamala ya simu.
Ni jambo linaloshangaza kuona vile wabunge wa CCM waliamua kuipitisha bajeti hiyo ya uonevu mkubwa kwa asilimia 100!
Ndipo hapo Taifa hili linapoona umuhimu wa hali ya juu kuwa na Katiba mpya ya nchi, ambapo wananchi wenyewe ndiyo tutakaokuwa na kauli ya namna ya kuiendesha Nchi hii badala ya mfumo wa sasa ambapo Chama cha Mapinduzi (CCM) ndicho kinachoamini kuwa kina hati miliki ya kutawala nchi hii na kutuona wananchi tuliobakia kukubaliana na maamuzi yanayofanywa na chama hicho cha CCM