Tozo ilipokuwa kwenye Bia hayatuhusu, Tozo kwenye umeme na miamala kidogo tu watu hoi

GUSSIE

JF-Expert Member
Dec 2, 2014
3,866
11,099
Wanabodi kuna vitu ni luxiory na vingine Necessity. Luxiory kwako yaweza kikawa necessity kwa mtu mwingine na hivyo hivyo necessity kwako yaweza ikawa luxiory kwa mtu mwingine.

Kitu au mahitaji kuwa muhimu au sio muhimu inategemea na chaguo la mtu husika

"Serikali iache kutoza bia kila mwaka". Huu ndio usemi ulikuwa wa watanzania serikali itafute vyanzo mbadala vya mapato kwa miaka zaidi ya thelathini( 30).Kutegemea kodi kwenye Bia ni aibu kubwa kwa imani ya baadhi ya watu hapa JF na kwa afya za watanzania bia hazifai zina Madhara mengi kiafya( Viongozi wa afya na dini walihimiza na wanahimiza bia hazifai Tuache)

Maombi yamekubalika, Wanywa bia na watoa ofa walipungua sana enzi za JPM watu waliishia kunywa bia za "Serengeti lite na Castle lite " bei yake imedumu kwa TZS 1,500 kwa miaka mitano ni bei chini ya dola moja za kimarekani, Makampuni ya bia Haya kutengeneza faida kubwa kama watu tulivyozoea kwa miaka mitano

Output ya bia iliyozalishwa *TZS 1500*Idadi ya walevi =Revenue Generated

Kama idadi ya walevi ni Zero hivyo Revenue ni Zero

Bunge la chama kimoja cha ccm wameamua kuwapa watanzania mbadala wa kodi ili Taifa lisonge mbele kwa manufaa, Ni kodi ya hiari kabisa

Una hiari ya kuacha kununua umeme ili kukwepa kodi ya elfu moja TZS 1,000 kwa mwezi, ukaamua kulala giza.

Una hiari ya kuacha kutuma au kutoa pesa kwenye wallet za simu Tigo pesa, M Pesa au Airtel Money. U kaamua kukaa na pesa ndani

Nimeandika hii mada baada ya kutembelea rafiki zangu wakiwa Bar wanaangalia mpira na kukuta mjadala huu kuwa mbona watanzania wanakuwa wagumu kuchangia Taifa Lao wakati wao wameamua kupunguza matumizi ya pombe kwa afya zao

Kutegemea kodi ya pombe huku wale vi wakipungua kwa mahubiri mazuri na wakovu Hakika Taifa litaangamia

Hakuna njia mbadala ya kupata mapato kwa sasa kwa mujibu wa Spika Ndugai, Na amehoji mwenye njia mbadala ya kupata mapato atoe maoni yake ( Spika Ndugai)

Njia tulizisoma darasani zote tumezitumia kama :
kukopa (loans) serikali imekopa mpaka watu wanatukana kwanini tunakopa sana,

Kodi( Taxation) Serikali imetoza kodi mpaka ikaambiwa inabambikia watu kodi

Misaada(Grants) Serikali imepokea na kuwekewa masharti kibao mpaka watu Wakasema ni aibu kuwategemea mabeberu

Mwisho, Serikali imeleta Tozo (Government levy) bado watu Wanalalamika, Tujadili vyanzo vya mapato kulisaidia Taifa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
... Mkuki kwa nguruwe ni mtamu kupitiliza! Kila mmoja na imwingie akilini inapohimizwa wananchi wakajiandikishe na wajitokeze kupiga kura kwa akili inamaanisha nini.

"Hakuna njia mbadala ya mapato kwa sasa"; akili za watu walioshindwa ila wanapenda kuendelea kutawala!

Isipoeleweka ni kwanini Katiba Mpya na Bora ni muhimu tutakuwa na akili za ajabu sana. "Katiba Mpya haileti chakula mezani"; akili za wasio na mbadala kabisa wa kulikwamua taifa yet baadhi ya wajinga watatekwa na hadaa za kipumbavu.
 
Wanabodi kuna vitu ni luxiory na vingine Necessity. Luxiory kwako yaweza kikawa necessity kwa mtu mwingine na hivyo hivyo necessity kwako yaweza ikawa luxiory kwa mtu mwingine...
Hakuna anayekataa tozo ya jengo ila mpangaji haoni sababu ya kulipia jengo ambalo si lake kwani yeye ni mpita njia tu; pia hakuna mwenye jengo ambaye amelalamika kwani anategemea mpangaji atamlipia, ni vizuri uelewe sakata lote kabla ya kukurupuka kuandika.
 
Mtu kutumia bia ni maamuzi yake binafsi, unaweza unywe mimi nisinywe, lakini tozo kwenye mafuta ya kula hiyo inamuumiza kila mmoja, na miamala ya simu watu wanatumia pesa ndugu zao vijijini serikali inachukua karibia robo huu ni wizi, serikali inaongeza umasikini kwa watanzania ambao ulishakuwepo.

Kutuma pesa kwa mitandao ya simu siku hizi sio hiyari, ni lazima; vijijini hakuna matawi ya benki, watu wana mahitaji yao ya msingi ya kununua, kuanzia sukari, mafuta, dawa wakiugua, nk. Kusema kutuma pesa kwa njia ya simu iwe hiari kama mtu akiamua aache maana yake unataka watu wasinunue mahitaji yao ya msingi, au wagonjwa wafe.

Vyanzo vipya vya mapato lazima viangaliwe vile ambavyo havitamuumiza mtanzania wa kawaida, na vinaingiza kiasi kingi kwa wakati mmoja; makampuni ya madini yanaingiza pesa nyingi, machimbo yapo karibia kila mkoa Tanzania, lakini viongozi wa CCM wakishachukua 10% hawana tena habari na masikini.

Halafu wakienda bungeni wanasema tuwaambie vyanzo vipya vya mapato, huu ni utani, rasilimali zote za hili taifa wameshindwa kuzisimamia sasa wanarudi kumkamua mtanzania anayejihangaikia kutafuta kula yake na watoto wake kwenye jua kali, huku wao bungeni posho nyingi na mishahara mikubwa kukaa kwenye AC lakini hawataki wakatwe kodi.
 
Wanabodi kuna vitu ni luxiory na vingine Necessity. Luxiory kwako yaweza kikawa necessity kwa mtu mwingine na hivyo hivyo necessity kwako yaweza ikawa luxiory kwa mtu mwingine...
Hatujawahi kuwa na tozo kwenye bia bali kodi, naona unachanganya kodi na tozo.
 
Mtu kutumia bia ni maamuzi yake binafsi, unaweza unywe mimi nisinywe, lakini tozo kwenye mafuta ya kula hiyo inamuumiza kila mmoja, na miamala ya simu watu wanatumia pesa ndugu zao vijijini serikali inachukua karibia robo huu ni wizi, serikali inaongeza umasikini kwa watanzania ambazo ulishakuwepo.

Kutuma pesa kwa mitandao ya simu siku hizi sio hiyari, ni lazima; vijijini hakuna matawi ya benki, watu wana mahitaji yao ya kununua, kuanzia sukari, mafuta, dawa wakiumwa, nk. Kusema kutuma pesa kwa njia ya simu iwe hiari kama mtu akiamua aache maana yake unataka watu wasinunue mahitaji yao ya msingi.
Kiufupi huu ni unyan'ganyi wa mchana kweupe, na si mpango endelevu
 
Mtu kutumia bia ni maamuzi yake binafsi, unaweza unywe mimi nisinywe, lakini tozo kwenye mafuta ya kula hiyo inamuumiza kila mmoja, na miamala ya simu watu wanatumia pesa ndugu zao vijijini serikali inachukua karibia robo huu ni wizi, serikali inaongeza umasikini kwa watanzania ambao ulishakuwepo...
mmmh sikubaliani na wewe

Mimi situmii mafuta ya kula kabisa nayakwepa sana sana

Hata sukari nakwepa sana sana

Mimi ukisema sukari bei juu nashangaa tu kwangu sio muhimu sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom