Toyota Prado Ipi Bora?

JembeNaNyundo

JF-Expert Member
Dec 9, 2016
532
646
Wakuu heri ya Mwaka Mpya!

Ninaomba ushauri wa kitaalam na uzoefu. Ninataka niagize Toyota Prado - Third generation (toleo la tatu), yaani hizi J120 series zilizotoka kati ya mwaka 2002 hadi 2009.
Ipi ni bora zaidi? Nimeweka baadhi ya matoleo na engine zake hapa chini.

TRJ120W 2,690cc (2TR)
RZJ125W 2,690cc (3RZ)
VZJ125W 3,370cc (5VZ)
VZJ120W 3,370cc (5VZ)
GRJ120W 3,950cc (1GR)
GRJ121W 3,950cc (1GR)

Shukrani

IMG_1681.JPG
 
Prado yako iwe na 1KZ engine petrol au diesel.
Engine isizidi cc3000
Na isiwe v6
Utaenjoy
Nimezitumia zote ila hiyo hapo juu hutajuta.
Epuka gari za diesel ambazo km zake zinazidi 100 000 maana prado iko at its best before km 300 000 kwa diesel.
 
mi nakushauri nunua magari haya yafuatayo..
1. starlet
2. passo
3. Kirikuu kama unataka na kubebea matikiti shambani.
ayi ma prado hayana dili kabisa, gari gani ukitaja hadi damu inasisimuka?
Asante pia kwa ushauri
 
Prado yako iwe na 1KZ engine petrol au diesel.
Engine isizidi cc3000
Na isiwe v6
Utaenjoy
Nimezitumia zote ila hiyo hapo juu hutajuta.
Epuka gari za diesel ambazo km zake zinazidi 100 000 maana prado iko at its best before km 300 000 kwa diesel.
Kama ni best before km 300 000 sioni hatari ya kununua ikiwa km100 000
 
Prado yako iwe na 1KZ engine petrol au diesel.
Engine isizidi cc3000
Na isiwe v6
Utaenjoy
Nimezitumia zote ila hiyo hapo juu hutajuta.
Epuka gari za diesel ambazo km zake zinazidi 100 000 maana prado iko at its best before km 300 000 kwa diesel.

kuna 1kz ya petrol?
engine zote alizotaja apo ni za petrol.

ushauri ni achukue yoyote yenye engine kati ya 2tr akikosa achukue yenye 3rz.

utofauti katika kutumia mafuta ukilinganisha na kz ni mdogo. lkn pia service ya gari ya diesel ni kubwa ukilinganisha na petrol.
 
Prado yako iwe na 1KZ engine petrol au diesel.
Engine isizidi cc3000
Na isiwe v6
Utaenjoy
Nimezitumia zote ila hiyo hapo juu hutajuta.
Epuka gari za diesel ambazo km zake zinazidi 100 000 maana prado iko at its best before km 300 000 kwa diesel.
version hii ya prado hakuna inayotumia engine ya 1KZ, ukikuta ina aina iyo ya engine jua wameshawai kuibadilisha engine, diesel version zake hutumua 1KD au 2KD engines....na GX version zake zinakuja na 5L engine
 
kati ya
TRJ120W 2,690cc (2TR)
RZJ125W 2,690cc (3RZ)

kuna ambayo ni 4 cylinder?

Ndio hicho kitu nasema sidhani kama kinawezekana kuwa na Landcruiser kubwa kama Prado ukakuta lina 4 Cylinder.

Na kama ipo, engine ya 4 Cylinder kuvuta Prado itakuwa haina nguvu, utakuta inalazimika kutumia mafuta yale yale kama 6 cyl.

Kwa nini usi consider Prado ya diesel? Again, kama lengo ni ku save kwenye mafuta.
 
Ndio hicho kitu nasema sidhani kama kinawezekana kuwa na Landcruiser kubwa kama Prado ukakuta lina 4 Cylinder.

Na kama ipo, engine ya 4 Cylinder kuvuta Prado itakuwa haina nguvu, utakuta inalazimika kutumia mafuta yale yale kama 6 cyl.

Kwa nini usi consider Prado ya diesel? Again, kama lengo ni ku save kwenye mafuta.

mkuu usipotoshe watu, 90% ya prado unazoziona mtaani zina 4 cylinders....,engine pekee yenye six cylinder kwaajili ya prado ni VZ series..hasa 5VZ. ....izo TR engine series, RZ series, 1kz, 5l, 3L zote ni 4 cylinder....iwe ya diesel au petrol. ....prado its a light landcruiser, haina nguvu kama mkonga inayotumia 1HZ. ni cruiser kwaajili ya matumizi ya kawaida tu. safari za hapa na pale na sio kwendea porini. na huwa inaingiana sana engine na toyota hilux
 
Sijawahi kupenda prado.....

Ford ni nzuri....ipo vizuri kwa road....ulaji wa mafuta sio kivile....kitu everest
 
Back
Top Bottom