Toyota Fortuner "Mjapan mwenye vinasaba vya Marekani"

Siwezi tumia gari ambayo inashea engine na kina prado na hilux😁😁 ...yani niwe kwenye huo mgari afu mtu wa Hilux anakukazia na humpiti kweli 😁
 
Mkuu hiyo kitu naikubali lakini machine za kimarekani ni hatari sana kuko na hii Chevrolet suburban ni kitu ya hatari nafikiri hawa fortuner waliiba formula hapa
 
Toyota fortuner, pacha yake Ford Endevour... haya magari mawili nikiyaona moyo wangu unasema paaaah... kibongo bongo, tunasema, one day yes
Kutoka hapa nilipo mpaka Ban-pho katikati mwa nchi ya Thailand ni kilometa 7191, Mbali kwelikweli.

Inaitwa Toyota Fortuner mid-size SUV mpango kazi wa kimarekani uliotekelezwa na Wajapan katikati ya viunga vya Ban-pho Thailand.

Akili inantuma kuamini kuwa Wajapani walitumia Mayakuza kuiba mbinu madhubuti za Mmarekani.Ukikutana na majasusi wa CIA huenda wakawa na siri niliyonayo mimi. Wapima vinasaba vya magari wanaweza wakawa na file lenye ukweli wa wapi ni asili ya Fortuner.

Ni bahati kufananishwa na Jeep Renegade, inatokea mara chache sana kufananishwa na Chevrolet Blazer. Awakukosea kuliita Fortuner wakimaanisha kitu chenye bahati.

Tegemea kukutana na Silver accents with wood like finish ukifungua macho yako mbele ya Fortuner. Hamna haja ya kuhubiri uwezo wa Fortuner. Ila andaa lita 80 za mafuta kujaza full tank gari hili.

Mimi bado naliita "The Godfather of the Road" ina nguruma kama simba mzee ikiwa Kwenye rami, ina engine ya diesel madhubuti CC 2982 na turbocharge kama ofa, kwanini iteseke sasa . Haitetemeki wala kuyumba hata ikiwa Kwenye speed ya 130Kmh. Ina sifa za kiasili za Kimarekani.

Kimo cha mjapan wa wastani ni futi 5 tu. Wao na Fortuner wapi na wapi. Maajabu ya Fortuner yanaelezwa mpaka Manhattan Newyork, Sitaki kukusimulia sana, maelezo utapewa pale Lumumba mtaa wenye madalali wakongwe, andaa peni na karatasi tu.

BRAVO! Toyota Fortuner Nabii wa Kijapan Aliyekubarika Dunia nzima. Ila bado najiuliza Fortuner kwenu ni wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kutoka hapa nilipo mpaka Ban-pho katikati mwa nchi ya Thailand ni kilometa 7191, Mbali kwelikweli.

Inaitwa Toyota Fortuner mid-size SUV mpango kazi wa kimarekani uliotekelezwa na Wajapan katikati ya viunga vya Ban-pho Thailand.

Akili inantuma kuamini kuwa Wajapani walitumia Mayakuza kuiba mbinu madhubuti za Mmarekani.Ukikutana na majasusi wa CIA huenda wakawa na siri niliyonayo mimi. Wapima vinasaba vya magari wanaweza wakawa na file lenye ukweli wa wapi ni asili ya Fortuner.

Ni bahati kufananishwa na Jeep Renegade, inatokea mara chache sana kufananishwa na Chevrolet Blazer. Awakukosea kuliita Fortuner wakimaanisha kitu chenye bahati.

Tegemea kukutana na Silver accents with wood like finish ukifungua macho yako mbele ya Fortuner. Hamna haja ya kuhubiri uwezo wa Fortuner. Ila andaa lita 80 za mafuta kujaza full tank gari hili.

Mimi bado naliita "The Godfather of the Road" ina nguruma kama simba mzee ikiwa Kwenye rami, ina engine ya diesel madhubuti CC 2982 na turbocharge kama ofa, kwanini iteseke sasa . Haitetemeki wala kuyumba hata ikiwa Kwenye speed ya 130Kmh. Ina sifa za kiasili za Kimarekani.

Kimo cha mjapan wa wastani ni futi 5 tu. Wao na Fortuner wapi na wapi. Maajabu ya Fortuner yanaelezwa mpaka Manhattan Newyork, Sitaki kukusimulia sana, maelezo utapewa pale Lumumba mtaa wenye madalali wakongwe, andaa peni na karatasi tu.

BRAVO! Toyota Fortuner Nabii wa Kijapan Aliyekubarika Dunia nzima. Ila bado najiuliza Fortuner kwenu ni wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app

Uchafu mtu ahakuna gari ya kishamba kama hiyo, bora hata prado japo nazenyewe huwa sizielewi.
 
Hiyo Fortuner sio gari tough ya off-road hiyo bado ipo kwenye luxury na wenzake wakina Prado na Surf.
 
Uwe unaweka na vipicha mkuu!
Haya ndo magari ya kuumeni.
Linaitwa toyota tacoma. Ukubwa wake, Linaizidi kwa mbali sana hilux ni off road lenye heshima zake!
Discovery 4 naipenda sana kwa mwonekano. Imekaa kiume zaidi.
images.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom