Tovuti ya Serikali ya 'Wananchi' hivi inafanya kazi kweli?

The Palm Tree

JF-Expert Member
Apr 13, 2013
7,951
12,535
Screenshot 2021-05-19 at 11.14.48.png

Hii tovuti wananchi.go.tz inaendeshwa na iko chini ya Wizara ya habari, utamaduni na michezo.

Lengo lake kubwa ni kwa kila mwananchi mwenye kero, malalamiko, maoni, ushauri, kutoa ripoti za uhalifu, rushwa nk kuandika kero au taarifa yake kwa maandishi na wao wizara wanaipokea na kisha kuipeleka kwa mtu anayelalamikiwa au mamlaka (taasisi au idara ama ofisi ya umma) inayohusika ili waitolee ufafanuzi/majibu/ufumbuzi.

Binafsi, nilishatoa kero na malalamiko na kero nyingi sana kupitia njia hii. Nyingi sijawahi kujibiwa na nakumbuka kuna kero moja ya kiutumishi, ni mwaka wa saba sasa haijawahi kujibiwa. Huwa kila nikifungua kufuatilia jibu langu huwa nashangaa kwani mara zote nakutana na maelezo mafupi tu 'Kero yako Inashughulikiwa'.

Tumekuwa tunasisitizwa tuache kulalamika tu na kuishambulia serikali na badala yake tutumie njia sahihi kuwasilisha kero au malalamiko au ushauri wowote ili ufanyiwe kazi kwa utaratibu unaotakiwa wa Kiserikali.

Sasa mtu afanyeje iwapo anapeleka malalamiko au kero au maoni yake na wahusika badala ya kufanyia kazi na kutoa majibu wake badala yake wao wanakaa tu na kuifungia kero au lalamiko ya wananchi ndani ya kabati zao...?

Huku ni kushindwa kuwajibika kwa taasisi, serikali au idara za serikali. Tafadhali, toeni majibu kwa watu ndani ya muda uliopangwa (ndani ya siku tano za kazi kama mlivyoandika wenyewe) kuanzia siku hoja au kero au lalamiko limepokelewa...

Kinyume chake, serikali itaendelea kulalamikiwa na kutukanwa kwa vitu vidogo vidogo tu vinavyosababishwa na watendaji wachache wazembe na wasio waaminifu toka taasisi, idara na ofisi zote za umma.
 
Tanzania hakuna taasisi inayoweza kuendesha website..sio ya uma wala binafsi. watu wengi hudhani ukisha launch website kazi inakua imeisha, wakati ndio kazi imeanza
 
Tanzania hakuna taasisi inayoweza kuendesha website..sio ya uma wala binafsi. watu wengi hudhani ukisha launch website kazi inakua imeisha, wakati ndio kazi imeanza
Isipokuwa BRELA, Ajira portal ma Tamisemi
 
Tanzania hakuna taasisi inayoweza kuendesha website..sio ya uma wala binafsi. watu wengi hudhani ukisha launch website kazi inakua imeisha, wakati ndio kazi imeanza
Huwa zinawekwa geresha tu hizo, nyingine hata hawazilipii kwenye database , yaan uki query some infos au ku upload comment zako unaambiwa server not found......juz Kati Kuna tangazo niliskia kwenye magar ya matangazo , ili kupata taarifa Zaid nikasearch tovuti na kukutana na contacts za ofisi husika , Cha ajabu aliepokea hahusiani na office Ila ni mkazi wa eneo lile na anashughuli flan halali na alinikaribisha , Sasa kilichonishangaza namba yake unafanya Nini kwenye sites za halmashauri na wameelekeza kabsa "kwa maelezo Zaid wasiliana nasi kupitia...."
 
Hii tovuti wananchi.go.tz, inaendeshwa na iko chini ya Wizara ya habari, utamaduni na michezo..

Lengo lake kubwa ni kwa kila mwananchi mwenye kero, malalamiko, maoni, ushauri, kutoa ripoti za uhalifu, rushwa nk kuandika kero au taarifa yake kwa maandishi na wao wizara wanaipokea na kisha kuipeleka kwa mtu anayelalamikiwa au mamlaka (taasisi au idara ama ofisi ya umma) inayohusika ili waitolee ufafanuzi/majibu/ufumbuzi...

Binafsi, nilishatoa kero na malalamiko na kero nyingi sana kupitia njia hii. Nyingi sijawahi kujibiwa na nakumbuka kuna kero moja ya kiutumishi, ni mwaka wa saba sasa haijawahi kujibiwa...!!

Huwa kila nikifungua kufuatilia jibu langu huwa nashangaa kwani mara zote nakutana na maelezo mafupi tu "kero yako inashughulikiwa....!!"

Tumekuwa tunasisitizwa tuache kulalamika tu na kuishambulia serikali na badala yake tutumie njia sahihi kuwasilisha kero au malalamiko au ushauri wowote ili ufanyiwe kazi kwa utaratibu unaotakiwa wa kiserikali...

Sasa mtu afanyeje iwapo anapeleka malalamiko au kero au Maoni yake na wahusika badala ya kufanyia kazi na kutoa majibu badala wao wanakaa na kuifungia kero au lalamiko ndani ya kabati...!

Huku ni kushindwa kuwajibika kwa taasisi, serikali au idara za serikali. Tafadhali, toeni majibu kwa watu ndani ya muda uliopangwa (ndani ya siku tano za kazi) kuanzia siku hoja au kero au lalamiko limepokelewa...

Kinyume chake, serikali itaendelea kulalamikiwa na kutukanwa kwa vitu vidogo vidogo tu vinavyosababishwa na watendaji wachache wazembe na wasio waaminifu toka taasisi, idara na ofisi zote za umma...
1621411064508.png
 
Kibongo bongo commitment na accountability vipo chini sana aisee ndio maana taasisi zetu kufeli ni ndani ya sekunde tu hapo.
 
Isipokuwa BRELA, Ajira portal ma Tamisemi
tamisemi ndo hata usizungumze, huwa wanaupdate zile content zinazotakiwa kwa wakati huo..kama matokeo nk..
jaribu kupitia baadhi ya page zake utaona maajabu..
nina uhakika utakuta waziri jafo akiwa waziri akikagua miradi.. na
 
tamisemi ndo hata usizungumze, huwa wanaupdate zile content zinazotakiwa kwa wakati huo..kama matokeo nk..
jaribu kupitia baadhi ya page zake utaona maajabu..
nina uhakika utakuta waziri jafo akiwa waziri akikagua miradi.. na
Watumishi portal Leo mwaka wa tatu kila ukijaribu majibu... Tupo kwenye matengenezo... Ni upuuzi na udanganyifu kwa umma !
 

Hii tovuti wananchi.go.tz inaendeshwa na iko chini ya Wizara ya habari, utamaduni na michezo.

Lengo lake kubwa ni kwa kila mwananchi mwenye kero, malalamiko, maoni, ushauri, kutoa ripoti za uhalifu, rushwa nk kuandika kero au taarifa yake kwa maandishi na wao wizara wanaipokea na kisha kuipeleka kwa mtu anayelalamikiwa au mamlaka (taasisi au idara ama ofisi ya umma) inayohusika ili waitolee ufafanuzi/majibu/ufumbuzi.

Binafsi, nilishatoa kero na malalamiko na kero nyingi sana kupitia njia hii. Nyingi sijawahi kujibiwa na nakumbuka kuna kero moja ya kiutumishi, ni mwaka wa saba sasa haijawahi kujibiwa. Huwa kila nikifungua kufuatilia jibu langu huwa nashangaa kwani mara zote nakutana na maelezo mafupi tu 'Kero yako Inashughulikiwa'.

Tumekuwa tunasisitizwa tuache kulalamika tu na kuishambulia serikali na badala yake tutumie njia sahihi kuwasilisha kero au malalamiko au ushauri wowote ili ufanyiwe kazi kwa utaratibu unaotakiwa wa Kiserikali.

Sasa mtu afanyeje iwapo anapeleka malalamiko au kero au maoni yake na wahusika badala ya kufanyia kazi na kutoa majibu badala wao wanakaa na kuifungia kero au lalamiko ndani ya kabati.

Huku ni kushindwa kuwajibika kwa taasisi, serikali au idara za serikali. Tafadhali, toeni majibu kwa watu ndani ya muda uliopangwa (ndani ya siku tano za kazi) kuanzia siku hoja au kero au lalamiko limepokelewa.

Kinyume chake, serikali itaendelea kulalamikiwa na kutukanwa kwa vitu vidogo vidogo tu vinavyosababishwa na watendaji wachache wazembe na wasio waaminifu toka taasisi, idara na ofisi zote za umma.
Utakuta mwendeshaji wa hiyo website ni mzee mwenye miaka 49.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom