Tour fupi ya shamba langu la greenhouse

Huyu jamaa Biashara2000 yuko vizuri, ukiwa na nia ya kulima, mtumie pls. Mie nililipia PDF za Kilimo kwake lakini sikulima. Nikaja kuanza kulima mwaka huu mwezi wa saba, sikuvuna chochote maana Shamba langu lilikuwa na waangalizi wengine wakati Mimi nahangaika na kibarua kingine. Mwezi wa tisa mwishoni nilimpigia Biashara2000 anipe mwongozo wa kulima pilipili hoho, na nililima kwa kufuata mwongozo wake. Nilisimamia Shamba kwa wiki Mbili tu na hoho zikawa fresh kabisa, na nikawaacha vijana wangu waendelee na utunzaji wa shamba. Kwa sasa niko mbali na eneo la Shamba yapata wiki 3, lakini mambo yanaendelea vzr. Jumapili naanza kuuza hoho . kwa hiyo huyu Biashara2000 habahatishi mambo, kilimo anakifahamu vyema saana
 
Habari mkuu,


Naomba tuwasiliane kuhusu hiki kilimo, ningependa nilime mwakani kigamboni, inaweza gharimu kiasi gani? Namba yangu ni 0786 333334
 
Huyu jamaa Biashara2000 yuko vizuri, ukiwa na nia ya kulima, mtumie pls. Mie nililipia PDF za Kilimo kwake lakini sikulima. Nikaja kuanza kulima mwaka huu mwezi wa saba, sikuvuna chochote maana Shamba langu lilikuwa na waangalizi wengine wakati Mimi nahangaika na kibarua kingine. Mwezi wa tisa mwishoni nilimpigia Biashara2000 anipe mwongozo wa kulima pilipili hoho, na nililima kwa kufuata mwongozo wake. Nilisimamia Shamba kwa wiki Mbili tu na hoho zikawa fresh kabisa, na nikawaacha vijana wangu waendelee na utunzaji wa shamba. Kwa sasa niko mbali na eneo la Shamba yapata wiki 3, lakini mambo yanaendelea vzr. Jumapili naanza kuuza hoho . kwa hiyo huyu Biashara2000 habahatishi mambo, kilimo anakifahamu vyema saana
Mkuu hizo PDF ulilipia kiasi gani?na Mimi nazihitaji, naona @ biashara2000 hajaona ujumbe wangu na wala hajasema chochote
 
Mkuu hizo PDF ulilipia kiasi gani?na Mimi nazihitaji, naona @ biashara2000 hajaona ujumbe wangu na wala hajasema chochote
Niliwasiliana nae juzi kwa ajili ya kutembelea na akaniambia hizo PDF unalipia 15k halafu siku unaenda shamba unalipia 15k ingine. Hiyo ndio mchanganuo wa ile gharama ya kutembelea shamba darasa.
 
Niliwasiliana nae juzi kwa ajili ya kutembelea na akaniambia hizo PDF unalipia 15k halafu siku unaenda shamba unalipia 15k ingine. Hiyo ndio mchanganuo wa ile gharama ya kutembelea shamba darasa.
Vaita, unaweza kuniambia mliwasiliana vipi? Bado namtafuta huyo jamaa
 
Ndugu C.Misonge huyu bwana nilimpigia simu, kwenye namba yake ambayo imo katika post yake ya kwanza kabisa.
 
Siku ya Jana nilikuwa naongea na wakulima mbalimbali wanaolima karibu na shamba langu. Tukawa tunaongea kuhusu uzoefu wetu katika kipindi kabla hatujaanza kulima. Wengi wao walikuwa wanasema wangejua wangeanza kilimo mapema kwani wakifikiria muda walioupoteza walipokuwa wakisita kuanza wanafikiria wangekuwa wamefika mbali kimaendrleo. Wanasema uoga wa kujaribu mambo mapya waliuruhusu kuwazuia. Wanasema sisi ni waoga wa kujihuaisha na biashara na kilimo.

Mimi nadhani hiyo ni kweli kabisa. Siai tunaogopa kuchukua fursa ya kilimo bila kuangalia potential ya Soko liko wazi kwa ajili ya mazao ya mboga mboga. Ingawa Soko lina changamoto zake lkn huwezi koaa faida km utafuata formula yake. Tusiogope. Tuamue kujaribu mapya. Huu muda ambao unajiuliza uliza na kuvuta muda, km ungeamua kuanza ungekuwa uahafika mbali kifedha
 
Kuna watu wanauliza kwa Yale maeneo amnayo yana asili ya kushambuliwa na wadudu na kuwa na magonjwa mengi, wanauliza waifanyaje ardhi yao ili waweze kulima? Nimeamua kujibia hapa ili ifaidishe na wengine

Nunua dawa inaitwa Farmguard weka kwenye dumu la Maji pulizia ktk eneo laki kabla hujapanda chochote. Baadae ukishapanda na Miche ishakua, changanya dawa inaitwa Blast na nyingine Ebony kisha pulizia kwenye Miche yako kwa ajili ya wadudu
 
za kwenu wana jamvi. Nimedhani itakuwa inahamasisha kama nami nta share experience yangu katika kilimo baada ya kuamua kwa hiari mwenyewe kujihusisha na kilimo ili kujiongezea kipato. Nilmtumia Biashara hiyopesa ya hiyo formula yake na pia nikaenda kwenye lile shamba darasa alilonielekeza pale kibamba nikajifunza kwa vitendo.
Nilianza kulima katika eneo langu dogo eneo la uani na nikaweka miche km 150 hivi. pia kwa kuwa nilikuwa nimeajiriwa ofisini nikamkabidhi kila kitu mfanyakazi wangu na kumpa ile elimu. Nilikuwa nalima nyanya. Uzuri alikuwa mwaminifu na alilitunza vizuri. Nikaa na focus ktk kazi yangu ya ofisi na yeye akawa analiendesha shamba vizuri. Kwa mtindo huu hakukuwa na matatizo mengi. Ilikuwa kilimo rahisi. Nilichogundua cha muhimu kuzingatia ni mbegu inayozaa mazao mengi na kufuata ushauri wake wa dawa na kukinga dhidi ya maradhi.

So kwa kumalizia niseme tu kilimo kinaweza fanywa kwa urahisi tu iwapo ushauri unafuatwa.
 
Kuna watu wanauliza kwa Yale maeneo amnayo yana asili ya kushambuliwa na wadudu na kuwa na magonjwa mengi, wanauliza waifanyaje ardhi yao ili waweze kulima? Nimeamua kujibia hapa ili ifaidishe na wengine

Nunua dawa inaitwa Farmguard weka kwenye dumu la Maji pulizia ktk eneo laki kabla hujapanda chochote. Baadae ukishapanda na Miche ishakua, changanya dawa inaitwa Blast na nyingine Ebony kisha pulizia kwenye Miche yako kwa ajili ya wadudu
Ndugu huu ushauri hapana ni vyema kwanza kujua ni wadudu gani wako sababu kila eneo na wadudu wake wanaoshambulia ,blast inaua wadudu gani!? Ebony ni ya ukingu ingawa sijajua ni 80 au 72 unayoongelea but kuitumia pia inategemea na msimu wa mvua au jua na stage ya ukuaji wa mmea na kujua kama unataka kukinga au kutibu,kutoa jibu la moja kwa moja hivi haliko applicable kote ,ahsante sana
 
Miradi iko mingi na inatoa elimu ya kilimo bure na kwa vitendo ,ukisha kua na documents za kilimo usiishie hapo ongeza ujuzi kwa kujifunza zaidi zao unalotaka kulilima utajua abc vyema zaidi sababu changamoto za shambani haziko sawa nchi nzima ,ahsanteni sana
 
Bw. Biashara naomba niongelee kidogo Leo kuhusu jambo dogo ingawa lina mchango mkubwa sana katika kuleta maendeleo ya watz katika kila nyanja ya maisha.

Juzi kati baada ya kuchangia katika post yako kuna kijana aliniandikia meseji alikuwa anaongelea na kuniuliza maswali kadhaa. Nilimuuliza kuhusu yeye na akaniambia kuwa yeye amekuwa akijifunza kilimo kwa miaka 4 sasa akitumia sh 7000 kwa wiki kuingia internet cafe (364,000) kwa mwaka lakini hajalima hata mche kwa muda huo wote. Aliniambia sababu iliyomfanya asiweze kulima hata Miche kadhaa ni kukosa mentor yaani msimamizi wa karibu. Hapo ndio nikapata somo ambalo nataka niongelee kwa kifupi sana.

Watz wengi hawawezi kufanya kitu chochote kile bila kuwa na msimamizi wa kuwasimamia na kuwashauri kwa ukaribu. Yaani mentor. Na hii ndio inafanya wengi wanajifunza huko mtandaoni lakini hawalimi. Hivyo ningependa nikushukuru kwa kubipa mentoring yako lakini niku challenge uongeze wigo huo kwa wengi zaidi. Ningeshauri pia wengine waliofanikiwa katika sekta mbali mbali wapende kusaidia
wanaojikongoja na waPlioko nyuma kimaendeleo. Tusiache mwaka huu wachache waumalize wakiwa wamefaidika na wengi wakishindwa kuanza kilimo na kumaliza mwaka mifukoni kweupe.

Watu wengi ndani yao wana hasira ya ndani kwa ndani kutokana na ugumu wa maisha na stress. Hivyo ni jukumu la kila MTU kuaaidiana na kila MTU kuamua i na umasikini katika sekta yoyote ile ya kimaisha
 
Nawatakia sikukuu njema. Kwa wale waliofanikiwa kuanza kilimo mwaka juu hongereni. Kwa walewalioshindwa bado hamjachelewa
 
Naomba kujua gharama za vifaa na ujenzi wa greenhouse. Hata kama ni fundi mzoefu anaweza kunipa taarifa kwasababu kwenye makampuni kama balton ni ghali sana.
 
Njia rahisi ni kununua chuma zitakazotosha ukubwa wa green house then tafuta fundi afanye kucopy au kama alishatengeneza ila usikubali akupe bei ya skeleton ya green house unless kama unamwamini sana.
Nylon sheet zinauzwa TShs 3000 kwa square meter au chini ya hapo
Insect net au shade net 5.5*30 m ni TShs 275,000 au chili ya hapo
Utanunua profile za kushonea nylon sheet pamoja na net yako moja ina mita 3 kwa TShs 12000
Fundi mtakubaliana kwa siku uwalipe au anaweza kukupa bei ya kazi yote
Utanunua cement mchanga na kokoto.
 
Back
Top Bottom