Total yatoa fursa vituo vya COCO na CODO kuzigeuza DODO! Kuwa umiliki kituo cha mafuta cha total

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,467
113,574
Wanabodi,

Japo hili ni Jukwaa la Siasa, na hii ni story ya fursa za Kiuchumi, issues zozote za utilities, umeme, maji na mafuta, ni siasa, hivyo ikitokea sintofahamu yoyote kwenye issues za mafuta ya fuel, nchi inatikisika!.

Kumetokea Tangazo fulani la Total kwenye gazeti, kuna jamaa ka panic, anataka kuwapanikisha Watanzania!.
What happened? Total yafungasha virago vyake Tanzania(?)

Kabla sijakisema nilicho dhamiria, naomba kwanza nitoe elimu kidogo kuhusu biashara ya mafuta na gesi Tanzanian.

Biashara ya mafuta na gesi Tanzanian imegawanyika katika makundi mawili,
1. Upstream- Watafutaji mafuta na gesi, wachimbaji mafuta na gesi, hawa wanadhinitiwa na PURA.
2. Downstream- hawa ni wasambazaji wa mafuta na gesi, yaani makampuni ya mafuta. Hawa wanadhibitiwa na EWURA.

Kwenye usambazaji wa mafuta, nako kuna makundi mawili,

Waagizaji wa mafuta ya jumla, bulk procurement na wasambazaji wa mafuta ambao wanachukua kutoka kwa bulk na kuuza kwenye vituo vya mafuta.

Ni makampuni machache ambayo wanafanya biashara ya mafuta kuanzia upstream, downstream na retail supply, kwa Tanzania kampuni ya kwanza ilikuwa Shell, ya Waingereza, pili Agip ya Wataliano na tatu ilikuwa Total ya Wafaransa.

Shell iliuzwa sasa ndio Puma, Agip ikauzwa na kuwa Gapco, hivyo kwa sasa, baada ya Total kuinunua Gapco, Tanzania, kampuni kubwa ya mafuta, kwa upande wa mtandao wa vituo vya mafuta, ni Total.

Kwa msio jua, Total ndio kampuni inayoongoza kwa uwekezaji Tanzania, yaani investment, mradi wa bomba la gesi la Hoima Uganda hadi Chongoleani ndio the biggest investment in the history of TIC, hata Dangote atasubiri!.

Tukija kwenye biashara ya reja reja ya mafuta, Total ndio inayoongoza kwa wingi wa vituo vingi.

Sasa naomba kuendesha shule fupi ya maneno matatu haya, COCO, CODO na DODO kuhusu vituo vya mafuta vya Total.

Kuna aina tatu ya vituo vya mafuta vya Total.
COCO ni Company Owned, Company Operated, hivi ni vituo vinavyomilikiwa na kampuni ya Total, 100% kwa 100% na kampuni ya Total inaviendesha, vikiwemo vituo vyake vyenyewe na vituo vyote vilivyokuwa Gapco.

CODO ni Company Owned, Dealer Operated, ni vituo ambayo Total inavimiliki lakini vinaendeshwa na watu wengine, dealers.

DODO ni Dealer Owned, Dealer Operated, hii ni mtu au kampuni binafsi inamiliki kituo na kukiendesha, ila Total wanakupa mkataba wa franchise, kwa kukijenga kwa viwango vya Total na kuuza bidhaa za Total.

Sasa Total Tanzania imemwaga fursa kibao kwa Watanzania kumiliki vituo kwa huo mtindo wa DODO ambapo Total inauza vituo vyake vyote vya COCO na CODO kuwa DODO!.

Changamkia Fursa.

Naomba kuchukua fursa hii kuwaonyesha uzinduzi wa kituo cha mafuta cha Dodo uliofanyika jana pale Goba Mshigeni.


Kwa faida ya wasiojua mambo ya Total karibuni mitaa hii
Kampuni ya Total Yainunua Gapco na Kuwa The Biggest Oil Company in Tanzania, Kenya & Uganda.

Maendeleo ya Kweli Yataletwa na Watanzania: Kampuni ya Mafuta ya Total Yazindua Kituo cha Kwanza cha Watanzania, Total Tegeta Service Station

Jee Kuna Ukweli Kuwa in Tanzania, Mafuta ya Vituo vya Total, " They are The Best?. If Yes, How Wakati Tunanunua Bulk?.

Leo ni Valentine: Jaza mafuta kituo cha Total, upate Zawadi ya punguzo la bei ya mafuta.

From Hyatt Regency, The Kilimanjaro: the 2nd Tanzania Oil & Gas Congress. Wazungu Wengi Kuliko Wenyeji!

Total Tanzania yazindua shindano la 'startupper of the year by total'

Total Tanzania Yafanya Makubwa, Kuigeuza Tanzania Kama Ulaya!, Yaanzia Temeke.

Vita dhidi maambukizi ya corona Tanzania, kampuni ya Total Tanzania mfano wa kuigwa!. Ukifika lazima unawe, upimwe na mashine ndipo uruhusiwe kuingia!

Paskali
Update
Ufafanuzi kutoka Total
Total-Tanzania.jpg

COUNTRIES DOWNSTREAM EASTERN AFRICATOP NEWS
CORRECTION: Total Commits to Keeping its Investments in Tanzania
OilNews September 2, 2020
FacebookTwitterShare
Total Tanzania has refuted claims that its current sales of stations, plots and depots was an indication of it exiting the East African country as alluded by the Africa Energy Chamber yesterday. According to the company the disposal of assets emanate from excess and duplicating infrastructure arising from the acquisition of GAPCO Tanzania Limited assets in 2018 for more than $200 million.

According to the company the joining of the two competitors in the past three years has left the oil marketer with redundant stations and depots some in close proximity. Infrastructure upgrades have also left some of its assets inaccessible and hence a need to dispose these assets.

“Indeed, the September 1 inauguration on the 8th Dodo station forming part of its over 90 stations in Tanzania demonstrates that Total Tanzania has a long term view and is committed to pursuing its development in the country,” Total Tanzania Director of Legal and Corporate affairs Marsha Msuya told OilNews Africa.

Late yesterday the President of the Africa Energy Chamber NJ Ayuk and the Executive President African Energy Chamber CEMAC Zone Leoncio Amada lashed ohut at the Tanzania government for creating a hostile environment for investors.

In its first edition, OilNews Africa had announced that Total Tanzania was exiting the country. After contacting the company, we have learnt that these affirmations are unfounded.

“We apologize to our readers, Total Tanzania and Tanzanian’s in general for our earlier article “Total Seeks Tanzania Downstream Business Exit After 50 years?” . OilNews Africa is committed to carrying factual articles and we expect “generally accepted credible news sources” to play their part in ensuring there is no misinformation originating from them ,” Kamau Mbote – OilNews Africa editor.
OilNewsAfrica has since unpublished an earlier article quoting the Africa Energy Chamber.
 
Idea ya kuuza hizo kampuni ndogo ndogo ni nzuri kwa sababu itasaidia kuongeza mzunguko wa pesa kwa jamii, sijui kama bei ya hizo kampuni itakuwa nzuri kwa watanzania ili wengi waweze kujitokeza kuzinunua.

Lakini pia serikali kujiingiza kwenye biashara ya mafuta nayo inaweza kupunguza idadi ya wataojitokeza kununua hizo kampuni kwa kuhofia ushindani na serikali kwenye biashara ya mafuta.
 
Idea ya kuuza hizo kampuni ndogo ndogo ni nzuri kwa sababu itasaidia kuongeza mzunguko wa pesa kwa jamii, sijui kama bei ya hizo kampuni itakuwa nzuri kwa watanzania ili wengi waweze kujitokeza kuzinunua.

Lakini pia serikali kujiingiza kwenye biashara ya mafuta nayo inaweza kupunguza idadi ya wataojitokeza kununua hizo kampuni kwa kuhofia ushindani na serikali kwenye biashara ya mafuta.
Tatizo Gov ushindani haitaweza itaanza kuwatia mitama ya uhujumu uchumi watu😁 ili ibakie peke yake sokoni.
 
Asante kwa taarifa,kuna changamoto ya utaratibu wao ambayo upo umewapata kipaumbele wenyewe mitaji mikubwa na ya kati kwa maana wafanyabishara wakubwa na wa kati,Je katika hili unaona nafsi hiyo ya kibiashara imekuja kumsaidia mfanyabiashara mdogo anayeelekea kuwa wa kati?
 
Asante kwa taarifa,kuna changamoto ya utaratibu wao ambayo upo umewapata kipaumbele wenyewe mitaji mikubwa na ya kati kwa maana wafanyabishara wakubwa na wa kati,Je katika hili unaona nafsi hiyo ya kibiashara imekuja kumsaidia mfanyabiashara mdogo anayeelekea kuwa wa kati?
Mwana minze, najua huwezi kusema baya lolote kwa kuwa hao jamaa wameshakualika mara kadhaa kwenye uzinduzi wa vituo vyao huko nyuma ukiwa kama MC.
No sijawahi kuwa MC event yoyote ya Total
P
 
Back
Top Bottom