Toleo Jipya: Uongozi wetu na Hatma ya Tanzania

Ni kitabu kizuri................ila mbona muda wa kukitoa ni questionable?
Hasa karibu na uchaguzi- ukizingatia hicho hua ndio msingi wa campain
za CHADEMA?

Just an observation! :drum:
 
Ni kitabu kizuri................ila mbona muda wa kukitoa ni questionable?
Hasa karibu na uchaguzi- ukizingatia hicho hua ndio msingi wa campain
za CHADEMA?

Just an observation! :drum:

kwanini iwe ni Chadema na siyo CCJ ambao ndio wako tayari kusimamia itikadi za mwalimu?
 
Ni kitabu kizuri................ila mbona muda wa kukitoa ni questionable?
Hasa karibu na uchaguzi- ukizingatia hicho hua ndio msingi wa campain
za CHADEMA?

Just an observation! :drum:

ha ha ha! wewe Mwanakijiji sio CHADEMA ni CCJ.Unahofu na CHADEMA,wanakuja kuwashika kwa sana tu.
 

“Mzee Mwanakijiji” umekiondolea udhu Kitabu cha Nyerere…

Jamani,
Nimesoma hicho kinachoitwa “toleo la Kizazi kipya” la Kitabu cha Nyerere cha “Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania”. Kwanza sijui nani amekupa ruhusa ya kukichapisha upya na kuweka “maoni” yako, ya hovyo! Ungefanya la busara kwa kuchapisha upya, bila ya kuchanganya na maoni yako, ili wasiokuwa na Kitabu hicho wakisome! Kwanza ni kinyume cha taratibu za uchapishaji, pili wewe huna hadhi ya kuweza kumchambua Mwalimu kwa suala alilokuwa analizungumzia, kwani wewe mawazo yako yanaanzia na kuishia kwenye “Richmond” na “Meremeta” tu, huna upana wa uchambuzi wa mambo ya Uongozi wa Nchi! Ungekuwa una uwezo huo usingeikimbia njaa ya Tanzania na kwenda kuishi kwa kubangaiza ughaibuni! Taasisi ya Mwalimu Nyerere lazima ikuchukulie hatua kwa kukiondolea tohara Kitabu hicho. Umeweka maoni yako mengi, lakini hukuweka maoni kuhusu Mwalimu Nyerere alimposema waziwazi, kwa jina, Samuel Sitta, Spika wetu wa sasa (Uk. 36 wa chapisho lako, lakini Uk. wa 26 wa Kitabu ‘orijino’ cha Mwalimu, aya inayohusu ‘Usugu wa Viongozi’), wakati huo akiwa Waziri wa Sheria alipojaribu kuliyumbisha Bunge na Chama kuipigania hoja ya Serikali ya Tanganyika iliyokuwa na nia ya kutaka kuuvunja Muungano, iliyomfanya Nyerere ahamaki na kutunga Kitabu hicho! Haishangazi sasa Mhe. Sitta huyu, akiwa Spika, analivuruga Bunge, mpaka Serikali ya Awamu ya Nne inashindwa kutekeleza vizuri Ilani yake ya Uchaguzi! Yeye na wenzake wanaivuruga CCM, mpaka imeundwa Kamati ya Mzee Mwinyi. Haishangazi sasa kwa nini CCJ imeundwa, ikiwa imebana chonjo! Mpendazoe alikwishasema anamsubiri Mhe. Sitta!
Bwassa

Bwassa labda wewe unalo toleo feki kwa sababu kwenye toleo orijino 'Usugu wa Viongozi' uko ukurasa wa 27 na sio 26. Pia bila shaka maneno yaliyomo kwenye toleo lako feki yako tofauti na yale yaliyo kwenye toleo orijino kwa sababu hakuna popote ambapo Mwalimu anamshambulia Sitta. Toleo orijino linasema:
"Jukumu la kueleza Taarifa hii ya Serikali katika Halmashauri Kuu ya Taifa aliachiwa Waziri wa Sheria na mambo ya Katiba, Mheshimiwa Samuel Sitta. Baadaye, baada ya kikao, nilimtafuta Ndugu Sitta, nikampa pole kwa kupewa jukumu la kueleza jambo ambalo halielezeki. Mapema nilikuwa nimeambiwa kwamba alikuwa ametamka Bungeni kwamba hapo hoja ya kudai Serikali Tatu itakapoanza kujadiliwa, yeye ataipinga, maana jimbo lake la uchaguzi, Urambo, halikuwa limemtuma kwenda Bungeni kudai Serikali ya Tanganyika. Wabunge wote wakweli wangeweza kusema hivho hivyo. hata Waziri Mkuu na Katibu Mkuu wangeweza kusema hivyo hivyo. Wao ni wateuliwa na Rais, ambaye alikwisha kwenda Bungeni siku chache tu zilizopita, na kupinga hoja ya Serikali tatu........"
Bwassa kama utasoma kwa makini utaelewa kwamba Sitta alikuwa na msimamo aliokuwanao Mwalimu wa kupinga madai ya kuwepo kwa Serikali tatu/kufufuliwa kwa serikali ya Tanganyika.

Tatizo tulilonalo Watanzania ni kuendekeza ushabiki usio na tija na kujaribu kupotosha ukweli kwa makusudi na wakati mwingine upotoshaji huo unaweza kuwa na madhara makubwa kwa mustakabali wa Taifa letu,
 
Jamani tunauana bila sababu, lazima tuwe pamoja kuweza kujenga nchi yetu. MMKJ ameona yeye mchango wake ni huo na kaufanya sisi tunapiga domo tu hapa, nina uhakika MMKJ ni msomi mzuri anajua pragriarism vizuri kuliko hata sisi wengine hapa hivyo hakuna sababu ya kumtukana na kumuuliza yeye ametoa maoni kwenye kitabu cha mwalimu kama nani. Tusipende kuhodhi hata vitu ambavyo ni kwa ajiri ya maendeleo yetu wenyewe.

Kwa ujumla kama Mwalimu angekuwa anarudi leo hata nguvu ya kutunga kitabu kama hicho asingeipata na angekufa ndani ya dakika moja baada ya kurudi
Nakubaliana nawe.

Kwa mawazo yangu finyu naamini kabisa kwamba Mwalimu angelikuwa hai angefurahi sana kuona kwamba wapo Watanzania wanaoweza kusoma maandiko yake na kuyachambua. Halikadhalika angefurahi kuona anao waumini wa dhati wanaoelewa alichokuwa akikifanya kwa ajili ya mustakabali mwema wa Taifa letu.
 
Jamani tunauana bila sababu, lazima tuwe pamoja kuweza kujenga nchi yetu. MMKJ ameona yeye mchango wake ni huo na kaufanya sisi tunapiga domo tu hapa, nina uhakika MMKJ ni msomi mzuri anajua pragriarism vizuri kuliko hata sisi wengine hapa hivyo ...

Jiongelee wewe.

Hakuna anaejua usomi wa mtu hapa, na kama Mwanakijiji amekwambia wewe kwamba kasoma kutupita mkaribishe chai mkanywe, lakini usituongelee na sisi.

Huyu mwandishi amechukua na kubadilisha maandishi ya mtu kinyume na misingi ya usambazaji vitabu, mawazo na maneno ya mtu mwingine, na akaweka alama za jina lake, ameiba.

Ukisoma "toleo la pili" huwezi jua mstari wa Nyerere unaishia wapi na chombezo za M.M.M. zinaanzia wapi maana amepanga aya upya na kufanya uhariri wake kuchanganya msomaji.

Anasema kwenye utangulizi kwamba amefanya hivyo kurahisisha maandishi ya Nyerere yaeleweke, lakini kwenye utangulizi kasema:
… kukiri kuwa Mwalimu Nyerere alikuwa na uwezo mkubwa wa kufanya mambo magumu yaeleweke kwa urahisi na masuala mazito yafahamike hata kwa mtu wa kawaida kabisa. Hivyo kijitabu hiki si kigumu kukielewa na wala si cha kifalsafa sana kama vitabu vyake vingine."


Sasa kama kitabu si kigumu, kwa nini atusaidie kukielewa kwa kuchombeza chombeza chumvi zake? Huyo mwandishi mwizi ndio unamwimbia chereko kwamba amesoma kutupita?
 

Jiongelee wewe.

Hakuna anaejua usomi wa mtu hapa, na kama Mwanakijiji amekwambia wewe kwamba kasoma kutupita mkaribishe chai mkanywe, lakini usituongelee na sisi.

Huyu mwandishi amechukua na kubadilisha maandishi ya mtu kinyume na misingi ya usambazaji vitabu, mawazo na maneno ya mtu mwingine, na akaweka alama za jina lake, ameiba.

Ukisoma "toleo la pili" huwezi jua mstari wa Nyerere unaishia wapi na chombezo za M.M.M. zinaanzia wapi maana amepanga aya upya na kufanya uhariri wake kuchanganya msomaji.

Anasema kwenye utangulizi kwamba amefanya hivyo kurahisisha maandishi ya Nyerere yaeleweke, lakini kwenye utangulizi kasema:
… kukiri kuwa Mwalimu Nyerere alikuwa na uwezo mkubwa wa kufanya mambo magumu yaeleweke kwa urahisi na masuala mazito yafahamike hata kwa mtu wa kawaida kabisa. Hivyo kijitabu hiki si kigumu kukielewa na wala si cha kifalsafa sana kama vitabu vyake vingine."


Sasa kama kitabu si kigumu, kwa nini atusaidie kukielewa kwa kuchombeza chombeza chumvi zako? Huyo mwandishi mwizi ndio unamwimbia chereko kwamba amesoma kutupita?

Hivi kwani Mwanakijiji keshachapisha kitabu hicho au ni majadiliano ya kwenye JF? Mie nimepitia maandiko yote ya Mwanakijiji sikuona mahali ambapo Mwanakijiji kafuta maneno ya Mwalimu na kuweka yake zaidi ya kutoa mawazo yake ambayo ameyaweka katika italics mwanzo wa kila Sura. Kama ni kutumia maandiko ya Mwalimu, naamini kabisa Baba wa Taifa letu alikiandika kitabu hicho akitaka idadi kubwa ya Watanzania wakisome na kuchangia mawazo yao kuhusu yaliyoandikwa. Sioni tatizo liko wapi! Kitabu hicho kilipotolewa kwa mara ya kwanza kiliuzwa kwa bei ya chini kabisa na kilinunuliwa kwa wingi hata na Wamachinga jijini Dar es Salaam.
 
Hivi kwani Mwanakijiji keshachapisha kitabu hicho au ni majadiliano ya kwenye JF?...

Hajachapisha? Kumbe amesimulia hadithi kwenye radio Mwanakijiji?

Hapana shaka amechapisha. Kwenye dibaji yeye mwenyewe amesema hivi:

"Ni lengo langu kutoa changamoto kwa kizazi hicho kwa kuchapisha
kijitabu
hiki cha Mwalimu kwa mtindo na namna hii na hivyo kuyaleta mawazo ya Mwalimu kwa kizazi kipya."


Amesema amechapisha. Unamtetea mtu kwa kumpalia makaa?

Mwandishi mnakili angeandika cha kwake kuchambua mawazo ya mwalimu, sio kutuchombezea na ya kwake. Aidha si kweli kwamba mabadiliko yote kwenye toleo la pili yana alama kama ulivyosema. Alisema kitabu kina makosa ya kiuandishi, hivyo anarekebisha. Sasa ukisahihisha wendelezo au ukiongeza mkato utaweka alama?

Aidha M.M.M. ana mamlaka gani ya kihistoria kutuchambulia mawazo ya Mwalimu Nyerere? Huoni kashindwa hata kuandika cha kwake? Na akiandika kitabu chake huyu M.M.M kwenye utambulisho mchapishaji wake atatuambia huyu ni mtaalam wa siasa na historia gani? Maana ukiniandikia kitabu lazima unijulishe umeyajuaje hayo kuliko mimi na wengine kutuandikia kitabu. Ulikutana na Mwalimu au umemsoma Nyerere shule gani, kwenye makala za mitandao ya Jamiiforums?

Mwandishi mwenyewe alishafiriki, hamuwezi kutuletea tolea la pili kupotosha historia.
 
Tindikali, Niliuliza swali. Asante kwa jibu.

Namtetea kwa msingi kwamba sidhani kuwa yaliyoandikwa kwenye kitabu hicho ni 'taboo' hayapaswi kamwe kuchambuliwa na kujadiliwa na yeyote anayetaka kufanya hivyo.

Mamlaka ya kuchambua mawazo ya Mwalimu maana yake nini? Mwalimu ameandika kitabu ili wananchi wasome, watafakari, wazingatie, wajadili kuhusu yaliyoandikwa na panapowezekana wayafanyie kazi yale waliyoyaelewa kwa manufaa ya Taifa kwa ujumla. Mie nadhani mihutasari ya kiserikali na labda kichama ndiyo yenye siri ambazo zinahitaji 'mamlaka' na ruksa ya kuchambua lakini si mawazo ya Mwalimu aliyoyatoa hadharani kwenye vitabu ama hotuba zake.

Hivi hakuna wanaoandika kujadili mambo waliyoyasoma kwenye vitabu au mahali popote pale? Hivi woteee wanaoandika kuhusu Mwalimu ama kujadili ya Mwalimu lazima wawe wamekutana naye? Kwa maana nyingine hotuba zote alizokuwa akizitoa Mwalimu ndani na nje ya nchi haziwezi kuchambuliwa na kujadiliwa na yeyote ambaye si mtaalam wa siasa na historia? Ina maana alikuwa anatoa hotuba na kuandika vitabu si kwa ajili ya jamii kwa ujumla ila wataalam wa siasa peke yao? Wiki hii wasomi pale Chuo Kikuu walikuwa wakijadili kuhusu Azimio la Arusha ambalo liliandikwa na Mwalimu je yaliyojadiliwa pale na wasomi na wachangiaji wengine wasio wasomi yalikuwa ni batili?

Kama Mwanakijiji kachapisha bila kufuata utaratibu unaohitajika aelezewe tu utaratibu ukoje. Sidhani kwamba hilo ni jambo ambalo haliwezi kurekebishika ili kutoa fursa ya yaliyomo kwenye kitabu hicho kujadiliwa.
 
Kama Mwanakijiji kachapisha bila kufuata utaratibu unaohitajika aelezewe tu utaratibu ukoje. Sidhani kwamba hilo ni jambo ambalo haliwezi kurekebishika ili kutoa fursa ya yaliyomo kwenye kitabu hicho kujadiliwa.

Sawa Bibi Ntilie. Tujadili kitabu. Haya, tunajadili kipi?

Tunajadili kitabu na mawazo ya Mwanakijiji au kitabu na mawazo ya Mwalimu?

Mamlaka ya kuchambua mawazo ya Mwalimu maana yake nini? ... siri ambazo zinahitaji 'mamlaka' na ruksa ya kuchambua
"Mamlaka” kwenye masuala ya uandishi haimaanishi "ruksa," madaraka, nguvu ya kuchapisha kitabu, bali karii, au utaalam ulioiva unaokubalika katika ulingo wa fani fulani. Unapoandika kitabu chochote unategemewa uwe na karii ya kuwachambulia wenzako swala fulani. Isipokuwa kama unaandika tamthilia kama za sungura, fisi na mapenzi.

M.M.M anatuandikia kitabu cha Nyerere, ni nani huyu mtu na anajua nini kuhusu Nyerere kuliko wasomaji? Weledi wa siasa na historia ameupata wapi, anafanya nini sasa hivi katika fani hiyo, au yuko na taasisi gani, wapi?

Eti “toleo la pili” la kitabu cha Nyerere, Nyerere mwenyewe keshafariki, umepoteza goroli?
 

Sawa Bibi Ntilie. Tujadili kitabu. Haya, tunajadili kipi?

Tunajadili kitabu na mawazo ya Mwanakijiji au kitabu na mawazo ya Mwalimu?

"Mamlaka” kwenye masuala ya uandishi haimaanishi "ruksa," madaraka, nguvu ya kuchapisha kitabu, bali karii, au utaalam ulioiva unaokubalika katika ulingo wa fani fulani. Unapoandika kitabu chochote unategemewa uwe na karii ya kuwachambulia wenzako swala fulani. Isipokuwa kama unaandika tamthilia kama za sungura, fisi na mapenzi.


Tindikali,
Asante kwa darasa. Naamini tunachozungumzia ni kujadili kitabu na mawazo ya Mwalimu si ya Mwanakijiji na wala si kuhusu utaalamu wa karii unaouzungumzia. Mwananchi yeyote yule anao uhuru wa kujadili mawazo ya Mwalimu. Pia, naamini kwa dhati kabisa kuwa Mwalimu hakuandika kitabu kile akitaka watakaojaribu kujadili yaliyoandikwa mle lazima wawe na utaalamu unaouzingumzia au wawe wanamjua vyema Mwalimu. Mara nyingi Mwalimu alikuwa akiandika hotuba zake na vitabu kama hiki tunachokizungumzia kwa lugha nyepesi ili wananchi wote wasomi na wasio wasomi waweze kupata ujumbe aliotarajia kuufikisha.

Narudia kusisitiza kwamba naamini kwa dhati kabisa kwamba Mwalimu hakuandika kitabu hicho ama maandiko yake yoyote yale akidhamiria huko mbele iwepo "mamlaka" ya aina yoyote ile itakayosababisha wananchi hata wale mbumbumbu wasiweze kujadili kuhusu aliyowahi kusema ama kuandika. Mwalimu hakuandika kitabu kile kwa ajili ya hao weledi wa siasa na historia kuja kukichambua aliandika kwa ajili ya wananchi wote wa Tanzania waelewe na kuzingatia kuhusu Hatma ya nchi yao.


Eti “toleo la pili” la kitabu cha Nyerere, Nyerere mwenyewe keshafariki, umepoteza goroli?

Ninachokiona kwenye baadhi ya maneno yako Mkuu Tindikali ni jeuri (arrogance) tu na kutotaka watu wajadili kuhusu yaliyoandikwa kwenye vitabu ama hotuba za Mwalimu. Labda hupendi wafanye hivyo kwa sababu zako binafsi na si kwa sababu Mwandishi halisi wa kitabu hicho (Mwalimu) asingelipenda kijadiliwe hata kama ni baada ya kifo chake.

Narudia, kama Mwanakijiji kakosea katika kusema ama kuandika kwamba ni 'toleo la pili' ama hakufuata utaratibu wa nukuu za kitabu hicho aelezwe kistaarabu tu. Lakini ukisema kwamba hastahili kwa sababu ya karii au kwa sababu hana utalaam ulioiva humtendei haki na ni dharau isiyo na sababu.

Aidha inabidi kuwapongeza watu kama Mwanakijiji ambao wako tayari kuyazungumzia mawazo ya Mwalimu hadharani kuliko nyie akina Tindikali ambao huenda mnamjua vizuri Mwalimu na mawazo yake lakini hamtaki kujitokeza kuchambua na kuzungumzia mawazo hayo kwa manufaa ya wananchi na Taifa kwa ujumla. Mmekaa kimya mkiangalia jinsi nchi inavyokwenda kombo. Wakijitokeza watu wanaojaribu kufanya hivyo mnawashukia kwa jeuri ya 'weledi' na maneno makali ya kejeli yasiyo na tija!
 
Mkuu Bibi Ntilie, asante sana kwa msimamo wako.
Mimi naomba niendelee kukijadili kitabu hiki. Wala sina nia sana ya kumtetea mleta hoja!
Inavyoonekana Mwalimu aliandika kitabu hiki aya moja moja akiwa na hasira kila baada ya kukutana na wakuu wa nchi kwenye mikutano yao ya aina mbali mabali ikiwemo ya faragha, wakati wa chai ya jioni na hata wakipata chui baridi,, (mtu asidakie hapa akaanza kudai nimesema Mwalimu alikuwa anapata chui tafadhali!)
Amesema wazi kwenye baadhi ya aya za kitabu hiki. Mwalimu ameandika hiki kitabu siyo kwa furaha hata kidogo, wala hakukiandika kwa ustadi sana. Inaonekana wazi alikuwa anataka aongee na wajukuu zake walioko nchi nzima. Mtanzania na mzalendo kutokijadili kitabu hiki ni kosa kubwa maana yeye ndivyo haswa alivyolenga. Nia ya mtoa hoja ni sawia na sambamba kabisa na ile ya mwalimu. Hata kama ningewekewa tindi kali kiasi gani mbele yangu nigelilitia maji mengi ili nisomapo mjadala wake ziwemo bado za kunitosha kuuelewa kuliko nig'aake ng'aake ovyo. Wallaahi ndivyo ningefanya!
Mwanakijiji hebu waandikie ule mfuko wa Mwalimu waombe kuwa tunahitaji kukichapisha na kukiuza faida inarudi kwenye mfuko huo huo! Tafadhali fanya hima Mkuu!
 
Mkuu Bibi Ntilie, asante sana kwa msimamo wako.
Mimi naomba niendelee kukijadili kitabu hiki. Wala sina nia sana ya kumtetea mleta hoja!
Inavyoonekana Mwalimu aliandika kitabu hiki aya moja moja akiwa na hasira kila baada ya kukutana na wakuu wa nchi kwenye mikutano yao ya aina mbali mabali ikiwemo ya faragha, wakati wa chai ya jioni na hata wakipata chui baridi,, (mtu asidakie hapa akaanza kudai nimesema Mwalimu alikuwa anapata chui tafadhali!)
Amesema wazi kwenye baadhi ya aya za kitabu hiki. Mwalimu ameandika hiki kitabu siyo kwa furaha hata kidogo, wala hakukiandika kwa ustadi sana. Inaonekana wazi alikuwa anataka aongee na wajukuu zake walioko nchi nzima. Mtanzania na mzalendo kutokijadili kitabu hiki ni kosa kubwa maana yeye ndivyo haswa alivyolenga. Nia ya mtoa hoja ni sawia na sambamba kabisa na ile ya mwalimu. Hata kama ningewekewa tindi kali kiasi gani mbele yangu nigelilitia maji mengi ili nisomapo mjadala wake ziwemo bado za kunitosha kuuelewa kuliko nig'aake ng'aake ovyo. Wallaahi ndivyo ningefanya!
Mwanakijiji hebu waandikie ule mfuko wa Mwalimu waombe kuwa tunahitaji kukichapisha na kukiuza faida inarudi kwenye mfuko huo huo! Tafadhali fanya hima Mkuu!

Asante MpendaTz,
Naomba nijihami kwa kusema kwamba utetezi wangu kwa mtoa hoja unatokana na sababu moja tu kwamba amesome kitabu/vitabu vilivyoandikwa na Mwalimu na ameona vina umuhimu wa aina yake na vinahitaji kusomwa na wengi na inapowezekana yaliyoandikwa yajadiliwe na kuzingatiwa. Simjui Mwanakijiji na hanijui zaidi ya kuwa tumo humu JF.

Nakubaliana nawe kwamba ni dhahiri yaliyojiri wakati ule yalimchefua Mwalimu kiasi cha kuamua kuandika kitabu hicho kutokana na matukio moja baada ya jingine. Moja lililowazi katika kitabu kile ni kwamba Mwalimu alijali zaidi mustakabali wa Taifa na jinsi ambavyo uongozi unahitajika kuwa makini katika kushughulikia masuala ya msingi ya kitaifa.

Pamoja na ushauri mzuri kwa Mwanakijiji, ningeongezea pia kwamba si vibaya akajaribu pia kuwatafuta viongozi wa Taasisi ili waweze kubadilishana mawazo kuhusu lolote linalomuhusu Mwalimu. Mzee Butiku alikuwa Private Secretary wa Mwalimu kwa miaka mingi tangu mara baada ya Uhuru hadi anang'atuka urais kwa hiyo yeye anamuelewa Mwalimu na mawazo yake kwa usahihi usio na shaka. Namba za Taasisi ziko kwenye Website yao www.nyererefoundation.co.tz kama sikosei.
 
Asante MpendaTz,
Naomba nijihami kwa kusema kwamba utetezi wangu kwa mtoa hoja unatokana na sababu moja tu kwamba amesome kitabu/vitabu vilivyoandikwa na Mwalimu na ameona vina umuhimu wa aina yake na vinahitaji kusomwa na wengi na inapowezekana yaliyoandikwa yajadiliwe na kuzingatiwa. Simjui Mwanakijiji na hanijui zaidi ya kuwa tumo humu JF.

Nakubaliana nawe kwamba ni dhahiri yaliyojiri wakati ule yalimchefua Mwalimu kiasi cha kuamua kuandika kitabu hicho kutokana na matukio moja baada ya jingine. Moja lililowazi katika kitabu kile ni kwamba Mwalimu alijali zaidi mustakabali wa Taifa na jinsi ambavyo uongozi unahitajika kuwa makini katika kushughulikia masuala ya msingi ya kitaifa.

Pamoja na ushauri mzuri kwa Mwanakijiji, ningeongezea pia kwamba si vibaya akajaribu pia kuwatafuta viongozi wa Taasisi ili waweze kubadilishana mawazo kuhusu lolote linalomuhusu Mwalimu. Mzee Butiku alikuwa Private Secretary wa Mwalimu kwa miaka mingi tangu mara baada ya Uhuru hadi anang'atuka urais kwa hiyo yeye anamuelewa Mwalimu na mawazo yake kwa usahihi usio na shaka. Namba za Taasisi ziko kwenye Website yao www.nyererefoundation.co.tz kama sikosei.

Usiwe na wasiwasi.. kuna mambo mengine yanakuja. Tumekuwa na mawasiliano na familia na wachapishaji wa kijitabu hiki cha awali. Hakuna ugomvi wowote.
 
hicho kitabu nilikua nakitafuta sana
asante sanaaaaaaaaaaaaaaa mkuu
hata kama unakile original kiweke tujue
maana mafisadi wamekificha hakipatikani
kabisa bongo
 
Mwanakijiji siku zote unaishia kusema tuu Mkuu, ila tunashukuru kwa changamoto zako, na jambo la kujiuliza ni kweli tanzania hatuna watu imara kama wewe mwanakijiji? wasiwasi wangu kwako ni kwamba tangu umelikimbia Taifa hii naona hauna mpango wa kurudi ndugu yangu.

Mwanakijiji naomba usiishie kwenye machapisho mkuu, tunakujuwa wewe ni mzalendo na haufurahishwi na yanayoendelea hapa nyumbani,

Mwanakijiji kale kajalida kako kalikuwa msaada mkubwa kwa watanzania, lakini kwa sasa hakaonekani
 
Back
Top Bottom