Toleo jipya la Kamusi ya Kiingereza ya Oxford sasa yaitambua rasmi Twitter.

Richard

JF-Expert Member
Oct 23, 2006
14,929
20,371
Kamusi ya kiingereza inayotolewa na Oxford University Press ya nchini Uingereza iitwayo Oxford English Dictionary, mwezi huu wa June imeingiza neno "Tweet" ambalo linamaanisha kutuma ujumbe kwenda twitter.



Kwenye kamusi hiyo neno Tweet linasemwa kwa kiingereza -"to send message on twitter". Ingawa neno tweet lipo katika kamusi hiyo likimaanisha wimbo wa ndege mdogo aina ya mbayuwayu, sasa limeingizwa rasmi katika kamusi hiyo iliyoanza kuuzwa mapema mwezi huu.

Mtandao wa twitter umekuwa ni maarufu duniani ukivutia watu wa rika zote na kufanya lugha ya kiingereza kukubali neno la twitter kama NOMINO na tweet kama KIARIFU hivyo kufanya maneno hayo kutambulika katika lugha ya kiingereza. Pia neno retweet limo katika kamusi hiyo likimaanisha kubadilishana ujumbe au kwa kiingereza -"sharing anothers tweet".

Katika kile kinachoonekana kwenda na wakati na teknolojia, kamusi hiyo pia imeingiza maneno mengine yanayohusiana na teknolojia ambayo ni "big data", crowdsourcing, e-reader, mouseover, redirect (the noun) au NOMINO na stream the VERB au KITENZI.

Neno "crowdsourcing" ni neno linalomaanisha kitendo cha kukusanya taarifa mbalimbali kutoka kwa watu tofauti kwa njia ya mahojiano ya simu au ana kwa ana lakini kwa minajili ya kutengeneza habari kamili. Njia hii inatumika sana kwenye mataifa yaliyoendelea kwa kuwepo ajira kamili ambapo mtafutaji anaitwa telephone researcher au marketer na kitendo chenyewe -"telephone marketing".

philomelos.png

Mbayuwayu

Pia kuna neno moja la mtaani au misimu au kwa kiingereza "Slang", linalosemwa huko nchini Marekani kwa kiingereza "to have a cow" ambalo linamaanisha kwa kiingereza "to have a fit" likimaanisha kwa kiswahili kwamba mtu amekasirika au amekasirishwa na jambo fulani kiasi cha kutaka kuchukua hatua fulani na neo hili anatumia sana yule jamaa aitwae Bart kwenye tamthiria za Simpsons.

Twitter ni huduma itolewayo kwenye mtandao wa internet inayowawezeha watumiaji wa jamii mbalimbali kwasiliana kwa kutumiana na kusoma ujumbe mfupi au tweets mpaka maneno yafikiayo 140 kwa wakati mmoja.

article-2343053-0220EFAE00000514-531_306x240.jpg

Alama maalum ya Twitter

Nimeona si mbaya kuweka habari hii hapa baada ya kupita katika duka moja kubwa la vitabu hapa ughaibuni ambalo linauza vitabu vya aina zote. Duka hilo liitwalo Waterstones ndilo duka kubwa kabisa la vitabu nchini Uingereza na lina matawi katika karibu miji yote mikubwa nchini humo.

Je kuna maneno yapi mapya ambayo yamejitokeza katika kipindi cha miezi sita iliyopita nchini mwetu Tanzania ningependa kuyapata hapa.
 
Ndiyo maana lugha ya Kiingereza ni kubwa na pana sana ukilinganisha na hii yetu ya Kiswahili kwa sababu taasisi husika za kukuza lugha hiyo zinaenda na wakati kwa kuikuza na kuipanua tofauti kabisa na sisi na Kiswahili chetu.

Bofya hapa upate maana ya Twitter kutoa Oxford Advanced Learner's Dictionary. Pia bofya hapa uone maana ya tweet kutoka kamusi hiyo hiyo ya Oxford.

Halafu, kamusi hiyo hiyo ya Oxford ina hadi maneno 'dala-dala' na 'matatu'. Bofya hapa na hapa ujionee mwenyewe.

Sisi kwenye kamusi zetu hata neno 'bodaboda' halipo!
 
Ni waingereza wanaokwenda Tanzania ndio wanaorudi na maneno hayo kwao na kushiriki kuyaingiza kwenye hizo kamusi.

Sisi tukiwaona wazungu wanakunywa chai na vitumbua kwa mama ntilie kwenye maeneo kama pale posta mpya tunashangaa lakini hatujui kwamba wengi wao wapo pale kujifunza maneno ya kiswahili.
 
Ni waingereza wanaokwenda Tanzania ndio wanaorudi na maneno hayo kwao na kushiriki kuyaingiza kwenye hizo kamusi.

Sisi tukiwaona wazungu wanakunywa chai na vitumbua kwa mama ntilie kwenye maeneo kama pale posta mpya tunashangaa lakini hatujui kwamba wengi wao wapo pale kujifunza maneno ya kiswahili.

Halafu tunapenda kulalamika kuwa eti Kiswahili hakina msamiati wa kutosha kama vile misamiati hushushwa toka mbinguni!

Misamiati huundwa na watumiaji wa lugha husika na kama neno halipo katika lugha yenu basi mnaliazima hivyo hivyo lilivyo au hata kwa kulifanyia mabadiliko kidogo.

Watu wangejua jinsi Kiingereza kilivyoazima misamiati toka kwenye lugha zingine wala wasingesema hivyo wasemavyo.
 
Back
Top Bottom