"Token Muslims" v/s "Tokeni Waislamu"tatizo ni "shule" au ni "Lugha"

Mbunge wa CCM

JF-Expert Member
Nov 13, 2009
475
22
leo nimesikitka sana na mwanJF mmoja aliyemshambulia mwenzake kuwa hana "shule" pale alipochukulia sehemu ya mchango wake kwenye thread ya kamati kuu ya CHADEMA iliyosema...."Token Muslims....." kuwa ni "......Tokeni Waislamu....." nami niliweka maoni yangu pale nikimkosoa vikali yule aliyemshambulia mwenzake. lakini nimeona niwatendee haki watanzania wenzangu kuanzisha thread inayojitegemea tupate kuichangia kwa mapana yake matatizo ya "shule" yetu watanzania.

mwenzetu kashutumiwa "shule" yake kwa sababu ya "lugha" tu. cha kujiuliza ni nani hana shule hapo. ni yule aliyechanganya kiingereza katikati ya kiswahili huku akiiwa na misamiati ya kutosha kabisa ya kiswahili ya kutumia, au ni yule aliyeona kuwa kwa kuwa ile mada ni ya kiswahili, basi pengine neno "token" lilipaswa kuwa "tokeni" na pengine limekosewa kutokana na makosa yauchapaj tu?

masikini watanzania, lugha ya taifa tunayo tumeng'ang'ani ya wenzetu na kuiabudu. atika safari zangu za kimaisha nimewahi kufika china mara kadhaa na kukuta huko maprofesa wengi tu huko wa fani mbalimbali ambao hata kiingeeza cha kuombea maji hawana! nani atasema kuwwa hawa wana tatizo la shule? je, wana tatizo la lugha? au wana tatizo gani sasa?

tatizo lao (kama ni tatizo kweli), basi si jingine bali ni kuelimika. ukielimika kikelikweli utagundua kuwa lugha ni chombo tu cha mawasiliano na ikiwa peke yake haimaanishi "kwenda shule" ndio maana kuna waingereza kwa kuzaliwa ambao hawajui kusoma na kuandika! utasema "wana shule" hawa eti kwa kuwa tu wanaongea kiingereza vizur kuliko maprofesa wa china?

mwisho natoa pole kwa mana JF anayetumia jina "injinia" kwa kushambuliwa ikali kutokana na "shule" ya aliyemshambulia.

matifa yetu yako nyuma sana kwa maendeleo huku eti kuna watu wanjisifu kuwa na "shule" za uhakika, cheki maprofesa na madaktari wa falsafa walivyorundikana kwenye baraza la mawaziri, waulize wamechangia nini kuboresha serikali? hje, ni kwa sababu wana shida ya "shule" kama "injinia" hapana.

tujadili "shule" zetu tafadhari
 
Dah
Anyway mie nahisi tatizo ni sisi wenyewe kutojiamini kwa mfano wachina wanaongea kikwao na majority hawajui kiingereza na pia mbona kuna viongozi wengi tuu duniani ambao hawajui kiingereza mpaka wanawekewa wakalimani? Mie nashauri ingekuwa bora tuka2mia kiswahili kama instructing language katika mashule (Tujivunie na tujiamini kwa kile tulichonacho).

Na ni kweli kabisa kuwa kujua kiingereza sio tija ila inatokana na mazingira andalizi yaliyowekwa, kwa mfano hapo kenya mnasema eti wako juu kielimu hakuna chochote ila tuu ni kwasababu walikuwa british colonialists waliweka msisitizo sana ktk lugha ya kiingereza tofauti na huku Tz ambapo ilitumika kiswahili kama unifying language..
 
How do you say "token Muslims" in Swahili?

unataka neno "token" tu kwa kuwa imejitokeza hapa?

kama hutaki kutunia lugha yako katika maisha ya awaida, huwezi kuijua lugha yako kikamilifu. muhimu jiamini na lugha yako na uiheshimu,mengine utayafahamu tu.

iwe aibu kutumia neno la kigeni na la kwetu lipo

ukombozi wa kweli hauji kwa kuomba samamki bali kwa kujifunza kuvua! upo mkuu?
 
Dah
Anyway mie nahisi tatizo ni sisi wenyewe kutojiamini kwa mfano wachina wanaongea kikwao na majority hawajui kiingereza ............ Mie nashauri ingekuwa bora tuka2mia kiswahili kama instructing language katika mashule (Tujivunie na tujiamini kwa kile tulichonacho).
..
asante mkuu kwa kuliona hili. hivi kama hujui vizuri lugha, unaweza kupata vizuri elimu?

pamoja na kujidanganya na tu-viingereza vya akina blueray tunawza tukasema tunawazidi nini wachina kwa mfano?

ukipita mitaa ya miji ya china hata majina ya biashara, mabango nk, vyote ni kwa kichina na maisha yanaenda bila wasiwasi! wanatumia kichina hichohicho hadi sasa wanashindana na mataifa ya magharibi kwa sayayansi, technolojia, viwanda, biashara nk

huku kwetu wataalamu wetu ni wa kuandika makaratasi tu!

kikwazo ni lugha, tuamke
 
Dah
Anyway mie nahisi tatizo ni sisi wenyewe kutojiamini kwa mfano wachina wanaongea kikwao na majority hawajui kiingereza na pia mbona kuna viongozi wengi tuu duniani ambao hawajui kiingereza mpaka wanawekewa wakalimani? Mie nashauri ingekuwa bora tuka2mia kiswahili kama instructing language katika mashule (Tujivunie na tujiamini kwa kile tulichonacho).

Na ni kweli kabisa kuwa kujua kiingereza sio tija ila inatokana na mazingira andalizi yaliyowekwa, kwa mfano hapo kenya mnasema eti wako juu kielimu hakuna chochote ila tuu ni kwasababu walikuwa british colonialists waliweka msisitizo sana ktk lugha ya kiingereza tofauti na huku Tz ambapo ilitumika kiswahili kama unifying language..

Umenichanganya maana nilidhani unasisitiza utumiaji wa kiswahili, lakini naona sijui hicho ichenye wino mwekundu ni kiswahili kipi?
 
unataka neno "token" tu kwa kuwa imejitokeza hapa?

kama hutaki kutunia lugha yako katika maisha ya awaida, huwezi kuijua lugha yako kikamilifu. muhimu jiamini na lugha yako na uiheshimu,mengine utayafahamu tu.

iwe aibu kutumia neno la kigeni na la kwetu lipo

ukombozi wa kweli hauji kwa kuomba samamki bali kwa kujifunza kuvua! upo mkuu?

Mjibu Bluray swali lake! hata mimi sielewi na nategemea nitafaidika na hilo jibu, Tone muslims maana yake nini??
 
Mjibu Bluray swali lake! hata mimi sielewi na nategemea nitafaidika na hilo jibu, Tone muslims maana yake nini??

anzeni kutumia na kukiheshimu kiswahili mtaelewa. great thinkers mnaomba samaki badala ya kujifunza kuvua wenyewe!

mmmhhh haya!

kwa kuku saidia, kwa kukusaidia kidogo, hapohapo kwenye tarakilishi yaku fungua tovuti yenye kamusi utaona, na nashauri usome na maneno mengine li uwe na misamiati ya kutosha ya lugha yako
 
anzeni kutumia na kukiheshimu kiswahili mtaelewa. great thinkers mnaomba samaki badala ya kujifunza kuvua wenyewe!

mmmhhh haya!

kwa kuku saidia, kwa kukusaidia kidogo, hapohapo kwenye tarakilishi yaku fungua tovuti yenye kamusi utaona, na nashauri usome na maneno mengine li uwe na misamiati ya kutosha ya lugha yako

Kweli kuchamba kwingi kutoka na m@v!... hakuna aliyeomba samaki wala mshipi, Umeulizwa swali dogo unaleta dibaji, walk the talk or cut it out....
 
Back
Top Bottom