only83
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 5,343
- 2,525
Mshauri wa chama hicho Dk Kitila Mkumbo na madiwani wawili, wametiwa mbaroni wakikabiliwa na tuhuma mbalimbali.
Wakati Dk Mkumbo ambaye ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akiwa amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Singida, akituhumiwa kutoa lugha ya matusi kwa mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi (CCM), Mwigullu Nchemba, Diwani wa Kata ya Mabogini Wilaya ya Moshi, Albert Msando na Alex Umbella wa Kata ya Kirua Vunjo Mashariki, wamehojiwa na polisi kwa makosa ya jinai.
Dk Mkumbo amepandishwa kizimbani jana akiunganishwa katika kesi inayomkabili Ofisa wa Sera na Utafiti wa chama hicho kikuu cha upinzani, Mwita Waitara Mwikwabe (37).
Mwanasheria wa Serikali, Maria Mudulugu alidai mbele ya Hakimu Ruth Massamu kuwa, Julai 14 mwaka huu saa 10.00 jioni, mshtakiwa Dk Mkumbo alitoa lugha ya matusi dhidi ya mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi.
Mwanasheria aliiambia mahakama kuwa, Dk Mkumbo alitamka kuwa mbunge huyo ni malaya, mzinzi na ni 'the comedy' (msanii), huku akijua wazi kuwa kitendo hicho ni kinyume cha sheria.
Mwansheria Mudulugu alisema kuwa mshtakiwa alitoa lugha hiyo ya matusi kwenye mkutano wa hadhara wa Chadema uliofanyika katika viwanja vya kituo cha mabasi cha Kijiji cha Nguvumali Kata ya Ndago, Jimbo la Iramba Magharibi.
Mshtakiwa alikana shtaka hilo na yupo nje baada ya kudhaminiwa wa watu wawili. Kesi hiyo itatajwa tena Julai 30 mwaka huu.
Wakati huo huo, vijana wawili wakazi wa Kata ya Ndago, Paulo Nashakigwa (27) na Emmanuel Shilla (24) wamepandishwa kizimbani katika mahakama hiyo wakituhumiwa kushiriki kumuua Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Yohana Mpinga (30).
Mudulugu alidai mbele ya mahakama hiyo kuwa Julai 14 mwaka huu, majira ya alasiri wakiwa katika Kijiji cha Nguvumali Kata ya Ndago wote kwa pamoja wakitumia fimbo na mawe, walimpiga Yohana na kusababisha afariki dunia.
Washtakiwa hawakutakiwa kujibu chochote kwa vile mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi za mauaji.
Washtakiwa hao wameunganishwa na wenzao 12 ambao wamesomewa shtaka hilo la mauaji Julai 16 mwaka huu. Kesi hiyo itatajwa tena Julai 30 mwaka huu.
Wakati Dk Mkumbo ambaye ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akiwa amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Singida, akituhumiwa kutoa lugha ya matusi kwa mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi (CCM), Mwigullu Nchemba, Diwani wa Kata ya Mabogini Wilaya ya Moshi, Albert Msando na Alex Umbella wa Kata ya Kirua Vunjo Mashariki, wamehojiwa na polisi kwa makosa ya jinai.
Dk Mkumbo amepandishwa kizimbani jana akiunganishwa katika kesi inayomkabili Ofisa wa Sera na Utafiti wa chama hicho kikuu cha upinzani, Mwita Waitara Mwikwabe (37).
Mwanasheria wa Serikali, Maria Mudulugu alidai mbele ya Hakimu Ruth Massamu kuwa, Julai 14 mwaka huu saa 10.00 jioni, mshtakiwa Dk Mkumbo alitoa lugha ya matusi dhidi ya mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi.
Mwanasheria aliiambia mahakama kuwa, Dk Mkumbo alitamka kuwa mbunge huyo ni malaya, mzinzi na ni 'the comedy' (msanii), huku akijua wazi kuwa kitendo hicho ni kinyume cha sheria.
Mwansheria Mudulugu alisema kuwa mshtakiwa alitoa lugha hiyo ya matusi kwenye mkutano wa hadhara wa Chadema uliofanyika katika viwanja vya kituo cha mabasi cha Kijiji cha Nguvumali Kata ya Ndago, Jimbo la Iramba Magharibi.
Mshtakiwa alikana shtaka hilo na yupo nje baada ya kudhaminiwa wa watu wawili. Kesi hiyo itatajwa tena Julai 30 mwaka huu.
Wakati huo huo, vijana wawili wakazi wa Kata ya Ndago, Paulo Nashakigwa (27) na Emmanuel Shilla (24) wamepandishwa kizimbani katika mahakama hiyo wakituhumiwa kushiriki kumuua Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Yohana Mpinga (30).
Mudulugu alidai mbele ya mahakama hiyo kuwa Julai 14 mwaka huu, majira ya alasiri wakiwa katika Kijiji cha Nguvumali Kata ya Ndago wote kwa pamoja wakitumia fimbo na mawe, walimpiga Yohana na kusababisha afariki dunia.
Washtakiwa hawakutakiwa kujibu chochote kwa vile mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi za mauaji.
Washtakiwa hao wameunganishwa na wenzao 12 ambao wamesomewa shtaka hilo la mauaji Julai 16 mwaka huu. Kesi hiyo itatajwa tena Julai 30 mwaka huu.