Toka Nyerere mpaka Samia, Tumekuwa na Viongozi maslahi ya Chama na siyo Taifa

Hamatan

JF-Expert Member
Nov 10, 2020
3,183
7,645
JULIUS KBARAGE NYERERE

Mwalimu Nyerere aliwahi kutamka kuwa katiba tuliyo nayo ni mbaya kwa sababu inamfanya Rais kuwa Mungu mtu. Akaonya pia kuwa siku akitokea Rais mbaya, nchi itajuta kwa sababu hakuna atakayemzuia kufanya chochote kwa sababu katiba inampa Rais mamlaka yasiyo na mipaka. Miaka 30 baadaye imekuja kudhihirika.

Tafakuri: Mwalimu alijua kuwa katiba ni mbaya. Alijua kuwa katiba mbaya italitesa Taifa. Kwa nini kipindi chote cha utawala wake hakufanya jitihada za kuibadilisha hii katiba mbaya tuliyo nayo?

ALI HASSAN MWINYI

Akaja Rais Mwinyi. Mwinyi, katika kitabu cha maisha yake anasema wazi kuwa Mwalimu alitaka mgombea binafsi aruhusiwe, na vyama viruhusiwe kuungana, lakini Kamati kuu ya CCM licha ya kuona uzuri wa kuwa na mgombea binafsi, na uzuri wa kuruhusu vyama kuungana, ilikataa kwa kuhofia kuwa mambo hayo yakiruhusiwa, CCM ingeweza kupoteza madaraka kiurahisi.

Tafakuri: Mwinyi alijua hila za CCM, na umuhimu wa kuwa na demokrasia halisi kuliko hii ya kiinimacho tuliyo nayo, kwa nini katika kipindi chake cha utawala cha miaka 10, hakufanya jitihada ya kuibadilisha hii katiba mbaya tuliyo nayo?

BENJIMIN WILLIAM MKAPA

Rais Mkapa, alijua uovu mbalimbali unaolindwa na katiba. Kwenye kitabu chake cha maisha yake, Mkapa alidai kuwa angependa kuiona Tanzania yenye Tume huru ya uchaguzi. Ina maana anajua fika kuwa Tume ya uchaguzi tuliyo nayo siyo huru.

Tafakuri:
Kwa nini Rais Benjamin Mkapa hakufanya jitihada za kuwa na katiba mpya akiwa madarakani?

JAKAYA KIKWETE

Jakaya Kikwete alijua fika unafiki na siasa za hila za CCM za kutozingatia maslahi ya Taifa kwanza, alijitahidi akaanzisha mchakato wa kupata katiba mpya. Lakini baadaye, hata huo mchakato ukaonekana ni kiinimacho.

Tafakuri:
Ni kweli, Kikwete aliingia kwenye mgogoro mkubwa na CCM, ambayo miaka yote imezoea kuendesha mambo kwa hila na ulaghai, lakini kwa nini hakuuvaa ujasiri ili asimame na Taifa kuliko kusimama na chama ambacho daima kimekuwa na nia ovu?

JOHN POMBE MAGUFULI

Huyu hakuwa na cha kujutia. Labda Mungu angemruhusu amalize uongozi wake, baada ya kutoka kwenye madaraka, huenda naye angeongelea ubaya wa katiba tuliyo nayo, kama walivyofanya wenzake.

Rais Magufuli, ni kama ndiye aliyetabiriwa na Mwalimu. Maana kipindi chake, mambo ya ajabu aliyatenda, hata bila ya kuzingatia sheria, kanuni, na katiba ya nchi. Alifanya alivyotaka, na aliyenyanyuka kutaka kuhoji, kama aliishi, alikiona cha mtemakuni.

Tafakuri:
Hata baada ya kuumizwa vikali na utawala wa awamu ya tano, hatujapata funzo bado?

SAMIA SULUHU HASSAN

Tangu aingie madarakani amekuwa akiongelea na kufanya mabadiliko ambayo tafsiri yake ni kuwa utawala uliopita ulionea watu, ulipora hela za watu wa nguvu, uliwadhulumu watu haki za kidemokrasia, uhuru wa maoni na kuwabagua.

Tafakuri:
Kama Rais Samia ana dhamira ya dhati, kwa nini asiende kwenye kiini cha tatizo ili matatizo tuliyoyashudia kwa muda mrefu yaondoke, na yasirudi tena?

Ukitafakari kwa umakini, kizuizi kikubwa cha ustawi wa Taifa letu ni CCM.

Polisi wanashindwa kufanya kazi kwa weledi na kwa haki kwa sababu ya CCM. CCM mara kadhaa imetumia jeshi la Polisi kuwakandamiza, kuwakomoa au hata kuwaangamiza wapinzani wao wa kisiasa.

Idara ya usalama wa Taifa inashindwa kufanya kazi kwa welwdi kwa sababu ya CCM. CCM ndio wanaoifanya taasisi hii muhimu kwa Taifa iache mambo muhimu yenye maslahi kwa Taifa, na kujishughulisha zaidi na siasa, na hasa kutumika na CCM dhidi ya wapinzani.

Mahakama nayo imepoteza weledi. Majaji una nyakati wamerumika kulinda maslahi ya CCM badala ua maslahi ya Taifa na haki za wananchi.

Bunge limekuwa kama idara ya chama. Bunge limekuwa pahali pa kupiga porojo na vijembe dhidi ya wapinzani, huku wanaofanywa hivyo wakilindwa kwa nguvu zote na spika. Marehemu Magufuli aliwahi kumwagiza spika, kwa uwazi kabisa, mbele ya umma, kuwa awafukuze wabunge ndani ya bunge ili wakitoka nje, yeye aweze kuwashugulikia. Agizo hilo spika alilitekeleza vizuri sana, na wabunge wa uoinzani walionja shubiri kwa kiwango kisichoweza kupimika.

Kwa ujumla CCM haina hata chembe ya huruma kwa wananchi wala Taifa. Kipaumbele chake ni kuhakikisha inabaki madarakani iwe kwa haki au dhuluma, iwe kwa amani au shari, iwe kwa uhai au mauaji.

CCM inaogopwa na Polisi, TISS, mahakama na Bunge. CCM inaogopwa na marais.

Wananchi wasipojitegemea wenyewe, wakasimama kwa dhati na ujasiri wa kuamua kupata katiba mpya, kwa manufaa ya Taifa, wasitegemee kama itapatikana kwa mapenzi ya CCM au Rais aliyopo madarakani. Kipingamizi kikubwa cha kuyapata maendeleo ya kweli kwa Taifa letu, ni katiba yetu mbovu. Na kipingamizi kikubwa cha kupata katiba nzuri inayoweza kulifaa Taifa letu, wakati wote, imekuwa ni CCM na Rais ambaye yupo madarakani.

Samia hata awe na dhamira njema kiasi gani kwa Taifa, bila ya katiba nzuri mpya, hawezi kufanikiwa, na hata akitaka kuwepo na katiba mpya, hatafanikiwa kuishinda CCM iliyotopea kwenye siasa ovu bila ya kujitoa mhanga wa kujitenga na uovu wa CCM, na kusimama na umma wa haki kwa manufaa ya Taifa.

Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Magufuli na sasa Samia, ukitazama juu juu, unaweza kuamini kuwa wanalipenda Taifa kuliko CCM, lakini ukweli ni kuwa wanaipenda CCM kuliko Taifa. Walikuwa tayari kushiriki na kuubariki uovu wa CCM ili tu wasitengane na wenzao ambao kwao CCM ni lazima iwe madarakani hata kama itabidi kumtumia ibilisi.

Tamko: ADUI MKUBWA WA USTAWI WA KWELI WA TAIFA LETU KWA KUPITIA KATIBU ILIYO BORA, NI CCM. Adui hashangiliwi, bali anapingwa, anashambuliwa na kuondolewa. Vinginevyo, adui abadilike na kuwa rafiki na kungana na walio wema katika kutafuta na kutenda mema.
 
Madaraka matamu Sana, muulize Lowassa atakwambia utamu wa madaraka, pia uliza viongozi mbalimbali kwa nini wanawaandaa watoto wao na kuwakabidhi mikoba ya siasa yote hii ni utamu wa madaraka.

Kwa mimi nilitegemea mtetezi wa wanyonge angetimiza azima ya kuleta katiba mpya lakini nae akalewa madaraka na kuanza mambo ya ajabu, nilitegemea mtetezi wa wanyonge angeondoka madarakani akiwa ameacha katiba ya wananchi lakini zaidi alididimiza mpaka demokrasia , mtetezi wa wanyonge alitetea tumbo lake na ukanda wake over.
Ngoja tuangalie mama anatupeleka wapi? Hakika kiongozi wa kweli ni Yule ambae ,ataleta katiba mpya, tume huru.
Vinginevyo ni porojo tu.

Madaraka ni matamu, viete, Benz na vingine lazima uwasahau wananchi.
 
"Hakika kiongozi wa kweli ni Yule ambae ,ataleta katiba mpya, tume huru.
Vinginevyo ni porojo tu"

Huu ndiyo ukweli. Bila hilo, yeyote yule, awe ni huyu wa sasa au wengine wajao, tujue ni wale wale. Anayeipenda Tanzania kwa dhamira, atataka Tamzania yenye misingi ya ustawi, na hilo huwezi kulipata nje ya katiba bora mpya.

Ili kufahamu kama Samia ni tofauti na wenzake au la, tumpime katika hili.

Nyumba haijengwi kwa kuanza na paa, bali kwa kuanza na msingi. Msingi wa nchi ni katiba. Mama Samia kwa sasa anahangaika na paa, lakini hili paa litapeperusha na upepo wakati wowote kama hakuna la maana linalofanywa kwenye msingi.
 
Mtawala yeyote ambaye ni ccm hawezi kusaidia kuleta Katiba mpya na Tume huru ya uchaguzi, maana wanajua ccm haiwezi kuendelea kutawala kukiwa na Tume huru.

 
Ukweli usiopingika
Hata wakitaka kuleta mabadiliko,Upinzani wa ndani ni mkubwa sana, kuna wengi wanafaidika na mfumo CCM.

Kama alishindwa Kikwete.
Sitarajii SASHA.

Dawa itoke mikononimwetuWtanzania wenye nia safi ya kuleta Mabadiliko kw kuyalazimisha.
Tukiogopa Jela na Vifo ,basi tuendelee kusubiri ashuke Malaika Mwenye Nguvu kumzidi Shetani.
Lakini Mungu ndiye aliyetuumbia Mfumo wa kuleta Mbadiliko lazima Tugharamike. Hakuna kupata mabadiliko kwa Sala na Maombi tuu.
Lazima tufanye Maamuzi Magumu .
 
Ukweli usiopingika
Hata wakitaka kuleta mabadiliko,Upinzani wa ndani ni mkubwa sana, kuna wengi wanafaidika na mfumo CCM.

Kama alishindwa Kikwete.
Sitarajii SASHA.

Dawa itoke mikononimwetuWtanzania wenye nia safi ya kuleta Mabadiliko kw kuyalazimisha.
Tukiogopa Jela na Vifo ,basi tuendelee kusubiri ashuke Malaika Mwenye Nguvu kumzidi Shetani.
Lakini Mungu ndiye aliyetuumbia Mfumo wa kuleta Mbadiliko lazima Tugharamike. Hakuna kupata mabadiliko kwa Sala na Maombi tuu.
Lazima tufanye Maamuzi Magumu .
Kuna haja ya sisi wananchi kuunganisha nguvu na kuunda vuguvugu la kupata katiba mpya kwa faida ya Taifa letu.

Tusisubirie embe chini ya mbuyu.
 
Tafakuri: Mwalimu alijua kuwa katiba ni mbaya. Alijua kuwa katiba mbaya italitesa Taifa. Kwa nini kipindi chote cha utawala wake hakufanya jitihada za kuibadilisha hii katiba mbaya tuliyo nayo?
Jibu jepesi hapo ni kwamba, kwa wakati husika ilihitajika iwepo kwa mazingira yaliyokuwepo.

Sasa mazingira yalishabadilika, lakini wanaokuja kuitumia hiyo katiba hawataki ibadilishwe, kwa sababu inawanufaisha wao.

Lakini sio kweli kusema kwamba
Rais mbaya, nchi itajuta kwa sababu hakuna atakayemzuia kufanya chochote kwa sababu katiba inampa Rais mamlaka yasiyo na mipaka.
"...hakuna atakayemzuia kufanya chochote kwa sababu katiba inampa Rais mamlaka yasiyo na mpaka."

Si kweli, kwa sababu mamlaka yote yapo kwa wananchi. Wananchi wakikataa katiba, ni lazima hiyo katiba itaondoka, pamoja na huyo rais mbaya anayeitumia.

Mamlaka yote hutokana na utashi wa wananchi, sasa kama wananchi hawajipangi ili kutimiza mamlaka yao, hilo ni swala tofauti.
 
Jibu jepesi hapo ni kwamba, kwa wakati husika ilihitajika iwepo kwa mazingira yaliyokuwepo.

Sasa mazingira yalishabadilika, lakini wanaokuja kuitumia hiyo katiba hawataki ibadilishwe, kwa sababu inawanufaisha wao.

Lakini sio kweli kusema kwamba

"...hakuna atakayemzuia kufanya chochote kwa sababu katiba inampa Rais mamlaka yasiyo na mpaka."

Si kweli, kwa sababu mamlaka yote yapo kwa wananchi. Wananchi wakikataa katiba, ni lazima hiyo katiba itaondoka, pamoja na huyo rais mbaya anayeitumia.

Mamlaka yote hutokana na utashi wa wananchi, sasa kama wananchi hawajipangi ili kutimiza mamlaka yao, hilo ni swala tofauti.
Kinadharia, kwa kiasi kikubwa upo sahihi. Kiuhalisia siyo kweli.

Mwalimu aliposema kuwa Rais akitaka kufanya chochote, hakuna wa kumzuia, alimaanisha hakuna utaratibu wa wazi na uliorahisi wa kikatiba na wa kuweza kumzuia Rais kufanya mambo ambayo yapo kinyume cha sheria, katiba au matakwa ya wananchi.

Kwa mfano, wakati wa utawala wa awamu ya 5, kinyume ya matakwa ya katiba na sheria za nchi, Rais Magufuli alisema ni marufuku vyama vya siasa (isipokuwa CCM) kufanya mikutano ya kisiasa. Kila mmoja alijua kuwa tamko la Rais lilikuwa ni kinyume cha katiba na kinyume cha sheria iliyoanzisha mfumo wa vyama vingi, lakini ni nani aliweza kumzuia? Rais Magufuli alimwondoa CAG kinyume cha katiba, nani angeweza kumzuia, kama mngetaka kumzuia, ni utaratibu gani mngeufuata wa kisheria kupinga maagizo haramu yale ya Rais Magufuli?

Mahakamani huwezi kwenda, kwa sababu Rais hashtakiwi. Ukiandamana, polisi wanaweza kukuvunja miguu, kukuweka uozee mahabusu au kukutengenezea kesi ya uhujumu uchumi ili ukae mahabusu kwa wakati usiojulikana. Ukipiga kelele, wasiojulikana wangeweza kukuteka, kukupoteza, au maiti yako ikashudiwa imetupwa pembeni ya bahari, na hata uchunguzi wa waliokutendea uovu huo, ukazuiwa.

Kwa katiba yetu ya sasa, njia pekee ya kumzuia Rais kutenda anachotaka, kama yeye Rais aking'ang'ania kufanya, labda kufanya maasidhidi ya Serikali yake, kitu ambacho ni patapotwa maana anaweza kutumia vyombo vya dola dhidi ya wananchi, na kusababisha maafa makubwa.
 
Wananchi hawahitaji katiba kuchukua madaraka yao. Hapo hakuna nadharia, ni uhalisia wakitaka kufanya hivyo.
Mwaka 2020 kulitakiwa kuwe na uchaguzi mkuu. Na mchakato wake ulistahili kuanzia na kura za maoni.

Cha kushangaza, ndani ya CCM, robo tatu ya wagombea wote waliopitishwa kugombea, hawakuchaguliwa na wajumbe, bali walipitishwa na Rais ambaye alikuwa ndiye Mwenyekiti wa CCM Taifa. Anakatwa mgokvea aliyepata kura za maoni zaidi ya 300, anapitishwa aliyepata kura 3. Wagombea wa upinzani, asilimia kubwa walikatwa ili wale walioteuliwa na Rais wapite bila kupingwa. Wagombea wachache wa upinzani walioachwa kugombea, Rais kwa kupitia agizo lake kwa wakurugenzi, walizuiwa kutangazwa washindi hata kama wangeshinda. Mwisho wa yote, si ndani ya CCM wala nje ya CCM, ambako kulikuwa na mtu wa kuzuia matakwa ya Rais Magufuli, japo kila mmoja alijua ni kinyume cha katiba.

Hili ndilo aliloliona Mwalimu Nyerere.
 
Kinadharia, kwa kiasi kikubwa upo sahihi. Kiuhalisia siyo kweli.

Mwalimu aliposema kuwa Rais akitaka kufanya chochote, hakuna wa kumzuia, alimaanisha hakuna utaratibu wa wazi na uliorahisi wa kikatiba na wa kuweza kumzuia Rais kufanya mambo ambayo yapo kinyume cha sheria, katiba au matakwa ya wananchi.

Kwa mfano, wakati wa utawala wa awamu ya 5, kinyume ya matakwa ya katiba na sheria za nchi, Rais Magufuli alisema ni marufuku vyama vya siasa (isipokuwa CCM) kufanya mikutano ya kisiasa. Kila mmoja alijua kuwa tamko la Rais lilikuwa ni kinyume cha katiba na kinyume cha sheria iliyoanzisha mfumo wa vyama vingi, lakini ni nani aliweza kumzuia? Rais Magufuli alimwondoa CAG kinyume cha katiba, nani angeweza kumzuia, kama mngetaka kumzuia, ni utaratibu gani mngeufuata wa kisheria kupinga maagizo haramu yale ya Rais Magufuli? Mahakamani huwezi kwenda, kwa sababu Rais hashtakiwi. Ukiandamana, polisi wanaweza kukuvunja miguu, kukuweka uozee mahabusu au kukutengenezea kesi ya uhujumu uchumi ili ukae mahabusu kwa wakati usiojulikana. Ukipiga kelele, wasiojulikana wangeweza kukuteka, kukupoteza, au maiti yako ikashudiwa imetupwa pembeni ya bahari, na hata uchunguzi wa waliokutendea uovu huo, ukazuiwa.

Kwa katiba yetu ya sasa, njia pekee ya kumzuia Rais kutenda anachotaka, kama yeye Rais aking'ang'ania kufanya, labda kufanya maasidhidi ya Serikali yake, kitu ambacho ni patapotwa maana anaweza kutumia vyombo vya dola dhidi ya wananchi, na kusababisha maafa makubwa.
Sasa mkuu Hamatan, haya uliyoeleza hapa kweli yanaruhusiwa na katiba yoyote, hata hiyo mbovu iliyopo? Hebu fikiria vizuri jambo hili, tusijaze tu kurasa humu ndani.

Haya yote yalifanyika nje ya katiba hiyo hiyo mbovu.

Hebu niambie, kiongozi wa aina hiyo, utatunga katiba ya aina gani ya kumzuia asifanye yake nje ya katiba hata ingekuwa nzuri kiasi gani?
 
Hili ndilo aliloliona Mwalimu Nyerere
Sijui; lakini sidhani kuwa ndilo hili alilokuwa akilisemea.

Huyu unayemzungumzia hapa, hakufuata aina yoyote ya katiba, hata hiyo mbovu, hakuifuata. Angeifuata hiyo iliyopo, hali ingekuwa ni tofauti na hayo uliyoeleza humu ndani.
 
Hatukuhitajika kabisa kuwa na katiba tulizowahi kuwa nazo. Tulitakiwa tuwe na katiba bora siku ya kuwanza tulipopata uhuru.
Jibu jepesi hapo ni kwamba, kwa wakati husika ilihitajika iwepo kwa mazingira yaliyokuwepo.

Sasa mazingira yalishabadilika, lakini wanaokuja kuitumia hiyo katiba hawataki ibadilishwe, kwa sababu inawanufaisha wao.

Lakini sio kweli kusema kwamba

"...hakuna atakayemzuia kufanya chochote kwa sababu katiba inampa Rais mamlaka yasiyo na mpaka."

Si kweli, kwa sababu mamlaka yote yapo kwa wananchi. Wananchi wakikataa katiba, ni lazima hiyo katiba itaondoka, pamoja na huyo rais mbaya anayeitumia.

Mamlaka yote hutokana na utashi wa wananchi, sasa kama wananchi hawajipangi ili kutimiza mamlaka yao, hilo ni swala tofauti.
 
Mjinga
Jibu jepesi hapo ni kwamba, kwa wakati husika ilihitajika iwepo kwa mazingira yaliyokuwepo.

Sasa mazingira yalishabadilika, lakini wanaokuja kuitumia hiyo katiba hawataki ibadilishwe, kwa sababu inawanufaisha wao.

Lakini sio kweli kusema kwamba

"...hakuna atakayemzuia kufanya chochote kwa sababu katiba inampa Rais mamlaka yasiyo na mpaka."

Si kweli, kwa sababu mamlaka yote yapo kwa wananchi. Wananchi wakikataa katiba, ni lazima hiyo katiba itaondoka, pamoja na huyo rais mbaya anayeitumia.

Mamlaka yote hutokana na utashi wa wananchi, sasa kama wananchi hawajipangi ili kutimiza mamlaka yao, hilo ni swala tofauti.
 
Sasa mkuu Hamatan, haya uliyoeleza hapa kweli yanaruhusiwa na katiba yoyote, hata hiyo mbovu iliyopo? Hebu fikiria vizuri jambo hili, tusijaze tu kurasa humu ndani.

Haya yote yalifanyika nje ya katiba hiyo hiyo mbovu.

Hebu niambie, kiongozi wa aina hiyo, utatunga katiba ya aina gani ya kumzuia asifanye yake nje ya katiba hata ingekuwa nzuri kiasi gani?
Kama tungekuwa na katiba ambayo inavipa vyombo vya usalama wajibu wa kuwajibika kwa umma, na pia katiba inayoruhusu wakuu wa vyombo vya usalama na Rais, kushtakiwa wao kama watu binafsi, wanapokiuka sheria na katiba, ingesaidia sana. Katiba iondoe kinga yoyote ya kisheria kwa kiongozi yeyote.
 
Back
Top Bottom