Mwaka wa kutoa hesabu huu,vipi bado inatafunwaNdugu wana JamiiForums,
Nchi yetu imetafunwa mno na ni wakati sasa tuseme imetosha. Tumsaidie Rais Magufuli na Serikali yake kuweza kuzifahamu kero zetu za yanayotusumbua kama watanzania ambayo tungependa yafanyiwe kazi.
Karibuni sana.
MWONGOZO: Elezea jipu/kero yako na kama ina ufafanuzi wa kutosha (nani, wapi, lini, kivipi n.k) ukiambatana na nyaraka itapendeza zaidi.
Kero hizi zitachapwa na kupelekwa kwa mamlaka husika ili zifanyiwe ufuatiliaji.
Si mmeng'ang'ania shangazi. Anapenda misifa na kujikwezaBarabara kuu ya kata ya Manolo kutoka makao makuu ya kata, Manolo, kwenda Shume Nywelo ni mbovu miaka nenda rudi. Wakulima wa kata hii wana bidii sana ya kulima. Wanakatishwa tamaa ya maendeleo na barabara hii. Mazao yao ya nyanya na viazi mviringo na maharagwe yanauzwa kwa bei ndogo kwa sababu ya ubovu wa barabara hii. (Wilaya ya Lushoto). Mkurugenzi Mkuu, Tarura, upo?
Tatizo la wakulima na wafugaji bado ni kubwa.Hapa kiukweli kazi bado ni mbichi,na wateule wa Rais wameshindwa kabisa .Katika maeneo yenye wafugaji kwa wingi hasa Wamasai,wanafanya wanavyotaka.Na hii ni kwa sababu wafugaji hawa,hasa Wamasai kama nilivyosema,wamewaweka viongozi mifukoni,iwe Polisi au viongozi wa kisiasa.Imefika mahali sasa ni kama wao ndio wanaosimika viongozi wa kisiasa.Wanachanga hela wanampa mgombea ambaye wanaamini atasimamia maslahi yao ili akahonge wajumbe.Hili limekuwa jambo la kawaida sasa,hata katika msimu huu wa uchaguzi.No naomba serikali isiruhusu Wamasai ku-take hostage wakulima,this is a situation which has the potential of breaking peace.Sema sisi wakulima tunakua wavumilivu,ila naomba nitoe angalizo,uvumilivu una mwisho,na isichukuliwe as a sign of weakness.Ndugu wana JamiiForums,
Nchi yetu imetafunwa mno na ni wakati sasa tuseme imetosha. Tumsaidie Rais Magufuli na Serikali yake kuweza kuzifahamu kero zetu za yanayotusumbua kama watanzania ambayo tungependa yafanyiwe kazi.
Karibuni sana.
MWONGOZO: Elezea jipu/kero yako na kama ina ufafanuzi wa kutosha (nani, wapi, lini, kivipi n.k) ukiambatana na nyaraka itapendeza zaidi.
Kero hizi zitachapwa na kupelekwa kwa mamlaka husika ili zifanyiwe ufuatiliaji.