Toka kwa Wananchi: Kero na vitendo vya kifisadi vinavyoendelea nchini vinavyotakiwa kufuatiliwa

sina ushahidi wa Takwimu but I know for a fact Ndalichako ni bomu tunalolilea,inawezekana msione sasa hivi,ngoja akae achumie tumbo lake ilhali anaiua Tanzania
 
USHAURI!
1. Ondoa wakurugenzi waliowekwa kiukada, hawana msaada wowote wa kuendesha mambo kiueledi zaidi ya siasa
2.Mchezo wa kupotezana, kutekana, kuumizana ni ushamba na dalili za kushindwa kujibu hoja kwa hoja
3. Achana na kuteua watu KIDINI, kuteua watu kwa mrengo wa udini ni kujibania pool ya talent za kusaidia maendeleo kwa upofu wa "hawa ni wenzangu" na "wale si wenzangu", wakati kumbe ni taifa la watu walewale tu, jahazi likizama tunazama wote!
4. Ondoa white elephants projects, Uza ndege hizo pesa tuingize kwenye umeme wa gesi
5. Kuua private sector ni kuturudisha kwenye siasa za uchumi zilizofeli za Julius Nyerere, ni aina ya uchumi muflisi
6. Nchi lazima iwe na mipango endelevu, siyo kila anyekuja anakuja na ishu zake, anavunjavunja zile alizoshiriki kuzipitisha
7. Lazima sheria za nchi, uhuru wa watu, Demokrasia na Utaalam viheshimiwe
8. Rudisha Trilion zetu 2.4
9. Hakikisha unaenda mahakamani kudai Trilion zetu 424 tulizoibiwa na ACACIA, Mtu akisamehe hizo ni mhaini, huwezi kusamehe pesa inayolingana na bajeti ya nchi ya miaka 15 halafu usiwe msaliti!
10. Elimu bora na siyo bora elimu, lazima Elimu ya vitendo itiliwe mkazo, siyo matheory ambayo ukishapiga NECTA unatupa kule hayakusaidi choochote, lete elimu ya ujasirimali, ufundi kama vile ujenzi, umeme, vyombo vya moto, electronics, computer, mabomba, ufugaji, ususi, ushonaji etc. Hiyo ndo elimu ya maana, Siyo habari za Historia ya Ulaya kwenye middle ages, itanisaidia nini mimi?
 
1. Ondoa wakurugenzi waliowekwa kiukada, hawana msaada wowote wa kuendesha mambo kiueledi zaidi ya siasa
2.Mchezo wa kupotezana, kutkana, kuumizana ni ushamba na dalili za kushindwa kujibu hoja kwa hoja
3. Achana na kuteua watu KIDINI, kuteua watu kwa mrengo wa udini ni kujibania pool ya talent za kusaidia maendeleo kwa upofu wa "hawa ni wenzangu" na "wale si wenzangu", wakati kumbe ni taifa la watu walewale tu, jahzilikizama tunazama wote!
4. Ondoa white elephants projects, Uza ndege hizo pesa tuingize kwenye umeme wa gesi
5. Kuua private sector ni kuturudisha kwenye siasa za uchumi zilizofeli za Julius Nyerere, ni aina ya uchumi muflisi
6. Nchi lazima iwe na mipango endelevu, siyo kila anyekuja anakuja na ishu zake, anavunjavunja zile alizoshiriki kuzipitisha
7. Lazima sheria za nchi, uhuru wa watu, Demokrasia na Utaalam viheshimiwe
8. Rudisha Trilion zetu 2.4
9. Hakikisha unaenda mahakamani kudai Trilion zetu 424 tulizoibiwa na ACACIA, Mtu akisamehe hizo ni mhaini, huwezi kusamehe pesa inayolingana na bajeti ya nchi ya miaka 15 halafu usiwe msaliti!
10. Elimu bora na siyo bora elimu, lazima Elimu ya vitendo itiliwe mkazo, siyo matheory ambayo ukishapiga NECTA unatupa kule hayakusaidi choochote, lete elimu ya ujasirimali, ufundi kama vile ujenzi, umeme, vyombo vya moto, electronics, computer, mabomba, ufugaji, ususi, ushonaji etc. Hiyo ndo elimu ya maana, Siyo habari za Historia ya Ulaya kwenye middle ages, itanisaidia nini mimi?

Kasema uje na takwimu! ;););):D..nakutania,nimeipenda hii posti
 
Serikali. Iweke lugha ya Kiswahili kwe ofisi za serikali mafano kama mahakamani, polisi hospitali, form ziwe za Kiswahili. Tanzania lugha yake ni kiswahili na sisi ndiyo wa Swahili wenyewe kwa nini watuchoshe!!?
 
Wewe umeshamshauri nini ngosha kwenye huu uzi.
Sina la kumshauri zaidi ya kuongeza muda wake wa utawala ili mlioko huko Tanzania mfurahie matunda yake nami siku nikirejea nikute kuna mwingine ambaye atakuwa anafuata njia zake alizotengeneza kwa miaka 30 ya uongozi wake.
 
Naiomba Serikali ya nchi yangu ya Tanzania itafakari mambo yafuatayo kwa marefu na mapana yake.

1. Suala la Stiglers Godge. Ni bomu linaloenda kuripuka na kuzamisha uchumi wa nchi. Wataua viumbe hai, watu watapiga pesa na umeme hautopatikana. Kwa nn imeachana na umeme wa Gesi?

2. Kutokushirikiana na wapinzani. Huu nao ni ujinga. Hakuna tatzo ambalo limetokea nchini bila kutahadharishwa au kutolewa maelezo na Wapinzani, serikali imekua ikipuuza. Ununuzi wa ndege, Accasia, Korosho, Stiglers Godge, Vitambulisho vya machinga, tekana tekana etc

3. Katiba bora. Serikali ianzishe mchakato wa kutunga katba iliyo bora itakayozifanya tasisi nying kujiongoza na kuepukana na ombwe la kila kiongozi kuja na mambo yake kichwani na kuvuruga yaliowahi kutendwa.

Mambi ni mengi
 
TCRA waweke katazo ya sms za matangazo ya hizi kampuni za bahati nasibu.... Nashauri wawe wanatuma sms mwisho tano wakiona muhitiko haupo wakupotezee na mchezaji watume walahu kumi tangu mara ya mwisho kucheza wakiona kimya waachane nawe maana imekuwa kero mno inapoteza muda wakati mwingine umebanwa na majukumu ya kazi unasikia sms imeingia kwenye simu unaenda angalia unakutana na sms ya hizi kampuni na wengine sio washiriki ila tunasumbuliwa kama vile wadahu wakongwe vile Nawasilisha
 
Mimi nawashauri wanaojenga Stiegler Gorge, wawafahamishe watanzania kwamba: kwa kuwa mto ambako hilo bwawa linajengwa ni mto mchang; kijiolojia mto ambao ni mchanga huwa una kazi tatu ambazo huitwa Erosion, Transport and Deposition, je, maji yatachukua muda gani kujaa kwenye Bwawa ili liweze kutoa umeme? Na je. Itachukua muda gani kwa tope kujaa na kuathiri nguvu ya bwawa kutoa umeme? Je. Gharama ya kusafisha bwawa hilo litakuwa kiasi gani?
 
Back
Top Bottom