Toka kwa Wananchi: Kero na vitendo vya kifisadi vinavyoendelea nchini vinavyotakiwa kufuatiliwa

Hii miradi ya kupaka rami juu nskumwaga chupping juu barabara za MWANZA nyegezi to Buhongwa nijipu, maana mashimo km lile LA,sahara Na barabara Kuu yanaachwa wahusika iangalieni tanroad mza
 
Tatizo fisadi kuu ndio yuko mstari wa mbele kwenye vita ya ufisadi na tayari ameshazunguka akili za wajinga na ni vigumu sana kwa hao wajinga kuamini kwamba anaweza akawa fisadi.
 
Vingozi wa dini hawana muda maalum wa kuasa jamii kuhusu yale wanayoyaona hayako vyema,ni vyema tukawaacha waendelee kwa kuwa hata tukiwapinga hawataacha kutuamsha,lakini hata kwa kusema hayo kwako ni mtizamo wako hamna atakayekupinga,hii ni nchi yetu sote tusiiache ikateketea kwa sababu yoyote ile,mtizamo wangu
 
Ndugu wana JamiiForums,

Nchi yetu imetafunwa mno na ni wakati sasa tuseme imetosha. Tumsaidie Rais Magufuli na Serikali yake kuweza kuzifahamu kero zetu za yanayotusumbua kama watanzania ambayo tungependa yafanyiwe kazi.

Karibuni sana.

MWONGOZO: Elezea jipu/kero yako na kama ina ufafanuzi wa kutosha (nani, wapi, lini, kivipi n.k) ukiambatana na nyaraka itapendeza zaidi.

Kero hizi zitachapwa na kupelekwa kwa mamlaka husika ili zifanyiwe ufuatiliaji.
She kero kubwa Ni Barabara kwa wakaazi wa kigamboni maeneo ya financial Mata wa sile
 
Mheshimiwa waziri wa Nishati Tanzania, sisi ni wakazi wa mtaa wa Ilangamoto, Halmashauri ya mji Makambako, mkoa wa Njombe.
Katika mtaa huu kuna wakazi wengi lakini pia kuna shule moja na Kiwanda kinachojengwa.
Sisi wananchi wa mtaa huu wa Ilangamoto tumekuwa tukiomba huduma ya UMEME tangu mwaka 2016 bila mafanikio.
Kwa kuwa sababu kubwa ya kucheleweshewa huduma hii imekuwa ikitajwa kama ni Bajeti, tunaomba Mh.Waziri wa Nishati kwa mamlaka yako utusaidie kupata huduma hii kwa wakati muafaka.
Ahsante.
 
Utasikia basi limeua wanne,
Piki piki imeua sita,
Au waliokufa muhimbili wamefika 100 kwa mwaka jana,
Meli ya Nungwi imeua 60,

Na hao ni wateja wa M-PESA, Tigo pesa na Airtel money,

Hela zao zinaendaga wapi?

Kuna utaratibu upi wa kuwapatia survivorship au next of kin wao?
Hili nalo neno
 
Maabala zilizojengwa mashuleni hazikamishwi.

Kama mtu kakwamisha si abainishe kuna shida gani?
Ni hasara kwani wananchi walishatimiza wajibu wao hadi hapo zilipo.

Sasa serikari si imalizie?
 
Kero kubwa ni barabara zinazoonganisha mkoa wa katavi, Tabora na Kigoma.. Pia kero nyinginezo Mhe Rais aje Katavi Kwan tangu alivyofanya kampeni ya uchaguzi 2015 kwa kuzindulia kampeni zake huku HAJARUDI MPAKA LEO, ila CHATO NA KANDA YA ZIWA anakwenda thaana
 
Ndugu wana JamiiForums,

Nchi yetu imetafunwa mno na ni wakati sasa tuseme imetosha. Tumsaidie Rais Magufuli na Serikali yake kuweza kuzifahamu kero zetu za yanayotusumbua kama watanzania ambayo tungependa yafanyiwe kazi.

Karibuni sana.

MWONGOZO: Elezea jipu/kero yako na kama ina ufafanuzi wa kutosha (nani, wapi, lini, kivipi n.k) ukiambatana na nyaraka itapendeza zaidi.

Kero hizi zitachapwa na kupelekwa kwa mamlaka husika ili zifanyiwe ufuatiliaji.
Nafikiri kwa namna ambavyo Rais anavyofanya kazi, hizo kero zitaondoka tu, kikubwa ambacho tunatakiwa kufanya ni kumuombea tu ili aweze kutekeleza yote haya
 
Mahakama ya mwanzo Sinza kitengo cha Mirathi: Dada anayehusika na mirathi ni jipu,anaomba rushwa waziwazi bila aibu,anaomba Nauli! Anakalia mafaili ya watu tangu mwaka 2016,anasumbua watu nenda rudi kila siku,anapoteza documents za watu! Huyo dada ni kero naomba achunguzwe na vyombo husika kisha atumbuliwe.
 
Wazanzibari hawataki muungano wameuchoka kweli kweli hili nalo ni big jipu mfikishie km ataweza kulitumbua😕😕
 
Kero kubwa kw nchi yetu kwa sasa ni hili wimbi la watu kujiuzuru ubunge au udiwani na kujivua uanachama wa chama kimoja na kukimbilia chama kingine.
Naliona jambo hili kama ni uhujumu wa uchumi maana Taifa linalazimika kutumia mabilioni ya shilingi kwenye uchaguzi mdogo wa kuziba nafasi hizo. Napendekeza watu hawa kupelekwa na kushitakiwa kwenye mahakama ya wahujumu uchumi kwa kulitwisha Taifa mzigo wa uchaguzi mdogo kwa makusudi. Pesa ambazo zingetumika kwenye huduma ya jamii au kwenye maendeleo fulani tunalazimika kuziingiza kwenye uchaguzi. Huu ni uhujumu uchumi.
 
Mita za maji za prepaid kwanza DAWASCO izipeleke kwa wadaiwa sugu alafu hizo pesa wanazowadai za nyuma ndo wakubaliane zilipwe kidogo kidogo. Hapo tutatatua maji yanayopotea zaidi ya 40%
 
Back
Top Bottom