Toka kwa Wananchi: Kero na vitendo vya kifisadi vinavyoendelea nchini vinavyotakiwa kufuatiliwa

RUSHWA MAHAKAMA YA MWANZO SINZA
wakazi wa Sinza waliofungua mirathi kwenye mahakama hii wanazungushwa njoo leo njoo kesho bila kujua hatma ya mirathi yao iliyofunguliwa tangu 2016,2017 na 2018.
Mhasibu wa mahakama anaomba rushwa waziwazi ili kuprocess majalada ya mirathi, Anaomba nauli, hela ya maziwa eti majalada yana vumbi.
Tunaomba huyu mhasibu mdada afanyiwe Special Audit ili ijulikane kama ameghushi na kuiba mirathi ya watu! Haiwezekani miaka 3 watu wanasubili mirathi ili hali wamekamilisha taratibu zote.

CC: Jaji mkuu
CC: Jaji Kiongozi
CC:Waziri wa sheria na katiba
CC: RC Dar es salaam
CC: DC Ubungo
 
Ningepewa Urais hata kwa siku 10 tu, ningehakikisha kwanza MBWA KOKO wote wanachagua moja kati ya mambo mawili:- Ama kuacha kejeli, matusi na dharau au kutafuta Nchi ya kuishi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ufanisi katika mahabara nyingi za hospital za serikali zinatia shaka inafikia laboratory attendant anarudisha majibu ya uwongo kwa doctor,ethics haipo kabisa,mtumishi mmoja wa hospital hiyo tajwa huwa anarudi na form anajazia tuu nyumbani kesho anarudisha kwa Dr. eti ni majibu.
Jipu uchungu nimeliona hospitali ya Mwananyamala kitengo cha maabara watu wanaanza kupewa huduma saa tano. Na wakati wafanyakazi wanafika ofisini saa moja wao ni stori tu na kuacha wagonjwa wanaendelea kuzidiwa....

Mtu amepima toka jana lakini kumpa tu majibu yake asubiri hadi saa tano ndo waanze kutoa majibu....wao na stori tu ofisini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna wafanyakazi wa TANROADS wanakuwa na gari Hardbody Ya Tanroads nyeupe inasimama njia ya Msata - Bagamoyo mida ya usiku, wanakula rushwa kwa kila fuso za mizigo zinazopita njia ile.

Kwa siku wafanyakazi hao huenda nyumbani na sh3m.

Tuanze na jipu hilo kwanza maana huo mchezo ulikuwepo tangu yeye akiwa waziri wa ujenzi.

utaifakwanza
Barabara ya Makongo - Ardhi University imekua kero kubwa.Hii ni ring-road but ujenzi umeishia upande cha Goba. Magari yanayopita hii barabara ni mengi, more than 70,000 per day. Tunaomba TANROAD wajitahidi, wamalize ujenzi wa barabara hii. Kwa kweli imekua ni kero kubwa kwa watumiaji na wakazi wa barabara hii.
 
Jambo la Msingi: Naomba kama una taarifa kuhusu mtu usomuelewa mtaani kwako mtolee taarifa huenda akawa ni mtu asiyejulikana...

Watu wasiojulikana wanalimaliza Taifa na wanatia hofu Raia. Kila Raia ana haki ya kuishi bila khofu. Haikupaswa kuwa hivi

Tanzania ya miaka hii inaogopesha...

Tahadhari katika Reply. "MIMI SI MWANA SIASA" nimeonelea nina Haki ya kuppst linalonikera nalo ni hilo tu!
 
Jambo la Msingi: Naomba kama una taarifa kuhusu mtu usomuelewa mtaani kwako mtolee taarifa huenda akawa ni mtu asiyejulikana...

Watu wasiojulikana wanalimaliza Taifa na wanatia hofu Raia. Kila Raia ana haki ya kuishi bila khofu. Haikupaswa kuwa hivi

Tanzania ya miaka hii inaogopesha...

Tahadhari katika Reply. "MIMI SI MWANA SIASA" nimeonelea nina Haki ya kuppst linalonikera nalo ni hilo tu!
Watu wasiojulikana ni CCM mbona unapata taabu kuwajua?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Zimesalia siku 30 kabla ya maadhimisho ya mei mosi 2019, Je, Mheshimiwa Rais ambaye ndiye mgeni Rasmi wa Maadhimisho, unapendekeza atatue kero IPI ili kuifanya mei mosi 2019 ya kipekee na yenye maana kwa watumishi wa umma kuelekea uchumi wa viwanda?. Toa maoni yako na wahusika watamfikishia.

Mimi kwa upande wangu nashauri amuagize CAG kukagua payroll za Taasisi za umma ili kubainisha Viwango vya mishahara kama vinaendana na elimu, ujuzi, uzoefu wa kazi na majukumu dhidi ya mishahara yao na kama wenye vyeo Fulani wanavistahili au LA, tukianza na maafisa Elimu nchi nzima, aafisa kilimo, wakurugenzi na wakuu was wilaya, makatibu tawala n.k na uwajibikaji wao ukilinganisha na maslahi manono wayapatayo
 
Ndege tayari, Standadi geji imekaribia kukamilika, flai ova ilee sasa Mzee baba Ongeza huo mshahara kwa 100% kama ulivyoahidi.

Watumishi tuendelee kuchapa kazi Maendeleo hayana Chama.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wazo lako mkuu no zuri kabisa kwamba kila MTU alipwe kulingana na ujuzi wake alionao pamoja na elimu pia .swala lingine ni kuhusu hatma ya kuwarudisha ama kuwalipa watumishi halali wa darasa LA saba waliohujumiwa ajira zao haiwezekani kuwarudisha basi walipwe mafao yao ya makato ya mifuko waliokua wanachangia. Kisheria .na watumishi tuliokazini tuongezewe mishahara kulingana na Elimu , na Taaluma zetu pia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aje na hoja ya salary standardization

Ni aibu sana yaani wote mmesoma masters ya education lakini mkija kwenye malipo ya kazi unakata tamaa.

Alieajiriwa Udsm kwa Mfano, ataanza na 2.4Milioni, alieajiliwa Chuo cha Ualimu likely wanaweza kufika 1.3Milion. Njoo kwa Walimu wa kawaida unaweza kupewa increment 2 ambazo hazivuki hata elfu 70000/=.

Sasa hapo nashindwaga hata kushangaa masters ukiwa chuoni sheria na utaratibu za kudahili ni zilezile, vigezo vya kuwa awarded hiyo masters ni hivyo hivyo na ajira unapangiwa na mwajiri wako hujipangii maana kama ni hivyo ningechagua kwenye green pasture.

Hii huwa inatukatisha tamaa sana na wakati mwingine hata ukirudi kazini na masters yako no body cares.

Mi nadhani ikiwekwa mishahara kwa kuangalia academic merits itasaidia hata usipopata cheo ambavyo ni vigumu kuvipata utalipwa unachostaili.

Ndio tupo tunakodoa macho na hiyo salary standardization likely inaweza kuondoa hii tofauti. Academic merits kiwe kigezo cha kwanza kulipwa mishahara na katu isiwe vyeo au kada mtu anayoifanyia kazi. Maana vyeo kuna watu wamo kwenye nafasi fulani by chance hata kada pia ndugu ulishatuathiri hapo nyuma.

Ila kusoma ni kujiendeleza na effort binafsi ambazo zinahitaji uwezo wako upstairs na kujitoa kuacha mambo mengine uboreshe career yako. Kwenye ualimu mambo hayapo hivyo hii kada inahitaji jicho la ziada
 
Awakate mishahara hadi 50% tujenge mareli,mabandari,maeapoti,mastigilaz goji nk. Tuwanyooshe hawa watumishi wanaiponda ccm.
 
Zimesalia siku 30 kabla ya maadhimisho ya mei mosi 2019, Je, Mheshimiwa Rais ambaye ndiye mgeni Rasmi wa Maadhimisho, unapendekeza atatue kero IPI ili kuifanya mei mosi 2019 ya kipekee na yenye maana kwa watumishi wa umma kuelekea uchumi wa viwanda?. Toa maoni yako na wahusika watamfikishia. Mimi kwa upande wangu nashauri amuagize CAG kukagua payroll za Taasisi za umma ili kubainisha Viwango vya mishahara kama vinaendana na elimu, ujuzi, uzoefu wa kazi na majukumu dhidi ya mishahara yao na kama wenye vyeo Fulani wanavistahili au LA, tukianza na maafisa Elimu nchi nzima, aafisa kilimo, wakurugenzi na wakuu was wilaya, makatibu tawala n.k na uwajibikaji wao ukilinganisha na maslahi manono wayapatayo
Ajiuzulu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
58 Reactions
Reply
Back
Top Bottom