Zanzibar 2020 Toka CHADEMA ianzishwe haijawahi kuwa na ushawishi Zanzibar

jingalao

JF-Expert Member
Oct 12, 2011
35,053
28,245
Kwa political analysists wazuri watakubaliana na mimi kuwa katika uhai wake kama Chama cha Siasa kimefail kuwa na ushawishi katika upande wa pili wa muungano. Jambo hili halina afya nzuri kwa chama cha siasa Tanzania kwani kinapaswa kuwa na uwezo, wanachama na nguvu katika pande zote za muungano.

Hii inaweza kuwa ni ishara ya Chama hicho kwa makusudi kutaka kuigawa nchi vipande vipande. Kwa mwenye akili anaweza kuhoji kwa nini miaka yote CHADEMA imeacha au kushindwa kuandaa nguvu ya represantation huko Zanzibar? Hii ni ishara ya namna gani wengi wanakichukulia chama hiki kama ni cha ukanda. Kisingizio cha kuunga mkono juhudi kimekuwa kinajirudia mara kwa mara.

Nikitolea mfano wa CUF, chenyewe kimeweza na kufanikiwa kupata uungaji mkono kutokea Zanzibar hadi bara, kilichowashinda CHADEMA ni nini? Nikiiangalia ACT imeweza kujipenyeza kutoka bara hadi Zanzibar. CHADEMA ikiri kuwa ni chama chenye misingi mibovu ya kushawishi umoja wa kitaifa. Hii ni mojawapo ya sababu kwa nini kinaangukia pua katika kila uchaguzi.
 
Hata CCM Zanzibar haina ushawishi bali hulazimisha kupendwa kwa nguvu
Hata hao CCM wapo kwa ajili ya madaraka.

Wanapata uteuzi wa ubalozi,ukurugenzi ,Ubunge, na teuzi nyingi ambazo zipo mikononi mwa Rais ambaye ni mwenyekiti wa CCM.
Siku CCM ikiondoka madarakani bara basi Zanzibar itapotea kabisa kabisa mana itakua haina maslahi kwao.

Waunguja wanabaki CCM kwa sababu ya njaa . Wengi wananufaika na Siasa na ajira tu hawana uwezo wa kujiajiri tofauti na Wapemba ambao wamejaa kila upande wa Dunia wakiwa wamejiajiri wenyewe . Wapemba wanaingia kwenye siasa kwa sababu wamechoka kubaguliwa na kudhulumiwa haki zao lakini hawatafuti maslahi kama wanaCCM waliojaa Unguja kuganga njaa.
 
Toka mfumo wa vyama vingi uanzishwe nchini, hata CCM haijawahi shinda uchaguzi Zanzibar
 
Back
Top Bottom