Togo, Burundi na Malawi wameonesha njia; Tanzania tufuate!

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,975
Yaliyotokea katika chaguzi kuu za nchi za Togo, Burundi na Malawi yameonyesha kuwa nchi za Afrika zinaweza kufanya Uchaguzi Mkuu ulio huru kwa amani na utulivu lakini kikubwa zaidi, zikapata viongozi wake bila kutegemea jicho la waangalizi wa kimataifa walioko nje ya Afrika.

Janga la COVID-19 limetoa funzo muhimu kwa nchi za Afrika kuhusu uwezo wa kuendesha chaguzi zake kuu bila kutegemea ''kiranja'' anayetoka nje ya Afrika (Ulaya na Marekani).

Walianza wananchi wa Togo ambao mwezi wa pili (February) walipiga kura za kuwachagua viongozi wao bila ya uwepo wa wasimamizi kutoka nje ya Afrika. Uchaguzi ulimalizika kwa amani na utulivu ambapo asilimia 76 ya wapiga kura walijitokeza kupiga kura .

Zoezi hili lilifuatiwa na nchi ya Burundi ambayo nayo mwezi wa tano (Mei), walifanya Uchaguzi wa amani na utulivu bila ya uwepo wa waangalizi kutoka nje ya Afrika. Uchaguzi ulimalizika kwa amani na utulivu ambapo asilimia 88 ya wapiga kura walijitokeza kupiga kura.

Nchi ya Malawi imekuwa ya tatu kufanya Uchaguzi Mkuu bila uwepo wa waangalizi wa nje ya Afrika. Uchaguzi wake umefanyika kwa amani na utulivu ambapo asilimia 64 ya wapiga kura walijitokeza kupiga kura.

Nchi ya Ethiopia ambayo ilikuwa pia inategemea kufanya Uchaguzi Mkuu mwezi wa nane (Augosti) bila waangalizi wa kutoka nje ya Afrika lakini Waziri Mkuu, Abiy Ahmed ameahirisha Uchaguzi huo bila kupanga tarehe nyingine. Maamuzi haya yamemfanya Spika wa Bunge kujiuzuru akimtuhumu Waziri Mkuu kwa kuvunja katiba kwa kuendelea kuwa madarakani baada ya muda wake wa kikatiba.

Mwezi wa tisa (Septemba) tutashuhudia pia wananchi wa Jamhuri ya Shelisheli wakipiga kura ya kumchagua Rais wa nchi bila uwepo wa waangalizi wa nje ya Afrika.

Baada ya Jamhuri ya Shelisheli, Tanzania tutafuatia mwezi wa kumi (Oktoba).

Chaguzi hizi zote zimedhihirisha na kutoa angalizo kuwa chaguzi nyingi katika nchi za Afrika huwa zinakuwa sio za amani na utulivu kutokana na waangalizi kutoka nje ya Afrika (Ulaya na Marekani) kuwa na ajenda zao zinazosababisha kuvunjika kwa amani na utulivu katika nchi za Afrika.

Nchi za Afrika zimekuwa zikiaminishwa kuwa bila kuwa na waangalizi kutoka nje ya Afrika (Ulaya na Marekani), basi Uchaguzi hauwezi kuwa huru nawa amani na utulivu. Janga la COVID-19 limeondoa hii mithiologia.

Nchi za afrika kwa sasa zimeonyesha uwezo mkubwa katika kuendesha chaguzi zake huru na zikamalizika kwa amani na utulivu chini ya waangalizi kutoka Jumuiya ya Afrika na asasi za kiraia za ndani ya nchi zake.

Huu ni ushindi mkubwa kwa nchi za Afrika.
 
Sheria zetu haziruhusu uchaguzi wa Rais kupingwa mahakamani kama tulivyoona Malawi.

Lakini kama Malawi au tunavyoona nchi zingine, kura huwa zinaibiwa na kupata matokeo yasiyo haki na huru.

Je, iwapo mwaka huu 2020 kura za urais zikaibiwa na baadhi ya wagombea na vyama vyao wakashindwa kukubaliana na matokeo nini kitafanyika?

Je, itabaki kauli ya "tunamuachia Mungu" na kumpa kazi ambayo siyo yake na tayari alisha ikasmisha kwetu kwa vile tuna utashi tofauti na ng'ombe?

Kwa vile WIZI huu hauna utatuzi ulio wekwa wazi kisheria ni bora tuujadili namna bora ya jukabiliana nao kabla haujatokea maana kusubiri mpaka utokee unaweza leta madhara hata ya machafuko.

Malawi, Zambia nk waliweza kwa nini sisi tukose ufumbuzi?
 
Wapinzani tokea mwaka 1995 wamekuwa wakidai wanaibiwa kura! Nini kimetokea tokea mwaka 1995?

Unauliza swali wakati jibu limetoka tokea mwaka 1995!
 
Wapinzani tokea mwaka 1995 wamekuwa wakidai wanaibiwa kura! Nini kimetokea tokea mwaka 1995?

Unauliza swali wakati jibu limetoka tokea mwaka 1995!
Swali/jibu lako liko katika mfumo wa kujisifu na majidai juu.

Kwamba hakuna lililofanyika tokea 1995 walipi anza wizi wao kumbe ni fahari? But this is 2020 na pengine Malawi wametoa somo la kupigania maamuzi yao.

Swali lilikuwa, wao sheria inaruhusu kwenda mahakamani jee huku ambako sheria iko kimya tumuachie Mungu?
 
Sheria zetu haziruhusu uchaguzi wa Rais kupingwa mahakamani kama tulivyoona Malawi.

Lakini kama Malawi au tunavyoona nchi zingine, kura huwa zinaibiwa na kupata matokeo yasiyo haki na huru.

Je, iwapo mwaka huu 2020 kura za urais zikaibiwa na baadhi ya wagombea na vyama vyao wakashindwa kukubaliana na matokeo nini kitafanyika?

Je, itabaki kauli ya "tunamuachia Mungu" na kumpa kazi ambayo siyo yake na tayari alisha ikasmisha kwetu kwa vile tuna utashi tofauti na ng'ombe?

Kwa vile WIZI huu hauna utatuzi ulio wekwa wazi kisheria ni bora tuujadili namna bora ya jukabiliana nao kabla haujatokea maana kusubiri mpaka utokee unaweza leta madhara hata ya machafuko.

Malawi, Zambia nk waliweza kwa nini sisi tukose ufumbuzi?
Sisi bado tupo nyuma sana katika masuala ya demokrasia.Nchi ipo mikononi mwa watu wachache
 
Wezi wa kura hapa nchni kwetu ni serikali yenyewe ikitumia vyombo vya dola.
Unamwishtaki nani wakati wale waliotakiwa kulinda sheria na katiba wamekuwa wahalifu??
 
Wezi wa kura hapa nchni kwetu ni serikali yenyewe ikitumia vyombo vya dola.
Unamwishtaki nani wakati wale waliotakiwa kulinda sheria na katiba wamekuwa wahalifu??
tapatalk_1592681667868[1].jpeg
Kwa urahibu huu unaweza kukumbuka idadi ya kura zilizotangazwa na msimamizi wa uchaguzi!
 
Swali/jibu lako liko katika mfumo wa kujisifu na majidai juu.

Kwamba hakuna lililofanyika tokea 1995 walipi anza wizi wao kumbe ni fahari? But this is 2020 na pengine Malawi wametoa somo la kupigania maamuzi yao.

Swali lilikuwa, wao sheria inaruhusu kwenda mahakamani jee huku ambako sheria iko kimya tumuachie Mungu?
Huku ambako sheria iko kimya au inabariki wizi huo basi umma unaoibiwa uchukue sheria mkononi mwao hakuna jinsi nyingine, swali ni jee umma umeandaliwa vya kutosha?
 
Sheria zetu haziruhusu uchaguzi wa Rais kupingwa mahakamani kama tulivyoona Malawi.

Lakini kama Malawi au tunavyoona nchi zingine, kura huwa zinaibiwa na kupata matokeo yasiyo haki na huru.

Je, iwapo mwaka huu 2020 kura za urais zikaibiwa na baadhi ya wagombea na vyama vyao wakashindwa kukubaliana na matokeo nini kitafanyika?

Je, itabaki kauli ya "tunamuachia Mungu" na kumpa kazi ambayo siyo yake na tayari alisha ikasmisha kwetu kwa vile tuna utashi tofauti na ng'ombe?

Kwa vile WIZI huu hauna utatuzi ulio wekwa wazi kisheria ni bora tuujadili namna bora ya jukabiliana nao kabla haujatokea maana kusubiri mpaka utokee unaweza leta madhara hata ya machafuko.

Malawi, Zambia nk waliweza kwa nini sisi tukose ufumbuzi?
Hapa kwetu ukijaribu kutafuta ufumbuzi unaambiwa umetumwa na mabeberu,unafanya uchochezi.Najaribu kutafakari na kuwaza kama chui akiwa hakimu mbuzi atapata haki yake?

Mwenye kuamua Tume yetu ya Uchaguzi inavyoundwa,inavyofanya kazi Naye ni mgombea,hivi anaweza kuwa muungwana kiasi gani hadi aunde Tume Huru ambayo inaweza kumtangaza mgombea mwingine kushinda?

Tumemsikia akitamka,tumeshuhudia yaliyotendeka katika uchaguzi za marudio za ubunge,udiwani na hatimaye serikali za mitaa na matokeo yake,bado tuamini kuwa nitakuwa na uchaguzi Huru na haki chini ya Tume hii?

Tusidanganyane,Watanzania tumegeuzwa mazuzu na watawala,wanatunga sheria na kanuni kabdamizi zinazominya Uhuru wa Wananchi kuchagua viongozi wanaowakubali.Kulazimisha kuwatawala wanadamu ni kitu kibaya sana na huleta chuki.
 
Kule Zanzibar wao wanasema ENOUGH IS ENOUGH kama wakiiba kura huenda yakajirudia ya 2001.
Kutugawa ndiyo silaha wanayotumia hawa jamaa,utasikia kuna Uzanzibar na Ubara,Unguja na Pemba,CDM,CUF,NCCR,ACT Wazalendo nk ili msimtambue adui yenu.Nia ni kuwafanya msiongee lugha moja.Sheria na kanuni kandamizi zinapitishwa/kuungwa mkono kishabiki hatimaye zikishapita zinachinjia demokrasia baharini.
Kuelekea uchaguzi wa 2020 mipango ya kuiba kura imekamilika na hayafanyiki kwa uficho tena na asilimia za ushindi wamepanga.Jukumu la kila mzalendo wa nchi hii kupaza sauti zetu kupinga hilo kwa kusema na kutenda-kura zetu zinaweza kututoa hapa.
 
Yaani Burundi ndio mfano wa kuigwa? Hahahaha no offence. Lakin ni.moja ya mifano ya kipumbavu kabisa
 
Wapinzani tokea mwaka 1995 wamekuwa wakidai wanaibiwa kura! Nini kimetokea tokea mwaka 1995?

Unauliza swali wakati jibu limetoka tokea mwaka 1995!

Hata Afrika tulitawaliwa toka miaka ya mwishoni ya karne ya 18, lakini tulikuja kujikomboa miaka zaidi ya 70 mbele.
 
Sio kila njia wanayopitia wenzio itakuwa ni njia sahihi ama bora na kwako pia kuipitia.
 
Back
Top Bottom