OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,189
- 103,708
Tazama nchi inaenda ikiwa imepoteza uelekeo kabisa. Tazama dreva ameendelea kubaki kwenye usukani wakati gari imekata sukani na shokapu. Tazama raia na upinzani wamedhurumiwa huku wasanii wetu wakiwa kimya kwamba hayawahusu.
Lakini ukimya huu umeshawishi watesi wanafikiria ukusanyaji wa kodi na tozo za ajabu ajabu kila kukicha.
Sasa imefika zamu ya kulima tozo mitandao ya kijamii. Ambayo ndio jukwaa la wasanii kumwaga sera zao. Mtabaki kujipendekeza kwa CCM kama mlivyofanya wakati wengine wananyanyaswa?
Msikilize Msaani wa vichekesho Eric Omondi akisemea mashabiki zake. Nyie wenzangu mtabaki kuimba matusi tu na kushindana followers.