Tofauti ya Matajiri wa Mikoa ya Kaskazini na Kusini mwa Tanzania

Mkuu kuduman201036 huyo wa katikati ya Malawi na Kongo anakupigiaje simu?hebu tupe hiyo stori[/Q Niliwahi mtembelea shemeji yangu MKE wa kaka nilipofika mara nilimuona anahangaika na simu ' akaniomba samahani ''shem'' hapa ninatafuta life kuna mtu ninawasiliana nae hivyo ananipa maelekezo , mara tukaambiwa wote tutoke nje ,woote nyumba ifungwe kwa saa moja hakuna mtu kuingia ndani ,kwa maelezo ya huyo shem wangu ni kwamba ndani kuna vifaa alivitayarisha kwa ajili ya kupokea mzigo zaidi ya milion 500 kati ya hizo million 100 zichomwe moto na majivu apelekewe huko mpakani .sasa hizo million 400 jinsi ya kuzitumia mashart yake daaaaaaah mm hoi.
 
Wakinga hawana tofauti na wamakonde unakuta jitu lina hela,halafu linalala chini,havai viatu,kutwa anashindia kuvaa msuli,msosi anaokula sasa duuh...utajiri wa kiboya.
 
Mkuu barafu ngoja hawa jamaa wakutumie bomu la juu kwa juu,maana umewasimanga sana
Yaani kuna Mkinga hapa ofisini kwetu tumemuonyesha hii "thread" imemchekesha sana,mpaka sasa tunamuita Mwandulami au Mwakipande...Yaani kasema 85% ya bandiko hili ni kweli,hizo chache zilizobaki amuachia mwandishi kwa "chuki" zake kwa Wakinga....ha ha ha ha ha ha ha ha ha
 
Dunia hii haina mipaka. Kuna watu wako Arusha, Moshi na huko kote mnakoita kaskazini wanapata utajiri kwa jitihada zao, na pia wapo wengi tu wanatumia uchawi, wizi kama akina Massawe, kuuza madawa ya kulevya kama akina Mosha n.k. Lakini pia kuna matajiri walioko nyanda za juu kusini, wanaopata utajiri kwa nguvu zao wenyewe, tena hawa ni wengi zaidi; nenda njombe, makambako, mafinga, uporoto, mbarali, mbozi ukaone vijana wanavyojishughulisha na kilimo n.k.

Kuna makabila kama wakinga wana historia ya kufanya sana kazi. Miaka ya themanini na sabini wakinga walikuwa wakifanya kazi kwenye jamii za kihehe, kiwanji, wanyakyusa n.k. Hata kipindi hicho uchawi ulikuwepo lakini walikuwa bado jitihada zao binafsi hazijawanufaisha.

Utumiaji wa pesa huendana na desturi. Baadhi ya jamii zimefundishwa kutunza pesa kulingana na ugumu wa kupata pesa. Kuna baadhi ya jamii huwa zina allergy na akaunti yenye pesa. Kama ni kijana kapata pesa atashinda bar, ataenda night club n.k. Lakini nyanda za juu hizo night clubs na vitu vingine kama hivyo hawavifagilii sana. LAKINI PIA WANAOPATA PESA KIRAHISI NA KILAGHAI HUWA NA MATUMIZI YA ANASA KWA SABABU HAWANA UCHUNGU NA WANAJUA WATAPATA TENA KESHO.

Usiwaite wale wasiotumia pesa kama wewe utakavyo, washamba, kwa sababu hawatumii pesa kama utakavyo wewe au hawapendi upendacho wewe.

Kama upo kazini hebu jaribu kulinganisha mf. kati ya mwajiriwa mchaga na mkinga ni nani ana matumizi makubwa ya pesa. Kama unakopesha pesa makazini, jiulize ni kabila gani wanakopa sana kwako kati ya mchaga na mkinga. Wale wasiokopa sana huwa wanahifadhi pesa.

Mwanzisha thread ni aina ya watu walioko hata kijijini kwetu. Wengine wakiona mazao ya shamba lako limestawili baada ya kulipa huduma stahili huanza kusema unaiba mazao ya mashamba ya jirani kichawi.

Acheni ushamba huo.
 
Mbona mimi tajiri hapa Iringa na wala sio mchawi?...tatizo lenu watu wa kaskazini hela zenu nyingi hamjazitolea jasho ni hela za dhulma na madawa ya kulevya.
 
Sijui lakini kusini ...lakini alichoongea kuhusu Kaskazini ni kweli ....huitwi Tajiri ..hadi Jamii inayokuzunguka uipe chakula cha Maana hapo ndio watatamka kwa kauli " SASA wewe ni Tajiri " .....

Na hata Huo utajiri una levels;

TAJIRI WA "KAWAIDA" .. au Ana Ela..
TAJIRI
KIFARU
MELI......YAANI Hawa ni wale ambao wana jeuri ya kila anapooonekana Kijijini ...kila Siku anachinja Ngombe hadi Siku atakayoondoka.....hawanunui bia kwa Kreti Bali LORI inaitwa.

Na pia kuna kuheshimiana ...Mfano ukikaaa na mtu MELI ..popote hutakiwi kulipia chochote hadi yeye aondoke ....Maana utakuwa unamdhalilisha...,Tena akikuta mmekaa atachukua bill zote atalipa .....AKIONDOKA anayefuatia kwa pesa ndio anabaki...hadi mwisho ...

Kuna jukumu la WAPAMBE hawa ..kazi Yao ni Kumsifia TAJIRI alioko mezani ....na mliobaki wenye pesa za KAWAIDA na wengine.......mnasikiliza na kujifunza Huku nanyi mkisifia kwa staha....

AKIONDOKA WAPAMBE wako wepesi kuhama Kusifia anayefuatia .."utasikia lakini Mangi na wewe una pesa ..sema basi tu jamaa kakuzidi kidogo tu...."

SASA tofauti ni kuwa WAPAMBE nao sio Kama wa mjini nao wanapesa za change ...na kuachiwa magari used wazungukie...na offcourse shida Ndogo Ndogo Kama Ada za watoto wanasaidiwa ..pia ...kwa kuwa wanaijuwa kazi Yao kweli kweli .....wanaweza kujua Mali za matajiri wote mjini na wanna habari zote kuliko TRA au usalama wa TAIFA ..hayo ndio Maisha ya Kaskazini.

Yanayopagawisha vijana kutafuta na wakiripoti mjini tu cha kwanza ni kupita Vijiweni kwa WAPAMBE Ili Kama alikuwa kwenye list ya MAFALA aoshe nyota angalau na yeye wamuandike kwenye list ya wenye Ela ya KAWAIDA..

Utawasikia ..."mnamkumbuka Yule fala alikuwa nyoka.......karudi na yeye Siku hizi anayo ELA "
Ha haha ha mkuu umenifurahisha sana kwa hii post nimefeel kabisa kuwa niko maeneo ya home....sina shaka wewe ni hommie kwa hii post.
 
Mkuu isupilo ndio ukweli wenyewe huo
mm mwenyewe kijana wa kusini, huo ndo ukweli, matajiri wa kusini yaan ukisikia flan ana pesa basi fuatilia nyuma yake anavyotesa wenzake kwa ushirikina, kesharoga wafanyakazi wao, ndugu wa karibu yaani full kafara na yeye mwenyewe pia anaishi maisha ambayo hayafanani na pesake. wako matycoon wa biashara za mbao ndo wanaroga wafanyakazi wao wanakufa katika incidence za utata...,mara kabanwa na gogo mara kaangukiwa na mti. Kazi ujitume na kutumia ujinyime huku unanyanyasa wenzako kwa ushirikina. About mbifile swe
 
mm mwenyewe kijana wa kusini, huo ndo ukweli, ***** zao matajiri wa kusini, yaan ukisikia flan ana pesa basi fuatilia nyuma yake anavyotesa wenzake kwa ushirikina, kesharoga wafanyakazi wao, ndugu wa karibu yaani full kafara na yeye mwenyewe pia anaishi maisha ambayo hayafanani na pesake. wako matycoon wa biashara za mbao ndo wanaroga wafanyakazi wao wanakufa katika incidence za utata...,mara kabanwa na gogo mara kaangukiwa na mti. Kazi ujitume na kutumia ujinyime huku unanyanyasa wenzako kwa ushirikina. About mbifile swe
Una tofauti gani na wale wavivu kijijini wanaoacha mashamba yao bila huduma, lakini wenzao mazao yao yakistawi huwakamata uchawi? Acha imani za kichawi. Utakufa na umaskini wako.
 
Wakinga hawana tofauti na wamakonde unakuta jitu lina hela,halafu linalala chini,havai viatu,kutwa anashindia kuvaa msuli,msosi anaokula sasa duuh...utajiri wa kiboya.


Mkinga na Mmakondeko wako tofauti sana ila kwenye imani za kishirikina kidogo wanashaibiriana, ila kwenye kushindia maandazi ni wakinga kwa sana. Mmakonde hana hiyo tabia pia toka kitambo mmakonde anavaa vizuri.
 
Utajiri wa wa kulala chini, kujisaidia choo kimoja tu yaani kama umebanwa na haja lazima urudi nyumbani ukajisaidie ni utajiri wa mateso........kuna mwingine ukiingia dukani kwake anakuona upo kama uvyozaliwa.......Wakinga watu wa ajabu sana..!!
 
Mbona mimi tajiri hapa Iringa na wala sio mchawi?...tatizo lenu watu wa kaskazini hela zenu nyingi hamjazitolea jasho ni hela za dhulma na madawa ya kulevya.
Wilitula wibita kwiii...Veve kweli umuhavi,wilutila na ndilye kiki
 
Usijidanganye, hata kaskazini hayo mambo yapo, ila sema kusini wamezidi mno. Mimi ni wa kaskazini na nimeshawahi kufanya kazi hapo USA River. Kipindi hicho ndo naanza kazi mara baada ya kumaliza chuo ilikuwa miaka ya 2006. Nikapanga nyumba moja hapo, tuko wapangaji saba. Sasa wakati huo sina hata TV nikawa ikifika saa mbili naenda kuangalia TV kwa nyumba ya jirani ambapo anakaa jamaa yangu bachela hajaoa bado. Alikuwa anafanya biashara ya kuuza vitu vidogo vidogo tuu pale stendi ya Usa River, vitu kama sigara, biscuti, popcorn, big G etc. Hana hata kibanda, anaenda tuu na malboro yake, akifika anavipanga juu ya box, anawauzia abiria.

Sasa kila anaporudi anamwaga hela zake mezani anaanza kuhesabu na kuzipanga za elf kumi, elf tano, mbili, moja, mia tano na silver. Huwezi amini jamaa alikuwa anafunga siku kwa mauzo ya laki 2 hadi 3. Sasa kipindi flani tukacheleweshewa mishahara hadi tarehe 10, nikawa sina hata senti mfukoni. Nikamcheki jamaa aniazime elf 5 tuu, kwa miadi ya kurudisha in 2 days, huwezi amini jamaa alinichomolea. Nikamfuata hadi stendi pale anapouza, akanionea huruma akanishika mkono akaniita pembeni akaniambia ukweli kuwa hii kazi ina masharti na nikivuja tuu biashara inakwisha. Sasa kunisaidia, akaenda kwa jamaa yake ndo akaniazimia kwa yule jamaa, akaja kunipatia. Tangu siku ile nikajifunza kitu.
 
Back
Top Bottom