sifa (nm): uzuri au ubaya wa kitu/mtu. Kwa mfano, mgombea hutakiwa kueleza sifa zake, na watu wakamhukumu kwa tabia yake
tabia (nm): mazowea (mazuri au mabaya) yanayotokana na kurudiarudia hali, mwendendo au matendo. Mfano, udaku, undumilakuwili, ukarimu, kulamba vidole wakati wa kula ni tabia.
Tafauti nyengine ni kuwa kisarufi kutokana na neno sifa tunaweza kupata tendo la kusifu, kusifika, kusifiwa lakini neno tabia haliwezi kunyambulika zaidi.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.