Tofauti kubwa ya dhamira baina viongozi wa Yanga na Simba ni hii hapa

kasenene

JF-Expert Member
Jun 6, 2008
1,632
2,413
Ni kweli timu zote mbili kwa hivi sasa zinaendeshwa na wawekezaji wenye malengo binafsi zaidi tofauti na hapo awali walipokuwa pembeni wakisaidia kama wafadhili. Lakini ukifanya tathimini zaidi utagundua kuwa timu hizi mbili ambazo ni kubwa hapa nchini zina malengo tofauti kwa sasa katika uendeshaji wake;-

  • Wakati viongozi Simba wanawekeza zaidi katika kujenga Club ya mafanikio uwanjani. Viongozi wa Yanga akili yao ipo katika kutengeneza pesa zaidi kwa sasa kwa kujitangaza kupitia rasilimali za Club kadiri zinapokuwepo kama "'Jersey'' n.k
  • Wakati Simba wanafikiria kuboresha utawala mzima wa Club ili kuweza kufikia malengo ya kuwa na Club kubwa na bora zaidi ya mpira wa miguu pamoja na michezo mingine huko mbeleni. Wenzao wa Yanga wanahangaika kuhakikisha kuwa kila anayeingia Yanga awe mchezaji au kiongozi lengo liwe ni kutengeneza pesa ya haraka haraka kupitia mauzo ya ''merchandise'' za club kama jersey kwa lengo la kurudisha pesa ya wawekezaji upesi.
  • Wakati Simba wakisajili wachezaji kwa lengo la kuimarisha timu zaidi mbeleni wenzao wa Yanga wameangalia zaidi wachezaji wanaoweza kuwaletea mafanikio ya haraka haraka kwa sasa ili kutengeneza pesa upesi upesi. .
  • Wakati wanachama na wapenzi wa SIMBA wamekuwa makini katika kufuatilia na kuhoji nini kinachofanyika ndani ya Club ili kuweza kufikia malengo upande wa pili yaani Yanga, wao wapo kimya na hii kwao sio agenda.
  • Wakati Simba wakiwaza kubeba kombe la Club Bingwa Africa na kuwa kati ya timu tano (5) bora za Africa muda woote. Wenzao wa Yanga wanawaza kuwafunga Simba na kutwaa ubingwa wa Tanzania
 
Thithi tuna watu

E9nS1wpXIAAr4GH.jpeg
 
Mbumbumbu fc wanajifariji katika kipindi kigumu wanachopitia! Kwa bahati mbaya huyo Haji Manara mwenyewe mnaye mlilia, ametugawa mashabiki na pia viongozi!

Wapo wanao mkubali, huku sisi wengine tukimuona kama mbumbumbi tu aliyepotea njia.

IMG_4503.jpg
 
Mbumbumbu fc wanajifariji katika kipindi kigumu wanachopitia! Kwa bahati mbaya huyo Haji Manara mwenyewe mnaye mlilia, ametugawa mashabiki na pia viongozi!

Wapo wanao mkubali, huku sisi wengine tukimuona kama mbumbumbi tu aliyepotea njia.
Manara hakuacha kazi Simba bali alifukuzwa na Bodi ya Wakurugenzi fahamu hilo kwanza. So alikuwa na uhuru wa kwenda popote.
FB_IMG_1629890928001.jpg
 
Mbumbumbu fc wanajifariji katika kipindi kigumu wanachopitia! Kwa bahati mbaya huyo Haji Manara mwenyewe mnaye mlilia, ametugawa mashabiki na pia viongozi!

Wapo wanao mkubali, huku sisi wengine tukimuona kama mbumbumbi tu aliyepotea njia.
Nini sasa mtani,embu acha izo shikamaneni na club yenu muwe kitu kimoja ili tukiwapiga msiseme amkuwa pamoja.
 
Unachekesha sana mtopolo...yaani muuza mechi za Simba amefukuzwa unadhani kuna mtu wa Simba anaumia?

Kwanza jua tumefurahi sana kwa kuwa sasa hamna pa kutokea na mlizoea kumtumia huyu jamaa arubuni wachezaji.

Safari hii tunaingia kila mechi tukiwa na amani kama vile ilivyokuwa Kigoma
Mbumbumbu fc wanajifariji katika kipindi kigumu wanachopitia! Kwa bahati mbaya huyo Haji Manara mwenyewe mnaye mlilia, ametugawa mashabiki na pia viongozi!

Wapo wanao mkubali, huku sisi wengine tukimuona kama mbumbumbi tu aliyepotea njia.
 
Aipiti lisaa bila mikia kuanzisha thread,manara na gsm wamejua kuwavuruga mikia
Ni kweli timu zote mbili kwa hivi sasa zinaendeshwa na wawekezaji wenye malengo binafsi zaidi tofauti na hapo awali walipokuwa pembeni wakisaidia kama wafadhili. Lakini ukifanya tathimini zaidi utagundua kuwa timu hizi mbili ambazo ni kubwa hapa nchini zina malengo tofauti kwa sasa katika uendeshaji wake;-

  • Wakati viongozi Simba wanawekeza zaidi katika kujenga Club ya mafanikio uwanjani. Viongozi wa Yanga akili yao ipo katika kutengeneza pesa zaidi kwa sasa kwa kujitangaza kupitia rasilimali za Club kadiri zinapokuwepo kama "'Jersey'' n.k
  • Wakati Simba wanafikiria kuboresha utawala mzima wa Club ili kuweza kufikia malengo ya kuwa na Club kubwa na bora zaidi ya mpira wa miguu pamoja na michezo mingine huko mbeleni. Wenzao wa Yanga wanahangaika kuhakikisha kuwa kila anayeingia Yanga awe mchezaji au kiongozi lengo liwe ni kutengeneza pesa ya haraka haraka kupitia mauzo ya ''merchandise'' za club kama jersey kwa lengo la kurudisha pesa ya wawekezaji upesi.
  • Wakati Simba wakisajili wachezaji kwa lengo la kuimarisha timu zaidi mbeleni wenzao wa Yanga wameangalia zaidi wachezaji wanaoweza kuwaletea mafanikio ya haraka haraka kwa sasa ili kutengeneza pesa upesi upesi. .
  • Wakati wanachama na wapenzi wa SIMBA wamekuwa makini katika kufuatilia na kuhoji nini kinachofanyika ndani ya Club ili kuweza kufikia malengo upande wa pili yaani Yanga, wao wapo kimya na hii kwao sio agenda.
  • Wakati Simba wakiwaza kubeba kombe la Club Bingwa Africa na kuwa kati ya timu tano (5) bora za Africa muda woote. Wenzao wa Yanga wanawaza kuwafunga Simba na kutwaa ubingwa wa Tanzania
 
Mbumbumbu fc wanaumia sana, timu imeuza wachezaji wa maana imenunua wachezaji wa mafungu eti inakuza vipaji, umewahi sikka wapi duniani timu inayo gombania makombe ikawa kituo cha kulea vipaji.
Ayo mambo wanaweza Arsenal tu. Timu kubwa inanunua wachezaji wakubwa walio pevuka na kuongeza vijana chache.
 
Mbumbumbu fc wanaumia sana, timu imeuza wachezaji wa maana imenunua wachezaji wa mafungu eti inakuza vipaji, umewahi sikka wapi duniani timu inayo gombania makombe ikawa kituo cha kulea vipaji.
Ayo mambo wanaweza Arsenal tu. Timu kubwa inanunua wachezaji wakubwa walio pevuka na kuongeza vijana chache.
acha ushabiki zaidi utakuja kutubu mwisho wa ligi mwaka huu.
 
Back
Top Bottom