Kuna tofauti gani kati ya Hayati na Marehemu?

Hayati na marehemu ni sawa tu. Inategemeana anayeitwa ana nyazifa gani
 
Hayati ni mtu aliyekufa akiwa na cheo cha juu sehemu flani na marehemu ndiyo hivyo kawaida yani .
 
nimetoka kumuuliza google transilate
marehem kasema kwa kizungu ni late

kwahiyo baba wa taifa ni late JKN sijua kwanini tumuite hayati na asiitwe marehemu..

kwa neno hayati google transilate bado anatafuta majibu....
Hayati ni neno la kiarabu manaake ni maisha/life. Inawezekana tumeliokota kutoka huko na kulitumia ndo mana hata Google translate inapata wakati mgumu kulitafsiri. nafikiri neno sahihi ni marehemu.
 
Marehemu ni mtu yeyote aliyekufa kufa tu na hayati ni mtu aliyekufa huku ameacha legacy nzuri kwa jamii yake!
Kufa n Kufa tu hata ufe ukiwa Rais wa Dunia umekufa tu ukiitwa hayati haikupi tiketi ya kuiona pepo
 
Kwa muda mrefu sana nilikua nikisikia toka kwa ndugu na watu wengine wakimuita merehemu mtu alie kufa siku nyingi zilizopita.

Hivo ilinijengea mimi pia mazoea ya kumuita marehemu, mtu alie kufa mda mrefu.

Pia nimekuwa nikisikia katika vyombo vya habari wakimuita hayati mtu ambae amekufa muda mrefu lakini akiwa na cheo fulani.

Kwa hivo katika fikra zangu zimeweza kufikiri kuwa huenda kuna makundi mawili ambalo kundi la kwanza ni la wale wasio na cheo chochote katika taifa ndio huitwa marehemu lakini pia kundi la pili ni la wale wenye vyeo katika taifa ndio huitwa hayati, sina uhakika na fikra zangu.

Kwahivo nimeona ni bora niilete huku mada ili niweze kupata uhakika wa tofauti kati ya marehemu na hayati.

JamiiForums great thinker.
Hayati ni mfu aliyekuwa na pesa, lakini marehemu ni mfu chokambaya.
Chezea pesa wewe.
 
hayati-kwa mtu aliyekuwa maarufu
marehemu-kwa mtu wa wakawaida tu asiyekuwa na umaarufu
 
Kama umeacha benki zaidi ya milioni mia wewe utaitwa HAYATI
Kama umeacha madeni utaitwa mdaiwa sugu mfu
Kama uliacha milioni mia kurudi chini utaitwa Marehemu
 
Back
Top Bottom