Zurie
JF-Expert Member
- Jul 6, 2014
- 1,743
- 4,270
Leo ni maadhimisho ya siku ya kimataifa ya viumbe hai wa porini na majini ambayo huadhimishwa kila mwaka mnamo Machi 3 ili kueneza uelewa wa mimea na wanyama mwituni
Mwaka huu, siku hii imefanywa mahususi ya kueneza uelewa kuhusu viumbe hai wa majini na umuhimu wao kwa maendeleo ili kuhakikisha wanatunzwa kwa ajili ya vizazi vijavyo.
Tanzania imebarikiwa kuwa na viumbehai lukuki walio nchi kavu na majini. Wanyamapori walio katika mbuga mbalimbali wamekuwa vivutio kwa watalii na kuleta ukuaji wa pato la taifa.
Mwaka 2018, hifadhi ya wanyamapori ya Serengeti iliibuka kuwa bora kuliko zote Afrika ikiipita Mala Mala ya Afrika Kusini na Mana Pools ya Zimbabwe katika utafiti uliofanywa na kampuni ya utalii ya Safari Bookings.
Mwaka huu, siku hii imefanywa mahususi ya kueneza uelewa kuhusu viumbe hai wa majini na umuhimu wao kwa maendeleo ili kuhakikisha wanatunzwa kwa ajili ya vizazi vijavyo.
Tanzania imebarikiwa kuwa na viumbehai lukuki walio nchi kavu na majini. Wanyamapori walio katika mbuga mbalimbali wamekuwa vivutio kwa watalii na kuleta ukuaji wa pato la taifa.
Mwaka 2018, hifadhi ya wanyamapori ya Serengeti iliibuka kuwa bora kuliko zote Afrika ikiipita Mala Mala ya Afrika Kusini na Mana Pools ya Zimbabwe katika utafiti uliofanywa na kampuni ya utalii ya Safari Bookings.