TMK Family na amka kijana

Lutala

JF-Expert Member
Jun 17, 2010
848
103
KUNDI la muziki wa kizazi kipya la TMK Wanaume Family la Temeke Dar es Salaam, limewataka wapenzi wake kujitokeza kwa wingi katika tamasha la Amka Kijana litakalofanyika Jumamosi hii, kwenye dimba la Uhuru jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jijini jana, Meneja wa kundi hilo Said Fella, alisema kuwa kundi hilo linatarajia kutambulisha mitindo yao mipya ya uchezaji ambayo wanaamini itawakuna wapenzi na mashabiki wao.

Fella alisema kuwa wanaamini hiki ni kipindi kizuri kwa mashabiki wao, kuipata burudani ya uhakika kutoka kwao baada ya kuikosa kwa muda mrefu.

Alisema bendi hiyo iliahirisha maonyesho yake katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramdhan na baadaye ikabidi wapishe maandalizi ya uchaguzi mkuu.

“Mkubwa TMK Wanaume Family, tunapenda kuwaambia wapenzi na mashabiki wetu waje kwa wingi katika tamasha la Amka Kijana litakalofanyika Jumamosi hii kwenye Uwanja wa Uhuru, watapata vitu vingi ikiwemo mitindo mipya,” alisema Fella.

Tamasha hilo litakalopambwa na burudani za kila aina, litahitimishwa kwa mechi ya kukata na shoka kati ya mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara, Simba, dhidi ya Azam FC.
 
Hakuna cha chawa wala kiroboto - TMK Family chini ya Fella ni kiboko mbaya
 
Hakuna cha chawa wala kiroboto - TMK Family chini ya Fella ni kiboko mbaya

hivi hawa ndio wale wavuta bangi waliokuwa wanapambua jukwaa la CCMm wakati wa kampeni? kamandio wenyewe nianze kuwashushia kibano sasa hivii.....
 
hivi hawa ndio wale wavuta bangi waliokuwa wanapambua jukwaa la CCMm wakati wa kampeni? kamandio wenyewe nianze kuwashushia kibano sasa hivii.....

Ndo wenyewe hao kaka jawana mpango sasa hii amka kijana sijui kama wao kwanza wameshaamka ...:A S angry:
 
Hakuna cha chawa wala kiroboto - TMK Family chini ya Fella ni kiboko mbaya

kwanza nianze na wewe Lutalatala ( sijui ludaladala) ebu tueleze maslahi yako kwenye hilo tamasha au huyo Saida Fela anakulipa shillingi ngapi au anakupa nini? adi uje ututangazie huoo upuunzi wa hao wavuta bangi wanaojificha chini ya koti la CCMm, nijuavyo mimi kule TMK huyu jamaa bonge nyanya wanamsema si riski, ebu tueleze vizurii

Apa umekosea chaka peleka hilo tangazo kwa mkweree na familia yake
 
kwanza nianze na wewe Lutalatala ( sijui ludaladala) ebu tueleze maslahi yako kwenye hilo tamasha au huyo Saida Fela anakulipa shillingi ngapi au anakupa nini? adi uje ututangazie huoo upuunzi wa hao wavuta bangi wanaojificha chini ya koti la CCMm, nijuavyo mimi kule TMK huyu jamaa bonge nyanya wanamsema si riski, ebu tueleze vizurii

Apa umekosea chaka peleka hilo tangazo kwa mkweree na familia yake

Ebu punguza mukrali kidogoo..Ni kweli hawa madogo chini ya huyo boss walitupiga sana vijembe chadema lakini tuwasamehe inawezekana hawa madogo walikuwa hajui nini wana tenda jukumuu letu kwa sasa ni kuwaelimisha na kuwarudisha kundinii
 
Ebu punguza mukrali kidogoo..Ni kweli hawa madogo chini ya huyo boss walitupiga sana vijembe chadema lakini tuwasamehe inawezekana hawa madogo walikuwa hajui nini wana tenda jukumuu letu kwa sasa ni kuwaelimisha na kuwarudisha kundinii

Weee ishia apo apo, unatakiwa kumfundisha mtoto mtukutu kwa kumchalaza bakora (japo mbili tatuu hivii) ili siku nyingine asirudie
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom