Lutala
JF-Expert Member
- Jun 17, 2010
- 848
- 103
KUNDI la muziki wa kizazi kipya la TMK Wanaume Family la Temeke Dar es Salaam, limewataka wapenzi wake kujitokeza kwa wingi katika tamasha la Amka Kijana litakalofanyika Jumamosi hii, kwenye dimba la Uhuru jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jijini jana, Meneja wa kundi hilo Said Fella, alisema kuwa kundi hilo linatarajia kutambulisha mitindo yao mipya ya uchezaji ambayo wanaamini itawakuna wapenzi na mashabiki wao.
Fella alisema kuwa wanaamini hiki ni kipindi kizuri kwa mashabiki wao, kuipata burudani ya uhakika kutoka kwao baada ya kuikosa kwa muda mrefu.
Alisema bendi hiyo iliahirisha maonyesho yake katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramdhan na baadaye ikabidi wapishe maandalizi ya uchaguzi mkuu.
Mkubwa TMK Wanaume Family, tunapenda kuwaambia wapenzi na mashabiki wetu waje kwa wingi katika tamasha la Amka Kijana litakalofanyika Jumamosi hii kwenye Uwanja wa Uhuru, watapata vitu vingi ikiwemo mitindo mipya, alisema Fella.
Tamasha hilo litakalopambwa na burudani za kila aina, litahitimishwa kwa mechi ya kukata na shoka kati ya mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara, Simba, dhidi ya Azam FC.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jijini jana, Meneja wa kundi hilo Said Fella, alisema kuwa kundi hilo linatarajia kutambulisha mitindo yao mipya ya uchezaji ambayo wanaamini itawakuna wapenzi na mashabiki wao.
Fella alisema kuwa wanaamini hiki ni kipindi kizuri kwa mashabiki wao, kuipata burudani ya uhakika kutoka kwao baada ya kuikosa kwa muda mrefu.
Alisema bendi hiyo iliahirisha maonyesho yake katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramdhan na baadaye ikabidi wapishe maandalizi ya uchaguzi mkuu.
Mkubwa TMK Wanaume Family, tunapenda kuwaambia wapenzi na mashabiki wetu waje kwa wingi katika tamasha la Amka Kijana litakalofanyika Jumamosi hii kwenye Uwanja wa Uhuru, watapata vitu vingi ikiwemo mitindo mipya, alisema Fella.
Tamasha hilo litakalopambwa na burudani za kila aina, litahitimishwa kwa mechi ya kukata na shoka kati ya mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara, Simba, dhidi ya Azam FC.