beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) imetoa angalizo kwa mikoa ambayo itanyesha mvua kubwa leo ikiwemo Singida, Rukwa, Mbeya, Njombe, Songwe na Iringa.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa kesho Januari 11, 2019 kutakuwa na angalizo la mvua kubwa kwa baadhi ya maeneo ya mikoa ya Singida, Dodoma, Rukwa, Mbeya, Songwe, Iringa na Njombe.
“Januari 12 na 13 hakuna taathari wananchi wanatakiwa kuzingatia angalizo la mvua hizo ili wasipate madhara,”taarifa ya TMA.
TMA imeeleza kiwango cha athari kinachoweza kutokea ni baadhi ya makazi kuzungukwa na maji, ucheleweshaji wa usafiri, kusimama kwa muda kwa baadhi ya shughuli za kiuchumi na kijamii