Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,064
- 22,757
Mwanasiasa mkongwe, kada na Waziri Mkuu Mstaafu John Malecela, jana alikuwa kivutio kwenye kikao hicho cha CC baada ya kuonekana akisamiliana na wajumbe wengi ambao walimtakia pole ya homa. Juzi, mkongwe huyo katika medani ya siasa, aliingia ukumbini akiwa ameongozana na Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete huku akionekana mwenye afya njema. Aliingia na kwenda moja kwa moja kukaa karibu na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, John Chiligati.
Yawezekana tinga tinga lililetwa makusudi kuipiga tafu CC ya CCM chini ya uenyekiti wa JK baada ya kushindwa kuukwaa mlima wa maamuzi mazito ya kuvua/kuvuliwa gamba ambayo yamekuwa yakihubiriwa na jeshi la kukodi kutoka CCJ. Lakini mambo hayakwenda hivyo !
Kama ilivyopangwa Tinga tinga mwenyewe ndiye aliyekuwa wa kwanza kurusha kombora la kukitaka kikao kiwatose watuhumiwa (?) wa Ufisadi. La haula ! Ukumbi ukawa kama vile umemwagiwa maji baridi na hakujitokeza hata moja miongoni mwa wajumbe kuunga mkono hoja hiyo.
Kama ilivyo desturi yake siku zote Mkuu wa dataz kwa kujua mission ya Dingi wake lakini bila kutafakari athari kwa tinga tinga iliyokosa dizeli kujaribu kuukwaa mlima likikokota zigo la Chama cha Magamba haraka haraka akakimbilia JF !
Na kama hili lingetokea, leo tungeshuhudia mengi kwani nyota zilizoanza kufifia, zingetupofusha tulio wengi kwa mwanga wake mkali.- According to the datas, Chenge ameachia ngazi rasmi leo ndani ya CC inayoendelea sasa hivi Dodoma!
Willie @ NYC, USA.