mundele
Member
- Jun 5, 2009
- 45
- 1
Nimejaribu kuisoma na kuichanganua timu yetu ya taifa na kujiuliza je? nini chanzo cha kutofanya vizuri katika michezo ya kimataifa? je? inawezekana kwamba ni tatizo la kocha kama wengi wetu tunavyofikiria? au ni urasimu uliopo kwenye vyama vyetu vya michezo nchini??? lakini nimegundua kwamba Tanzania ina wachezaji zaidi ya 10 wanaocheza mpira wa kimataifa katika mataifa mbalimbali ulimwenguni na wengiwao kwenye Super league za mataifa hayo...Nafikiri labda tungewatumia hao wachezaji wetu wa nje labda wangekuja na technics mbalimbali za kimpira walizozipata kutoka huko kwenye vilabu vyao kuliko kungangania suala la kocha ambalo linaonekana ni ndiyo tatizo kwa sasa...Huo ni mtazamo wangu tu wadau, Kazi kwenu.....