figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,890
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga amekutana na muwakilishi wa Sports Pesa Tanzania,Luca Neghesti kumpa taarifa Waziri huyo kuhusu maandalizi ya kuileta timu ya Everton inayoshiriki ligi kuu ya Uingereza kwa ajili ya kucheza mechi za kirafiki hapa nchini.
Waziri huyo pia amekutana na wawakilishi wa timu hiyo ofisi kwake jijini Dar es salaam kwaajili ya ziara hiyo hapa nchini.
Aidha Waziri Mahiga amesema ziara hiyo itasaidia kuitangaza Tanzania duniani pamoja na kuhamasisha mchezo wa mpira wa miguu kwa vijana wa Kitanzania.