Time travel na ufunuo wa ufufuko

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,633
697,597
Tuifahamu time travel ninini kwanza (si lazima iwe sawa na ile unaifahamu wewe) .... Ni sawa na kurudisha muda nyuma na kuleta uhalisia wa jambo lililipita ulifanye tena ama kupeleka muda mbele na kufika ambako wengine hawajafika bado... Yaani uifike kesho kupitia muda kabla kesho yenyewe haijafika.... Kitabu cha A girl from tomorrow kinaweza kukupa mwanga zaidi kwenye hili....

Nina hisia zinazonipa uhalisia mwingi sana katika siri ambazo bado hazijafunuliwa... Uhalisia wa uhai na maisha tena baada ya kifo.. Baada ya roho kutengana na mwili.. Kuna muunganiko unaweza kuja kutokea tena katika uhalisia wake na hapa ndio ile dhana ya time travel inaweza kuwa halisi

Kuna chords za siri bado hatujazipatia... Siri iliyojificha nyuma ya kifo na maisha baada ya Kifo na ufufuko mpya kutoka kifoni... Kwanini nawaza haya? Uhalisia ni upi? Je ni mauzauza tu ama kuna mwanga wa ukweli uliofichama!? Hebu twende kipengele kwa kipengele kuanzia kiimani mpaka nje ya imani na utata wake...

Asili ya binadamu ni Afrika... Hili halijawahi kukanushwa popote... Na tunaambiwa aliishi miaka million nyingi... Asili ya dunia ni mashariki ya kati kiimani na kidini... Misahafu karibia yote na madokezo ya kidini yanazungumzia uumbaji wa dunia kwenye ulimwengu wa kiimani kama chanzo na asili yake ni mashariki ya kati.. Hapo ndio penye chimbuko... Lakini umri ukitofautiana kutoka imani moja mpaka nyingine... Kwenye mada hii nitabaki upande wa asili ya mwanadamu na si asili ya dunia....

Kuna dondoo zisizopungua tano, zinazotoa fununu juu ya maisha baada ya kifo na ufufuko ama uhai tena... Hebu tupitie moja baada ya nyingine

1. KIDINI (Imani katika Mungu mmoja)
Zipo dini hasa ukristo na uislam.. Zinaamini katika ufufuko mara baada ya kifo lakini ufufuko huo haufanyiki sasa hivi bali kuna siku inayoitwa mwisho wa dunia ama siku ya kiama... Ndio wafu wote watafufuliwa... Kumbuka hawafufuki wenyewe WATAFUFULIWA...

2. KIDINI(katika imani ya miungu)
Zipo dini zisizoamini katika Mungu mmoja bali miungu... Yaani mungu jua, mungu miti, mungu mwezi, mungu moto nknk.. Hawa wanaamini ya kwamba binadamu anapokoma kuwa hufa na kuzaliwa tena mahali pengine kwa sura na hata umbo lingine... Na wapo watu wanatoa na shuhuda kabisa kwenye hili....

3. WAFANYA TAHAJUDI
Hawa huingia kwenye kundi la kile kipengele cha kufungua jicho la tatu... Uwezo wa kufungua jicho la tatu.. Kuona yajayo, kubashiri na hata uwezo wa kubadili mambo kadhaa yajayo kabla ya kuyafikia... Hawa nao huamini katika reincarnation... Pitia Liao fans four lessons

4.WATABIRI na WAPIGA RAMLI...
Ni watu wenye kipawa cha asili ama kipawa wezeshi kwa kutumia nguvu za ziada wanaoweza kukisoma na kukutabiria mambo yako yajayo kabla hujayafika na hata yaliyopita pia! Dhana ya time travel!? Kuna wabahatishaji lakini pia kuna wenye hakika hasa kupitia na kutumia alama za viganja, tarehe muda na nyota...

5. WAOTA NDOTO (NDOTO MAONO)
Hapa kuna watu huota na kitu kikatokea kama kilivyo... Tunafahamu kuna ndoto nyingi lakini ndoto maono hutoa uhalisia wa ajabu kabisa... Je hizi nazo ni sehemu ya time travel!? Baadhi ya ndoto huhusisha jumbe toka kwa marehemu kama vile wako hai mahali fulani na wanatoa maagizo kabisa......

Kwa kuzingatia dondoo tajwa hapo juu kuna uhalisia mwingi kwamba kuna siri za hii dunia hatujafunuliwa bado na hii inatokana na kujikita zaidi kwenye sayansi na dini za kigeni... Tunafundishwa vitu vyenye limitations nyingi huku pengine wenzetu wakiwa tayari wamesha unlock siri hizi kwa sehemu kubwa. ...

Kama imeshindikana kabisa kuficha kuwa asili ya mwanadamu ni Afrika. Basi huyu mwafrika kabeba siri kubwa kwenye uumbaji na kikomo cha kuwa... Sasa kuko wapi kushindwa kwake?

Sayansi hizi za kiafrika zisizo na ithibati zinatoa mwanga muhimu kwenye hili... Lakini zinatuthibitishia kuwa kuna ulimwengu mwingine usioonekana upo na unaexist
Sayansi ya kupaa kwa ungo bila kuonekana na wengine
Sayansi ya kumuua mtu na kumfanya msukule
Sayansi ya kuingia kwennye nyumba ya mtu bila kufungua milango wala madirisha
Sayansi ya kudhuru kwa kutumia macho tu.. (Zongo nk)
Sayansi ya kutabiri kwa kutumia jivu maji kwenye beseni ama mchanga....

Kuna ulimwengu usioonekana upo
Kuna mahali wafu wapo wanaendelea na maisha na kuna siku watarejerea kwenye miili yao
Dhana ya recycle bin inatoa mwanga kwenye hili... Waafrika kuna maarifa tulipokwa.. Turudi kwetu tuanze upya.. Tutaushangaza ulimwengu
.
 
Kupatwa Kwa time travel!!!!!!!!
Hizi sayansi za kilozi na dini zinaelezeaje dhana ya muda...?
Kwasababu ili ujue kitu lzm ukifahamu kiundani.
Na ili uelewe time travel ni lazima uelewe space inakanuni zipi (the nature of space). Ktk dhana zako ulizoeleza hapo time travel hasa Kwa kurudi nyuma inawezekana kivipi..? (itakuwa vyema ukijibu kwa kina ukizingatia space).
 
Kupatwa Kwa time travel!!!!!!!!
Hizi sayansi za kilozi na dini zinaelezeaje dhana ya muda...?
Kwasababu ili ujue kitu lzm ukifahamu kiundani.
Na ili uelewe time travel ni lazima uelewe space inakanuni zipi (the nature of space). Ktk dhana zako ulizoeleza hapo time travel hasa Kwa kurudi nyuma inawezekana kivipi..? (itakuwa vyema ukijibu kwa kina ukizingatia space).
Nimetumia time travel kwa maono yangu na ufahanu wangu na sio hiyo uliyojifunza kwa mzungu...
Kwahiyo kwa muktadha wa mada yangu bado niko sahihi... Labda unikosoe kwa kutumia maneno ya kiingereza na kuyapa tafsiri tofauti na ilivyozoeleka
 
Nimetumia time travel kwa maono yangu na ufahanu wangu na sio hiyo uliyojifunza kwa mzungu...
Kwahiyo kwa muktadha wa mada yangu bado niko sahihi... Labda unikosoe kwa kutumia maneno ya kiingereza na kuyapa tafsiri tofauti na ilivyozoeleka
he he! Kuna usemi mmoja tu umekosea! Kufunzwa na mzungu!! Na nitanena sentensi moja tu.. sayansi ni mawimbi ya ubongo wa mwanadamu ktk mazingira yake.
 
Nina swali endapo ni nje na mada kwanini mungu na shetani wamekuwa wakijihusisha Sana na matendo ya mwanadamu kwani hakuna vyengine vya kufanya...?
Hapana sio kweli hawajihusishi bali wanahusishwa na shida iliyopo ni kwamba hatuwachori kama nguvu fulani iliyo juu ya uwezo wa kibinadamu bali tunawachora kwenye maumbile na uwezo wa kibinadamu ambao uko so limited
 
.
[/QUOTE]
Ulichoandika ni moja ya mambo ambayo imekuwa kama Taboo kwa baadhi ya watu kulingana na imani zao kujadili lakini lazima kijadiliwe kwa kuwa kipo. Babu yangu alikuwa mwalimu wa dini alikuwa mkufunzi kwenye moja ya vyuo vya kanisa la AIC baada ya kufariki mimi nilijirithisha vitabu vyake kati ya vitabu kimoja kinaitwa THE LIFE AFTER DEATH chapisho la kwanza 1912 kina kurasa chache sana kama 65 lakini yaliyondikwa ndio yalinifikirisha sana ni wazi kuwa suala la mauti NI kama imeamuliwa kutofundishwa kwa waumini kwani yangeleta mkananyikona hivyo pengine kupunguza ufuasi kumbuka mafundisho mengi ya dini nyingi ni kuhusu maisha baada ya kifo..... Kwa mujibu wa kitabu hiki mtu akifa huendelea kuishi ila huwa amebadili form anakuwa kama ilivyo vitu usivoona lakini vipo kama upepo gas na vinginevyo
 

Attachments

  • IMG_20190904_095454.jpg
    IMG_20190904_095454.jpg
    61.3 KB · Views: 59
  • IMG_20190904_095537.jpg
    IMG_20190904_095537.jpg
    97.5 KB · Views: 61
Ulichoandika ni moja ya mambo ambayo imekuwa kama Taboo kwa baadhi ya watu kulingana na imani zao kujadili lakini lazima kijadiliwe kwa kuwa kipo. Babu yangu alikuwa mwalimu wa dini alikuwa mkufunzi kwenye moja ya vyuo vya kanisa la AIC baada ya kufariki mimi nilijirithisha vitabu vyake kati ya vitabu kimoja kinaitwa THE LIFE AFTER DEATH chapisho la kwanza 1912 kina kurasa chache sana kama 65 lakini yaliyondikwa ndio yalinifikirisha sana ni wazi kuwa suala la mauti NI kama imeamuliwa kutofundishwa kwa waumini kwani yangeleta mkananyikona hivyo pengine kupunguza ufuasi kumbuka mafundisho mengi ya dini nyingi ni kuhusu maisha baada ya kifo..... Kwa mujibu wa kitabu hiki mtu akifa huendelea kuishi ila huwa amebadili form anakuwa kama ilivyo vitu usivoona lakini vipo kama upepo gas na vinginevyo[/QUOTE]



hebu ukiweza screen shot baadhi ya pages tafadhali
 
Ulichoandika ni moja ya mambo ambayo imekuwa kama Taboo kwa baadhi ya watu kulingana na imani zao kujadili lakini lazima kijadiliwe kwa kuwa kipo. Babu yangu alikuwa mwalimu wa dini alikuwa mkufunzi kwenye moja ya vyuo vya kanisa la AIC baada ya kufariki mimi nilijirithisha vitabu vyake kati ya vitabu kimoja kinaitwa THE LIFE AFTER DEATH chapisho la kwanza 1912 kina kurasa chache sana kama 65 lakini yaliyondikwa ndio yalinifikirisha sana ni wazi kuwa suala la mauti NI kama imeamuliwa kutofundishwa kwa waumini kwani yangeleta mkananyikona hivyo pengine kupunguza ufuasi kumbuka mafundisho mengi ya dini nyingi ni kuhusu maisha baada ya kifo..... Kwa mujibu wa kitabu hiki mtu akifa huendelea kuishi ila huwa amebadili form anakuwa kama ilivyo vitu usivoona lakini vipo kama upepo gas na vinginevyo

hebu ukiweza screen shot baadhi ya pages tafadhali
[/QUOTE]
hebu jaribu hii kama itashindikana nitaarifu halafu nitafanya utaratibu wa kukiscan nikutengenezee pdf https://books.google.co.tz/books?id...cal publishing committee of harrogate&f=false
 
Back
Top Bottom