Time Travel: Je, linaweza kuwa suluhisho la kifo?

nimevutiwa na maelezo mkuu.

sasa labda wewe kwa unavoelewa ili mtu usafiri uende kwenye past ufanyeje..?

je uwe na spidi kali sana ukitembea huko angani ?

au uwe na spidi kali ukitembea hapa duniani ?

naamini dunia in Mengi sana na hizi tafiti za wanasayansi zinazidi kuniongezea imani yangu juu ya DINI HII YA kiislamu.

maana ninaona kabisa kwamba kuna mambo ya aabu yapo katika uislamu ambayo najiuliza hao waliyoyanukuu walikuwa na ujasiri gani kunukuu ?

ina maana hawakuhofia kwamba watu watahisi ni uongo kama vile mtume muhammad kwenda miiraji n. k

kuna hadithi inasema "katik pepo kuna daraja mia, baina ya daraja na daraja katika hizo daraja mia upishano wake ni baina ya mbingu na ardhi "

mtu anawezakuona hizi ni stori za kutunga lkini hata wanasayansi sasa hivi wanatuambia kwamba hata umbali baina ya nyota moja na nyingine unaweza kufika KM 340000 sasa angalia kuna nyota ngapi huko juu na huo umbali baina ya nyota na nyota ?

pia wanasema watu wa astronomy ya kuwa kuna madudu makubwa huko juu ambayo ukubwa wake basi jua lijirudie siochini ya mara 1000(kwa uchache) ndo linaweza kufanana na hayo madudu.

kiufupi Uislamu umeeleza Mengi sana ambayo wanasayansi ndo wanatafuta sababu zao na kuzielezea hapo.

lakini mimi najikita sana na kufatilia mambo ya astronomy huko nazidi kuamini kwamb Qurani imetoka Kw Mungu.

yani inaonesha ya kuwa dunia ni kijitu kidogo sana katika uislamu.kwa sababu mifano inayppogwa na Mafundisho ya uislamu ni mifano ambayo mtu anaweza kuona ni kujikuza lakini ipo

Kwanza kabisa mimi si sheikh na nipo katika kujifunza,maelezo yako nimeyasoma na nimeyaelewa vyema na nina uhakika kila unachokisema unamaanisha.

Na hapa hakuna kufichana lazima tuwekane wazi ili tufahamiane vizuri.

Mwanzo unakumbuka ulimgusia "Makarim Shirazi" ? Nikakuuliza swali wewe ni SHIA au umeamua kumfatilia huyo sheikh wa Kishia bila kujua ?

Muda huu umetaja suala la Ufalme na Usultani,hapa najua kabisa umemaanisha japokuwa hapakuwa na haja ya wewe kuweka kauli hiyo.

Sababu najua umemaanisha na mimi nakuuliza swali je Usultani na Ufalme ni jambo baya ? Je Uislamu unakataza Ufalme ? Kwanini umeiweka kauli hiyo hapa ? Je kulikuwa na haja ?


Haya unayoyasema yako sahihi na yapo na tunayaona.

Nakupata vizuri. Hivi visa navyovitoa ingekuwa vizuri kama ukiwa unaweka na marejeo,kama unavyonituhumu mimi ya kuwa siweki ushahidi.

Nakupata vizuri.

Uko sahihi kabisa.


Kaka elimu haitaki mja uwe kama sponchi lazima uchuje kipi cha kuchukua na kipi cha kuacha. Kama mwanachuoni mkubwa alipata kuathiriwa na mtu muovu vipi mimi ambae sina elimu,unamjua Imaamu Safarini ? Mwenye kitabu kiitwacho "Aqidat as Safariniyyah" ?

Sasa kama leo hii kuna watu wanaitakidi Jibril alifanya hiyana juu ya kupeleka ujumbe kwa mtume na alipaswa apelekewe Ali,huku ni kuitukana dini ya Uislamu,mtu ambae anasema mama Aisha ni mzinifu wakati Qur'aan imewatakasa wakeze mtume,na mtu ambae anaitakidi ya kuwa Qur'aan haijakamilikana iliyokamilika iko pangoni ? Hivi mtu huyu atakueleza nini katila Dini akawa mkweli ?

Kaka ukisoma katika kitabu cha Mukadima wa Sahihi Muslimu cha Imam Muslim ameelzea maneno ya Imamu Muhammad bin Sirrin akionyesha umuhimu wa kuwajua rijali katika mapokezi ya habari anazo nasibishwa nazo mtume,na hii ni baada ya kudhihiri fitna na akasema ya kuwa kuuliza juu sanadi ndio dini basi tuangalie wapi unachukua dini yako.

Mtume ameondoka ameacha Uislamu ukiwa safi na usiku wake ni sawa na mchana wake. Kaka siwezi kuchukua dini lwa mtu mzushi na muongo kama Jahmiyyah,Ashaira,Mu'tazila ambao wapo karibu sana kiitikadi na MASHIA,Maturudiya na wengineo katika makundi potofu.

Kaka bora wewe unione mimi sina maarifa ila sitaki kuichanganya Itikadi yangu na uchafu.


Kuna muda nilikugusia athari walizokuwa nazo wanazuoni wa dini ya USHIA kutokana na wao kujikita na Falsafa ikawapelekea kukana baadhi ya sifa za Allah.

Nakuuliza swali,hivi Qur'aan ni maneno ya Allah au ni kiumbe ?

Pili,utata uko wapi wakati jambo hili limeshawekwa wazi karne na karne na wanazuoi wa Tafsiri ? Ndio maana nilikuuliza unatumia tafsiri gani ? Sababu nilijua tu kama wewe sio SHIA basi umeathirika na USHIA. Sasa wewe si unasema au unahimiza juu ya utafiti,je ushawahi kusoma Tafsiri za Qur'aan nje ya Tafsiri za Kishia ? Na kama umesoma ni tafsiri zipi umesoma ? na kama hujasoma kwanini mimi unataka niwe huru wakati wewe hauko huru ?

Sasa,nenda kasome Tafsiri ya Imaam Ibn Kathiir iitwayo "Al Qur'aan Adhwiim" katika kuilezea aya hiyo ya pili ya surt ar Raadi,uone je hiyoaya ina utata au utata mnauweka nyinyi ?

Kaka kwanza ulitakiwa ujue ni kwa namna gani wanazuoni walivyopambana kwa idhni ya Allah juu ya kuihudumia Qur'aan na kuweka wazi aya zote zinazohisiwa na watu kwamba zina utata,rejea pia kitabu cha Imaamu Muhammad al Amiin ash Shanwitwiy kiitwacho"Dafu'u Ihami adh Twirab 'an Ayaat al Kitaab" pia rejea kitabu cha Mwanachuoni mkubwa wa Hadithi aitwae Abdul Muhsin al Abaad al Badr kiiteacho "Ayaat mutashabihaat al Alfadh fi Qur'aan al Kariim" na namna ya kuzitofautisha. Ili uone ya kuwa kila kitu kilishawekwa wazi muda mrefu na mnayoyaleta nyinyi ni Talbisat za kuwayumbisja watu kwa makusudi wakati mambo yako wazi na dalili ziko wazi ila hamzifati kwa makusudi.

Ile ya Ysuf Ali sio Tafsir,bali ni tarjama kwa lugha ya kiingereza,tafuta Tafsir za wanazuoni wakubwa ambao wamejea maana ya aya kwa mtume na maswahaba zake. Aya hizo zimewekwa wazi. Na hapo Yusif Ali hajatafsiri bali matini ya aya ndio yanasema hivyo.


Nakuuliza swali rahisi,sasa wewe baada ya kuona aya na ukadai kwamba ina utata,je ni wewe umeliona hilo au wanazuoni wako wameliona hilo ndio wewe ukakariri ?

Je baada ya kuhisi utata huo je ulisoma vitabu vya madhehebu ngapi za Uislamu juu ya aya hiyo na madhehebu hizo zimesema kwamba aya hiyo ina utata au ?

Je kabla ya wanazuoni wako je maimamu gani wa Kishia kati ya wale 12 walisema kwamba aya hiyo ina utata ? Je kama hakuna,wewe na maimamu wa Kishia nani mwenye elimu kubwa ?

Unajua kuna ujinga mwingine huwa mnajitakia tu,muonekane mnajua kuhoji wakati mnapotea,rudini katika asili kila kitu kipo.

Sababu nimeshakujua wewe ni nani kiitikadi,nakuuliza maswali kulingana na maelezo yako,je ina maana mpaka muda huu Allah hajamteua huyo mja wa kutoa huo utata ? Na kama bado wewe umejuaje hilo na unahisi huyo mja ni nani ? Al Mahdi au ? Jamaa acheni kudanganya watu,mtakuja kuulizwa kwa huu ujinga mnaoufanya mwa kuitukanisha dini ya Allah.


Hivi hata unachokiandika huwa unakihakiki ?

Kaka katika maelezo yangu humu nimekuuliza maswali kadhaa,naomba unijibu maswali yangu yote niliyokuuliza.

Pili,marejeo yote niliyokupa naomba ukayafatilie na uyasime kikamilifu.

Ninacho kukumbusha ni kuwa dini ya UISLAMU imekamilika na USHIA sio Uislamu bali ni dini pweke inayojitegemea na hakuna hata ibada moja ya kishia inayo fanana na ya Uislamu.

Kama kuna lolote nililokosea ni kwa udhaifu wangu na Allah aliye juu ametakasika na ukamilifu ni wake yeye.
ndo maana KIRANGA kila siku umu anasema icho mnachokiita kitabu kitakatifu quran ni kama hadithi za kipepe au ludilofa tu kwa maana kuna contraditions nyingi sana

siku mkifanikiwa kusolve hizo contradictions nyinyi kwa nyinyi basi KIRANGA atawaelewa lakin nyie wenyewe hamuelewani who is KIRANG mpaka hawaelewe ahahhahaha
 
ndo maana KIRANGA kila siku umu anasema icho mnachokiita kitabu kitakatifu quran ni kama hadithi za kipepe au ludilofa tu kwa maana kuna contraditions nyingi sana

siku mkifanikiwa kusolve hizo contradictions nyinyi kwa nyinyi basi KIRANGA atawaelewa lakin nyie wenyewe hamuelewani who is KIRANG mpaka hawaelewe ahahhahaha
Sawa mkuu.
 
ndo maana KIRANGA kila siku umu anasema icho mnachokiita kitabu kitakatifu quran ni kama hadithi za kipepe au ludilofa tu kwa maana kuna contraditions nyingi sana

siku mkifanikiwa kusolve hizo contradictions nyinyi kwa nyinyi basi KIRANGA atawaelewa lakin nyie wenyewe hamuelewani who is KIRANG mpaka hawaelewe ahahhahaha
Contradiction zipi? Sio Kwamba nyie ndio mnakitafutia contras ajili ya kujustify Ego zenu
 
Hapa ndio inakuja maana ya kwenye Biblia kwamba kwa Mungu siku Moja ni sawa na miaka elfu moja kwetu. Kumbe ni issue ya time travel
Mkuu usidanganyike na huo msemo eti kwa mungu siku elfu blah blah sio kweli hata kidogo
 
SALUTE
Mara nyingi huwa nasema vitu tunavyoona ni vya kijinga havi-make sense machoni na masikioni mwetu ndio huwa na maana na vimeleta mabadiliko makubwa duniani kwetu. Mfano swali la kijinga zaidi alilowahi kujiuliza mwanasayans Issac Newton leo hii limetulitea mabadiriko na maendeleo kwenye maisha, hebu fikiria kama leo hii isac newton angekuuliza kwanini apple limemuangukia kichwani halikwenda juu ungemuona vipi? Hilo swali unaloliona la kijinga limeleta maendeleo makubwa sana.

Pia ndoto moja aliyoota albert Einstein waweza kuona ni ya kawaida sana au haina maana lakini ni moja kati ya ndoto iliyoleta mafanikio makubwa duniani, kupitia ndoto tu ya kawaida sana aliyoota tulipata kitu kinachoitwa Theory of Ralativity mambo ya Emc2 yote yote unaweza ona ni kitu cha kawaida ila kina impact kubwa kwenye tasnia ya sayansi

Tarehe 11/5/2019 nilibahatika kuangalia muvi hii inayoitwa Avangers: Endgame, content iliyomo kwenye muvi hii ni Time Traveling, baada ya kuangalia muvi I really admitted that Death might no longer a threat to Mankind!.. Baada ya thanos ku-wipe nusu binaadamu wote ulimwenguni (Universe) , njia pekee iliyobakia kutimka ili kuwarudisha wale waliopotea. Probably Human can stop his Destiny which is Death, Nawaza tu labda Binaadamu twaweza kukiepuka na kukizuia kifo kwa kutumia Theory ya Time Traveling.

Time Travel ni nini?
Ni kitendo cha kusafiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine ndani ya muda, namaanisha kua mtu anaweza kusafiri leo hii kwenda miaka 5,10,20,25 nk ijayo (Future) au kusafiri kurudi miaka 10,20,30,40,nk iliyopita (Past). Hadithi nyingi za zamani zimekua zikielezea swala hili la kusafiri katika muda.

Huko India kuna hadithi inamzungumzia mfale Raivata Kakudumi ambae alisafiri kwenda mbinguni kukutana na mung wake Brahma, aliporudi alishangaa kua ni miaka mingi imepita. Japan pia kuna hadithi inaitwa Nihongi, inamwelezea kijana mmoja mvuvi anayeitwa Urashima taro ambae alitembelea sehemu iliyochini ya maji, baada ya siku tatu alirudi kijijini kwake akakuta ni miaka 300 imepita, alikuta familia yake imefariki yote. Pia kwa wayahudi mnamo karne ya 1BC mwanafunzi aitwae Honi ha-M'agel inasemekana ailisinzia kwa muda wa miaka 27 alipoamka alikuta hakuna mtu aliyemjua sehemu aliyokua anaishi. Na simulizi nyingii sana kuhusu hii nadharia zimetolewa waweza tafuta ukasoma zaidi.

Wakati watu wengi wakidhani kua muda hautofautiani lakini Mwanasayansi Albert Einstein anaelezea kua muda (Time) haupo hivyo wanavyodhani, unaweza kutofautiana kwa mazingira tofauti, kutegemeana na kasi unayotembea nayo angani (in space)…Theory of special relative ya Enstein inasema kua muda kwenda haraka au kwenda taratibu inategemea na kasii unavyo safiri, mtu akisafiri kwa kasi ya mwanga kwa chombo cha anga angani umri wake utakua mdogo kulinganisha na ndugu au wazazi wake aliowaacha angani..kama akirudi yeye atakua kijana lakini nduguze watakua wamezeeka au wakawa wameshafariki.

Pia kwenye theory ya Albert Einstein ya Theory of General relativity anaelezea kua Garvity (kani ya uvutano) inaweza kupeleka muda mbele au kurudisha nyuma. Anaeleza kua chombo cha anaga kikiwa huko anagani kikakutana na kani ya uvutano basi hua kani hiyo husababisha muda kua slow, hivyo basi hata wanasayansi wa anaga wanakubali kua wasafiri wa anga wanaporudi duniani hua wapo nyuma kimuda yaani saa ya duniani inakua mbele kwa muda microsecond 38 kwa siku. Wanahitimisha kwa kusema mfano msafiri mmoja wa anaga ana pacha wake duniani ammbae hafu akikaa huko angani labda siku 14, Yule pacha aliyebaki duniani atamshinda kwa muda wa microsecond 532 (chukua Microsecond 38 zidisha siku 14)

TIME MACHINE
Ili kufanikisha kusafiri katika muda inabidi kuwe na kifaa kinachoiitwa Time machine ambacho hichi kifaa kinauwezo wa kupeleka muda mbele au kurudisha muda nyuma. Bado wanasayansi wanalifanyia kazi suala hili, muda sio mrefu inaweza kuthibishwa kua Time machine inaweza kuanza kufanya kazi. Jinsi Nadharia ya Time Machine inavyofanya kazi kiukweli inanishinda kuielezea kwa Kiswahili kutokana na Ambiguity ya lugha yetu hii. Humo ni masuala ya physics tu so nashindwa niwekeje kwa lugha yetu labda aliyesoma hii kitu akaelewa inavyofanya kazi atatuelezea lifecoded.

Kwenye hili suala la tme Travel kuna kitu kinaitwa Grandfather Paradox ambapo hiki ni kitendo ambacho Time Traveller anarudi kwenye wakati uliopita kisha anaua wazazi wake au babu zake ili yeye awe hakuzaliwa.Kwa mujibu wa wanasayansi na wanafalasafa kama Plato kwenye theory yake ya Platonism anasema kua kubadili maisha yako ya nyuma hakuwezi kuathiri maisha yako ya sasa, lakini mambo yote hayo mawili yanakuja kupingwa na nadharia ya Butterfly Effectt ambapo inasema kua mabadiriko kidogo kwenye sehemu moja yanaweza kuleta mabadiriko makubwa au utofauti mkubwa baadae katika sehemu nyingine

Hii inamaanisha kwamba kama time traveler akirudi katika maisha yaliyopita akamuua baba aua babu yake anaweza sababisha mabadiriko katika maisha yake aliyotoka au future yake.

Kwa muhtsari huu kuhusu theory ya Time Traveling iko hivo japo watafiti wengi wanasema Time Travel hauwezekani iko too theoretically ila mimi naona hiki kitu ni real kabisa kipo, kwanini? Unajua binaadamu hawezi kufikiri nje ya vitu ambavyo vipo duniani nikimaanisha kuwa hata mimi au wewe hatuwezi kuwaza au kufikiri nje ya vile vitu tulivyoviona, kuambiwa au viliwahi kuwepo.

Utawaza Mungu kwakuwa ulisikia kuwa kuna Mungu, utawaza nyumba kwakua ushaiona nyumba nk nk. Mantiki yangu ni kwamba hata hao watu wanaosema time travel is real hawakukaa tu wakafikiri kitu amabacho hakipo, mtazamo wangu naamini hiki kitu kipo na kinafanya kazi labda kwa siri kumbuka hata Internet tunaambiwa imeletwa mwaka 1991 na Tim Berners lee lakini ni kitu kipo toka miaka ya 1950s sema Tim aliifanya kua Popular baada ya kutengeneza World Wide Web.

Lakini haya ni mawazo yangu tu kwamba labda kama Time Machine ikifanikiwa kutengenezwa watu wanaweza kuitumia kukwepa kifo labda kwa kurudisha muda nyuma na kukwepa kile kitu kilichopelekea kufariki..kwa mafano kwenye muvi inaitwa Time Trveler’s wife wameelezea tukio hili linavyoweza kufanyika.
~Da'vinci..
Mungu amesema sitashindana na Binadamu milele miaka yake itakuwa mia na ishirini maximum.Wewe Da'Vinci na wote wanaodhani mwanadamu anaweza kushindana na Mungu mnajidanganya.Mungu ameshasema mwanadamu atakufa na atakufa.That is sealed.

Unajua,hizi zote ni hila za Lucifer a.k.a the Devil or Satan kuonyesha kwamba aliyosema Mungu ni uongo.Mungu habadiliki, wala si mwanadamu hata aseme uwongo.Nia ya Shetani ni kupotosha na kugeuza imani ya Binadamu towards him.
Narudia tena kwa wale waliokuja JF kujifunza na kutafuta knowledge ya kweli,this is not true knowledge.Hizi ni hila ovu za wazi za Shetani za kutenganisha Wanadamu na Mungu wao.Msiamini this nonsense,it is pure heresy.
 
Mungu amesema sitashindana na Binadamu milele miaka yake itakuwa mia na ishirini maximum.Wewe Da'Vinci na wote wanaodhani mwanadamu anaweza kushindana na Mungu mnajidanganya.Mungu ameshasema,mwanadamu atakufa atakufa.That is sealed.

Unajua,hizi zote ni hila za Lucifer a.k.a the Devil or Satan kuonyesha kwamba aliyosema Mungu ni uongo.Mungu habadiliki, wala si mwanadamu hata aseme uwongo.Nia ya Shetani ni kupotosha na kugeuza imani ya Binadamu towards him.
Narudia tena kwa wale waliokuja JF kujifunza na kutafuta knowledge ya kweli,this is not true knowledge.Hizi ni hila ovu za wazi za Shetani za kutenganisha Wanadamu na Mungu wao.Msiamini this nonsense,it is pure heresy.
Time Travel ni ushetani mkuu??
 
Kwa mara ya kwanza, hospitali moja nchini Uhispania imeweza kupandikiza mapafu ya binadamu kwa kutumia mbinu ya upasuaji wa roboti aliyepewa jina la "Da Vinci".
IMG_20230426_125319.jpg
 

Similar Discussions

81 Reactions
Reply
Back
Top Bottom