Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,299
- 33,082
Kua kwenye diet kunafanya nitafute namna mbalimbali ya kula na kuenjoy vyakula ninavyovipenda.Bila kuharibu juhudi zangu za kupunguza uzito.
katika glasi ni mchanganyiko wa Maziwa mgando,tikiti maji na asali
Napenda sana tikiti maji lakini baada ya kula kwa wiki tatu mfululizo ladha yake imeanza kunichosha.leo katika juhudi za kumalizia kipande kilichobaki niliamua kulichanganya kwenye maziwa mgando.
Nimependa sana Ladha yake na nime-enjoy kula.Hii imenipa sababu yakuendelea kula tikiti maji kwa wiki nyingine moja ,uku nikiendelea kuongeza namna mbalimbali za kuenjoy tunda hili.
Mahitaji
1.weka maziwa kwenye glasi ,ongeza asali kisha korogo ili kuchanganya.
2.chukua glasi nyingine weka vipande vichache vya kitiki maji kisha mimina maziwa kiasi.kisha weka tena matunda na uweke maziwa juu fanya hivyo adi glasi ijae
3.Mwisho kabisa kwa juu,weka vipande vya tikiti maji kisha Nyunyuzia asali.Weka frijini kwa muda kidogo ili iwe baridi.tayari kwa kula.
Maelezo ya ziada
sikuweka vipimo kamili,kua huru kuweka kiasi utakacho.Kwa wale wenzangu tunaopunguza
uzito,jali kiasi cha maziwa unayokunywa na kiasi cha asali unachotumia.Nashauri utumie
nusu ya paketi ya maziwa (Tanga fresh) na asali kijiko kimoja cha chakula.kama kawaida
pima kiasi kwa kuzingatia diet yako.
Unaweza kutumia Nsizi mbivu badala ya tikiti maji au laa ukachanganya matunda yote mawili.
katika glasi ni mchanganyiko wa Maziwa mgando,tikiti maji na asali
Napenda sana tikiti maji lakini baada ya kula kwa wiki tatu mfululizo ladha yake imeanza kunichosha.leo katika juhudi za kumalizia kipande kilichobaki niliamua kulichanganya kwenye maziwa mgando.
Nimependa sana Ladha yake na nime-enjoy kula.Hii imenipa sababu yakuendelea kula tikiti maji kwa wiki nyingine moja ,uku nikiendelea kuongeza namna mbalimbali za kuenjoy tunda hili.
Mahitaji
- Maziwa mgando-Nimetumia Tanga fresh
- Asali
- Tikiti maji-kata vipande vidogo
1.weka maziwa kwenye glasi ,ongeza asali kisha korogo ili kuchanganya.
2.chukua glasi nyingine weka vipande vichache vya kitiki maji kisha mimina maziwa kiasi.kisha weka tena matunda na uweke maziwa juu fanya hivyo adi glasi ijae
3.Mwisho kabisa kwa juu,weka vipande vya tikiti maji kisha Nyunyuzia asali.Weka frijini kwa muda kidogo ili iwe baridi.tayari kwa kula.
Maelezo ya ziada
sikuweka vipimo kamili,kua huru kuweka kiasi utakacho.Kwa wale wenzangu tunaopunguza
uzito,jali kiasi cha maziwa unayokunywa na kiasi cha asali unachotumia.Nashauri utumie
nusu ya paketi ya maziwa (Tanga fresh) na asali kijiko kimoja cha chakula.kama kawaida
pima kiasi kwa kuzingatia diet yako.
Unaweza kutumia Nsizi mbivu badala ya tikiti maji au laa ukachanganya matunda yote mawili.