Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,592
- 29,721
Kampuni za simu nilizotaja hapo juu zinagawana wingi wa wateja ktk soko la mitandao ya simu nchini.
Ili kuwamotisha wateja kampuni hizi zimekuwa zinaandaa na kuendesha bahati na sibu mbali mbali huku zikitoa zawadfi kubwa kubwa za kuvutia.
Nimekuwa nafuatilia tangu mwanzo wa gamming zao ambapo kila mshindi anayetajwa au kufikiwa live anaonesha dalili ya kuandaliwa ama kuarifiwa kabla kuhusu ushindi wake. Pia washindi hawa ni kama wameandaliwa maana most of washindi kama hawajatokea dar es salaam basi ni mikoa ya kati (wachache) na kaskazini. mikoa ya kusini ni kama hawatumii mitandao hii ambayo mashindano yake hujiendesha automatic kwa mteja kujiunga. Sijasikia mshindi wa nyumba, gari, hela kuubwa katoka mtwara, lindi, ruvuma, au kusini kusini. washindi wengi ni dar to kaskazini. Pia hivi karibuni hizi kampuni zimepunguza bei za mawasiliano lakini ndo zimezidisha lottery kwa mfumo wa kuuliza maswali na kujibu ili kujiongezea points. Maswali yao yanakujia pale tu simu yako ikiwa na vocha tu na si vinginevyo.
Nimejaribu kuuliza watu wengi kama wanawafahamu ndugu, jamaa au rafiki zao waliowahi kushinda hizi promosheni majibu yanakatisha tamaa kuwa hawafahamu. Ila pia hizi kampuni zimejiingiza ktk mtego wa matangazo ya promosheni zao. Wanaposema VIGEZO NA MASHARTI KUZINGATIWA mbona hawasemi ni vigezo gani au masharti gani yanayozingatiwa? kama wanaweza kutuma wito wa kujiunga na maswali lukuki kwa subscriber wanashindwa nini washindwe kutuma hivyo VIGEZO NA MASHARTI? kuna jamaa yangu alishawahi kufuatwa na meneja masoko wa kampuni moja ya simu akimtaka waingie mkataba wa kupitisha zawadi mikononi mwake kwa masharti ya kifisadi nashukuru jamaa alikataa baada ya kustukia hali halisi.
Kwa kuwa michezo hii husimamiwa na GAMMING BOARD (wakati wa uchezeshaji tu) inaleta picha kwamba serikali kupitia board hii inashiriki kuwahadaa na kuwaibia wateja wa mitandao hii. Kama Gamming Board inasmamia promosheni hizi kwa nini ishiriki mwishoni tu? nina dukuduku kadhaa
Ili kuwamotisha wateja kampuni hizi zimekuwa zinaandaa na kuendesha bahati na sibu mbali mbali huku zikitoa zawadfi kubwa kubwa za kuvutia.
Nimekuwa nafuatilia tangu mwanzo wa gamming zao ambapo kila mshindi anayetajwa au kufikiwa live anaonesha dalili ya kuandaliwa ama kuarifiwa kabla kuhusu ushindi wake. Pia washindi hawa ni kama wameandaliwa maana most of washindi kama hawajatokea dar es salaam basi ni mikoa ya kati (wachache) na kaskazini. mikoa ya kusini ni kama hawatumii mitandao hii ambayo mashindano yake hujiendesha automatic kwa mteja kujiunga. Sijasikia mshindi wa nyumba, gari, hela kuubwa katoka mtwara, lindi, ruvuma, au kusini kusini. washindi wengi ni dar to kaskazini. Pia hivi karibuni hizi kampuni zimepunguza bei za mawasiliano lakini ndo zimezidisha lottery kwa mfumo wa kuuliza maswali na kujibu ili kujiongezea points. Maswali yao yanakujia pale tu simu yako ikiwa na vocha tu na si vinginevyo.
Nimejaribu kuuliza watu wengi kama wanawafahamu ndugu, jamaa au rafiki zao waliowahi kushinda hizi promosheni majibu yanakatisha tamaa kuwa hawafahamu. Ila pia hizi kampuni zimejiingiza ktk mtego wa matangazo ya promosheni zao. Wanaposema VIGEZO NA MASHARTI KUZINGATIWA mbona hawasemi ni vigezo gani au masharti gani yanayozingatiwa? kama wanaweza kutuma wito wa kujiunga na maswali lukuki kwa subscriber wanashindwa nini washindwe kutuma hivyo VIGEZO NA MASHARTI? kuna jamaa yangu alishawahi kufuatwa na meneja masoko wa kampuni moja ya simu akimtaka waingie mkataba wa kupitisha zawadi mikononi mwake kwa masharti ya kifisadi nashukuru jamaa alikataa baada ya kustukia hali halisi.
Kwa kuwa michezo hii husimamiwa na GAMMING BOARD (wakati wa uchezeshaji tu) inaleta picha kwamba serikali kupitia board hii inashiriki kuwahadaa na kuwaibia wateja wa mitandao hii. Kama Gamming Board inasmamia promosheni hizi kwa nini ishiriki mwishoni tu? nina dukuduku kadhaa
- vigezi vipi na masharti vinahusika ktk promosheni hizi?
- namba za washiriki zinapoingizwa kwenye kompyuta ya promosheni nani anathibitisha?
- kwa nini washindi hawaoneshi kufurahia ama kuwa surprised na ushindi wao?
- kwa nini promosheni hizi zisikabidhiwe wakala kuziendesha? maana fairness haipo endapo kampuni zitajiendeshea bahatinasibu zao ambazo hushawishi ufisadi.