Malalamiko mbalimbali kuhusu mabadiliko ya vifurushi yaliyofanywa na mtandao wa Tigo kwa mwaka 2020

Habari

NB: uzi huu hauchochei/ kutangaza mtandao wowote bali ni maoni tu.

Nimekuwa mtumiaji pendwa wa mtandao wa simu wa Tigo kwa miaka mingi kutokana na huduma zao kuwa bora (kwa maeneo niliopo) ikiwa ni pamoja na internet yenye kasi ya kuridhisha vilevile kupitia vifurushi vyenye gharama rafiki (kwangu mimi) hivyo kuniweza kupata sms, dakika na bando za intaneti kwa nyakati husika.

Tukiachilia mbali sifa mbalimbali mtandao wa simu wa Tigo umejipatia kumetokea na sintofahamu kwa siku za hivi karibuni ambapo vifurushi mbalimbali vya Tigo kuongezeka bei tofauti na mwanzo

Mfano 1: GB 1 iliuzwa kwa shilingi 1000 hivi saaa ni 3000
Mfano 2: SMS 3000 ulipata kwa shilingi 1000 hivi sasa unapata sms 1000 kwa shilingi 1000

Na vifurushi vingine vingi zaidi kubadilika

Maoni yangu:

- Baada ya mtandao wa simu wa Tigo kuweka kifurushi cha combo chenye dakika nyingi pia wajaribu kupunguza bei Za vifurushi(bei sio rafiki)/kurejesha vifurushi vilivyokuwepo wiki kadhaa nyuma

- Kuboresha vifurushi vya internet kwani bei na vifurushi haviendani hata kidogo.

- Matumizi ya data yarandane na kifurushi (Nikiangalia data usage kwa siku husika kama ni 1GB na kifurushi changu kiwe kimeisha Kwa 1GB kwani muda mwingine utakuta tofauti data usage 1GB ila kifurushi cha 3Gb kimetumika)

All in all ni maoni tu sio kwa ubaya ni kwa uboreshaji tu...
 
Bila shaka utakuwa unatembea sana na vifurushi vya ofa.

Nadhani vifurushi vikubwa ndio wamepunguza vya Wiki na Mwezi... kawaida yangu huwa data (internet) nanunua kifurushi chake na voice kifurushi chake.

Kwa upande wangu naona gharama zimeshuka compared na hapo kabla.
 
Watu hao wa pwani waliipenda sababu ya unafuu na vile walijibu mahitaji ya vijana kinyume na hapo wasingeweza.

By the way pwani Kuna idadi kiasi gani ya watu hadi I-guarantii survival ?
Naona leo baada ya kulalamikiwa sana wameamua kufanya mabadiliko
 
kweli mkuu wamerekebisha nilikuwa sijaona mana niliwapotezea tangu ijimaa hata kwangu kwenye size yako wamebadilisha mana ijumaa nilitaja kujiunga nikakuta vifurushi vya kise kinoma wametoa ile ofa ya uniofa
nikanyuti sijajiunga na nikaapa nitakuwa napokea tu simu na kusms nikahamia halotel Call na intenet y
ila now wameleta deal nzuri Size yako hapo sawa tigo tupo pamoja nyinyi tigo rafiki zangu tangu 2005 nilikuwa tayari niachane na nyinyi na nilienda kurenew line yangu ya halotel ila now tutaendelea
kwa ofa hiiView attachment 1337737

Sent using Jamii Forums mobile app
Duh! Mbona wamekupendelea hivi! Hahahaha. Wanatumia vigezo gani kuwapendelea wengine kwenye hiyo "Size yako". Mimi wamenionea balaa...ahhahaha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mambo ya vodacom hayo. Hadi raha yani.
Screenshot_20200128-110454.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unapigwa hapo, huku airtel kwa buku 10 tunapewa dakika elfu tatu kupiga airtel-airtel na dakika 100 mitandao yote kwa siku 30. Halafu hayo mambo ya kufosiana kuongea saa nne za usiku mpaka saa kumi na moja ya alfajiri yameshapitwa na wakati. Kwa vifurushi vya maongezi airtel wako vizuri kuliko mitandao yote. Kwa vifurushi vya data halotel anaongoza.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unapigwa hapo, huku airtel kwa buku 10 tunapewa dakika elfu tatu kupiga airtel-airtel na dakika 100 mitandao yote kwa siku 30. Halafu hayo mambo ya kufosiana kuongea saa nne za usiku mpaka saa kumi na moja ya alfajiri yameshapitwa na wakati. Kwa vifurushi vya maongezi airtel wako vizuri kuliko mitandao yote. Kwa vifurushi vya data halotel anaongoza.

Sent using Jamii Forums mobile app
Upo sawa...eti unamaongezi na mtu unasubiri mpaka ifike saa nne usiku...Tigo wamekuwa wa hovyo sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu salam za asubuhi hope ziko poa kwenu na mmeamka salama ila mimi hapana nimelala kwa taabu sana jana na joto la jiji hili.

Kisa hawa Tigo wametubadilishia vifurushi na kuweka gharama juu isio mkidhi mlaji. Lakini bado hawajachoka sasa hivi wamekuja na mpya

Unanunua kitu kupitia Tigopesa na pesa ipo ila unaambiwa huna salio la kutosha nimenunua umeme jana asubuhi hadi leo kimya kikuu. Ukipiga numbers zao wapo busy kibaya taarifa za mabadiliko hawajatoa wala nini sasa kilichobaki sasa hivi.

Nikuja na #hashtag #ott operation tokomeza Tigo. Kama wana hasira na line zao kuwekwa ban ni jukumu la kudeal na Serikali sio Wananchi walalahoi.

FB_IMG_1580282812131.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom