stickvibration
JF-Expert Member
- Feb 7, 2017
- 3,227
- 5,132
Mimi ni mteja wa hii kampuni kuanzia Tritel hadi kampuni kuuzwa kwenda Mobitel pia kampuni ikauzwa kwenda Buzz hadi leo hii kufikia kampuni kuitwa TIGO. Mimi yule yule nipo tu na hata namba ni ile ile tu.
Tatizo kubwa ni pale nikitaka kujiunga Siku Bonus ya Internet napata ofa ya 2000=1GB kwa siku lakini nikitaka kujiunga INTERNET kwa kupitia Tigo Niwezeshe ya Sh. 2000 hiyo hiyo napata 2.5 GB kwa siku kisha nalipa Sh. 2400(400 ni interest).
Sasa inakuwaje mnatulazimisha kujiunga kwa tigo niwezeshe? Je, ni ili tulipe hiyo riba?
Maana Tigopesa ninayo hela ya kutosha lakini bila kupitia Tigo Niwezeshe naambulia 1 GB tu.
Tuangalieni kwa macho ya tofauti sisi ambao imani zetu haziruhusu kukopa ama kukopesha kwa riba ukizingatia sisi ni wateja wenu wakongwe!
Tatizo kubwa ni pale nikitaka kujiunga Siku Bonus ya Internet napata ofa ya 2000=1GB kwa siku lakini nikitaka kujiunga INTERNET kwa kupitia Tigo Niwezeshe ya Sh. 2000 hiyo hiyo napata 2.5 GB kwa siku kisha nalipa Sh. 2400(400 ni interest).
Sasa inakuwaje mnatulazimisha kujiunga kwa tigo niwezeshe? Je, ni ili tulipe hiyo riba?
Maana Tigopesa ninayo hela ya kutosha lakini bila kupitia Tigo Niwezeshe naambulia 1 GB tu.
Tuangalieni kwa macho ya tofauti sisi ambao imani zetu haziruhusu kukopa ama kukopesha kwa riba ukizingatia sisi ni wateja wenu wakongwe!